< Psalms 141 >
1 “For the leader of the music. A psalm of David.” I cry to thee, O LORD! make haste unto me! Give ear to my voice, when I cry unto thee!
Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
2 Let my prayer come before thee as incense, And the lifting-up of my hands, as the evening sacrifice!
Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
3 Set a watch, O LORD! before my mouth; Guard the door of my lips!
Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
4 Let not my heart incline to any evil thing; Let me not practise wickedness with the doers of iniquity, And let me not eat of their delicacies!
Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
5 Let the righteous smite me, —it shall be a kindness; Let him reprove me, and it shall be oil for my head; Let him do it again, and my head shall not refuse it; But now I pray against their wickedness!
Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
6 When their judges are hurled over the side of the rock, They shall hear how pleasant are my words.
Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
7 So are our bones scattered at the mouth of the underworld, As when one furroweth and ploweth up the land. (Sheol )
Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol )
8 But to thee do my eyes look, O Lord Jehovah! In thee is my trust; Let not my life be poured out!
Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
9 Preserve me from the snares which they have laid for me, And from the nets of evil-doers!
Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
10 Let the wicked fall together into their own traps, Whilst I make my escape!
Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.