< Revelation 2 >
1 To the angel of the church in Ephesus write: These things saith he that holdeth the seven stars in his right hand, who walketh in the midst of the seven golden candlesticks:
“Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
2 I know thy works, and thy labor, and thy endurance, and that thou canst not bear evil men; and thou didst try those who say they are apostles, and are not, and didst find them liars;
Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
3 and thou hast endurance, and hast borne on account of my name, and hast not become weary.
Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
4 But I have this against thee, that thou hast left thy first love.
Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
5 Remember therefore whence thou hast fallen, and repent, and do the first works; or else I will come to thee, and will remove thy candlestick out of its place, unless thou repent.
Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
6 But this thou hast, that thou hatest the deeds of the Nicolaitans, which I also hate.
Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
7 He that hath an ear, let him hear what the Spirit saith to the churches. To him that overcometh I will give to eat of the tree of life, which is in the paradise of my God.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
8 And to the angel of the church in Smyrna write: These things saith the first and the last, who was dead, and lived again:
“Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
9 I know thy affliction and poverty, (but thou art rich, ) and the blasphemy of those who say they are Jews, and are not, but are a synagogue of Satan.
Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
10 Fear not the things which thou art about to suffer. Behold, now, the Devil is about to cast some of you into prison, that ye may be tried; and ye will have tribulation ten days. Be thou faithful unto death, and I will give thee the crown of life.
Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
11 He that hath an ear, let him hear what the Spirit saith to the churches. He that overcometh shall not be hurt by the second death.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
12 And to the angel of the church in Pergamus write: These things saith he that hath the sharp two-edged sword:
“Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: “Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
13 I know where thou dwellest, where the throne of Satan is; and thou holdest fast my name, and didst not deny my faith, even in the days in which Antipas was my witness, my faithful one, who was slain among you, where Satan dwelleth.
Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
14 But I have a few things against thee; thou hast there them that hold the teaching of Balaam, who taught Balak to put a stumbling-block in the way of the sons of Israel, and to eat things sacrificed to idols, and to commit fornication.
Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
15 So thou also hast men holding the teaching of the Nicolaitans, in like manner.
Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
16 Repent therefore; or else I will come to thee quickly, and will make war with them with the sword of my mouth.
Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
17 He that hath an ear, let him hear what the Spirit saith to the churches. To him that overcometh, I will give of the hidden manna, and will give him a white stone, and on the stone a new name written, which no one knoweth but he that receiveth it.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
18 And to the angel of the church in Thyatira write: These things saith the Son of God, who hath his eyes like a flame of fire, and his feet are like fine brass:
“Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: “Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
19 I know thy works, and love, and faith, and service, and thy endurance, and that thy last works are more than the first.
Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
20 But I have this against thee, that thou sufferest thy wife Jezebel, who calleth herself a prophetess, and she teacheth and seduceth my servants to commit fornication, and to eat things sacrificed to idols.
Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
21 And I gave her time to repent, and she will not repent of her fornication.
Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
22 Behold, I will cast her into a bed, and those who together with her commit adultery into great distress, unless they repent of her deeds.
Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
23 And her children I will slay with death; and all the churches shall know that I am he who searcheth the reins and hearts; and I will give to every one of you according to your works.
Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
24 But to you I say, the rest who are in Thyatira, as many as have not this teaching, such as have not known “the depths” of Satan, as they speak; I put upon you no other burden;
“Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
25 but that which ye have, hold fast till I come.
Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
26 And he that overcometh, and he that keepeth my works to the end, to him I will give authority over the nations, —
“Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
27 and he shall rule them with a rod of iron, as the vessels of a potter are broken to shivers, —as I also have received of my Father.
Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
28 And I will give him the morning star.
Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
29 He that hath an ear, let him hear what the Spirit saith to the churches.
“Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!