< Psalms 140 >

1 “For the leader of the music. A psalm of David.” Deliver me, O LORD! from the evil man, Save me from the man of violence,
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
2 Who meditate mischief in their heart, And daily stir up war!
ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
3 They sharpen their tongues like a serpent; The poison of the adder is under their lips. (Pause)
Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
4 Defend me, O LORD! from the hands of the wicked, Preserve me from the man of violence, Who have purposed to cause my fall! (Pause)
Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
5 The proud have hidden snares and cords for me; They have spread a net by the way-side; They have set traps for me.
Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
6 I say to Jehovah, Thou art my God; Hear, O Jehovah! the voice of my supplication!
Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
7 The Lord Jehovah is my saving strength: Thou shelterest my head in the day of battle!
Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
8 Grant not, O LORD! the desires of the wicked; Let not their devices prosper; Let them not exalt themselves!
Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
9 As for the heads of those who encompass me, Let the mischief of their own lips cover them!
Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
10 Let burning coals fall upon them; May they be cast into the fire, And into deep waters from which they shall not arise!
Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
11 The slanderer shall not be established upon the earth; Evil shall pursue the violent man to destruction.
Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
12 I know that the LORD will maintain the cause of the afflicted, And the right of the poor.
Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
13 Yea, the righteous shall praise thy name; The upright shall dwell in thy presence!
Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.

< Psalms 140 >