< Psalms 3 >
1 “A Psalm of David, when he fled from his son Absalom.” How many, O LORD, are mine enemies! How many are they who rise up against me!
Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
2 How many are they who say of me, “There is no help for him with God”! (Pause)
Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
3 But thou, O LORD! art my shield, My glory, and the lifter-up of my head.
Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
4 I call upon the LORD with my voice, And he heareth me from his holy hill. (Pause)
Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
5 I lay me down and sleep; I awake, for the LORD sustaineth me.
Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
6 I will not fear the ten thousands of people Who on every side set themselves against me.
Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
7 Arise, O LORD! Save me, O my God! For thou smitest the cheek of all my enemies; Thou breakest the teeth of the wicked.
Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
8 Deliverance cometh from the LORD: May thy blessing be with thy people! (Pause)
Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.