< Psalms 56 >

1 “For the leader of the music. To be sung to the tune of “The dumb dove among strangers.” A psalm of David, when the Philistines took him in Gath.” Have pity upon me, O God! for man panteth for my life; My adversary daily oppresseth me!
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 Mine enemies daily pant for my life, And many are they who war proudly against me.
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 When I am in fear, I will put my trust in thee!
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 Through God shall I praise his word; In God do I put my trust; I will not fear; What can flesh do to me?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 Every day they wrest my words; All their thoughts are against me for evil.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 They gather themselves together, they hide themselves, they watch my steps, Lying in wait for my life.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 Shall they escape by their iniquity? In thine anger cast down the people, O God!
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 Count thou my wanderings; Put my tears into thy bottle! Are they not recorded in thy book?
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 When I cry to thee, my enemies shall turn back; This I know, that God is for me.
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 Through God shall I praise his word; I shall glory in the promise of Jehovah.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 In God do I put my trust; I will not fear: What can man do to me?
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 Thy vows are upon me, O God! I will render praises to thee!
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 For thou hast delivered me from death, Yea, my feet from falling, That I may walk before God in the light of the living.
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.

< Psalms 56 >