< Proverbs 29 >
1 He who, being often reproved, hardeneth his neck, Shall suddenly be destroyed, and that without remedy.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 When the righteous are powerful, the people rejoice; But when the wicked beareth rule, the people mourn.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 He who loveth wisdom rejoiceth his father; But he who is a companion of harlots destroyeth his substance.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 A king by equity establisheth a land; But he who receiveth gifts overthroweth it.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 A man who flattereth his neighbor Spreadeth a net for his feet.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 In the transgression of a wicked man there is a snare; But the righteous shall sing and rejoice.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 A righteous man careth for the cause of the poor; A wicked man discerneth not knowledge.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Scoffers kindle a city into a flame; But wise men pacify wrath.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 If a wise man contend in a cause with a fool, Whether he rage or laugh, there will be no rest.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 The bloodthirsty man hateth the upright; But the righteous seek to preserve his life.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 A fool letteth all his anger come out; But a wise man keepeth it back.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 If a ruler listen to words of falsehood, All his servants become wicked.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 The poor man and the oppressor meet together: The LORD giveth light to the eyes of them both.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 The king that judgeth the poor with uprightness, His throne shall be established for ever.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 The rod and reproof give wisdom; But a child left to himself bringeth shame to his mother.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 When the wicked are powerful, transgression increaseth; But the righteous shall see their fall.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Chastise thy son, and he will give thee rest; Yea, he will give delight to thy soul.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Where there is no vision, the people become unruly; But he that keepeth the law, happy is he.
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 A servant will not be corrected by words; For, though he understand, he will not obey.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 Seest thou a man hasty in his words? There is more hope of a fool than of him.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 He that bringeth up his servant delicately from childhood Shall have him become a son at the last.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 An angry man stirreth up strife, And a passionate man aboundeth in transgression.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 A man's pride will bring him low; But he that is of a humble spirit shall obtain honor.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 He who shareth with a thief hateth himself: He heareth the curse, but maketh no discovery.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 The fear of man bringeth a snare; But whoso putteth his trust in the LORD shall be safe.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Many are they who seek the ruler's favor; But every man's judgment cometh from the LORD.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 As the unjust man is an abomination to the righteous, So the upright in his way is an abomination to the wicked.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.