< Psalms 38 >

1 “A psalm of David. To bring to remembrance.” O LORD! rebuke me not in thy wrath, Nor chasten me in thy hot displeasure!
Zaburi ya Daudi. Maombi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.
2 For thine arrows have deeply pierced me, And thy hand hath been heavy upon me.
Kwa kuwa mishale yako imenichoma, na mkono wako umenishukia.
3 There is no soundness in my flesh, because of thine anger; Nor rest in my bones, because of my sin.
Hakuna afya mwilini mwangu kwa sababu ya ghadhabu yako, mifupa yangu haina uzima kwa sababu ya dhambi zangu.
4 For my iniquities have gone over my head; Like a heavy burden, they are more than I can bear.
Maovu yangu yamenifunika kama mzigo usiochukulika.
5 My wounds putrefy and are loathsome on account of my folly.
Majeraha yangu yameoza na yananuka, kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6 I am bent; I am bowed down greatly; I go mourning all the day long.
Nimeinamishwa chini na kushushwa sana, mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.
7 For my loins are full of burning heat, And there is no soundness in my flesh.
Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo, hakuna afya mwilini mwangu.
8 I am weakened and bruised exceedingly; I roar by reason of the disquietude of my heart.
Nimedhoofika na kupondwa kabisa, nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.
9 O Lord! thou knowest all my desire, And my groaning is not hidden from thee!
Ee Bwana, yote ninayoyaonea shauku yako wazi mbele zako, kutamani kwangu sana hakufichiki mbele zako.
10 My heart panteth; my strength faileth me; The very light of my eyes is gone from me.
Moyo wangu unapigapiga, nguvu zangu zimeniishia; hata macho yangu yametiwa giza.
11 My friends and acquaintance keep aloof from my woe, And my kinsmen stand afar off:
Rafiki na wenzangu wananikwepa kwa sababu ya majeraha yangu; majirani zangu wanakaa mbali nami.
12 While they who seek my life lay snares for me; They who seek my hurt threaten destruction, And meditate deceit all the day long.
Wale wanaotafuta uhai wangu wanatega mitego yao, wale ambao wangetaka kunidhuru huongea juu ya maangamizi yangu; hufanya shauri la hila mchana kutwa.
13 But I, like a deaf man, hear not; And, like a dumb man, open not my mouth.
Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia, ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,
14 I am like one who heareth nothing, And in whose mouth is no reply.
nimekuwa kama mtu asiyesikia, ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.
15 For in thee, O LORD! do I put my trust; Thou wilt hear, O Lord, my God!
Ee Bwana, ninakungojea wewe, Ee Bwana Mungu wangu, utajibu.
16 For I have prayed, “Let them not rejoice over me; Let them not exult at the slipping of my feet!”
Kwa kuwa nilisema, “Usiwaache wafurahie, wala wasijitukuze juu yangu mguu wangu unapoteleza.”
17 For I am ready to fall, And my pain doth never leave me;
Kwa maana ninakaribia kuanguka, na maumivu yangu yananiandama siku zote.
18 For I confess my iniquity, And am troubled on account of my sin.
Naungama uovu wangu, ninataabishwa na dhambi yangu.
19 But my enemies flourish and are strong; They who hate me without cause are multiplied.
Wengi ni wale ambao ni adui zangu hodari, wale wanaonichukia bila sababu ni wengi.
20 They who repay good with evil are my enemies, Because I follow that which is good.
Wanaolipa maovu kwa wema wangu hunisingizia ninapofuata lililo jema.
21 Forsake me not, O LORD! O my God! be not far from me!
Ee Bwana, usiniache, usiwe mbali nami, Ee Mungu wangu.
22 Make hast to mine aid, O Lord, my salvation!
Ee Bwana Mwokozi wangu, uje upesi kunisaidia.

< Psalms 38 >