< Psalms 56 >
1 “For the leader of the music. To be sung to the tune of “The dumb dove among strangers.” A psalm of David, when the Philistines took him in Gath.” Have pity upon me, O God! for man panteth for my life; My adversary daily oppresseth me!
Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
2 Mine enemies daily pant for my life, And many are they who war proudly against me.
Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
3 When I am in fear, I will put my trust in thee!
Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
4 Through God shall I praise his word; In God do I put my trust; I will not fear; What can flesh do to me?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
5 Every day they wrest my words; All their thoughts are against me for evil.
Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
6 They gather themselves together, they hide themselves, they watch my steps, Lying in wait for my life.
Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
7 Shall they escape by their iniquity? In thine anger cast down the people, O God!
Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
8 Count thou my wanderings; Put my tears into thy bottle! Are they not recorded in thy book?
Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
9 When I cry to thee, my enemies shall turn back; This I know, that God is for me.
Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
10 Through God shall I praise his word; I shall glory in the promise of Jehovah.
Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
11 In God do I put my trust; I will not fear: What can man do to me?
katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
12 Thy vows are upon me, O God! I will render praises to thee!
Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
13 For thou hast delivered me from death, Yea, my feet from falling, That I may walk before God in the light of the living.
Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.