< Psalms 11 >

1 “For the leader of the music. A psalm of David.” In the LORD do I put my trust. Why say ye to me, “Flee, like a bird, to your mountain?
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
2 For, lo! the wicked bend their bow; They make ready their arrows on the string, To shoot in secret at the upright in heart.
Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
3 If the pillars be broken down, What can the righteous do?”
Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
4 The LORD is in his holy palace; The LORD'S throne is in heaven; His eyes behold, his eyelids prove the children of men.
Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
5 The LORD trieth the righteous; But the wicked, and the lover of violence, his soul hateth.
Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
6 Upon the wicked he will rain lightning; Fire and brimstone and a burning wind shall be the portion of their cup.
Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
7 For the LORD is righteous; he loveth righteousness; The upright shall see his face.
Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.

< Psalms 11 >