< Proverbs 11 >

1 False scales are an abomination to the LORD; But a perfect weight is his delight.
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
2 When pride cometh, then cometh disgrace; But with the humble is wisdom.
Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
3 The integrity of the upright shall guide them; But the perverseness of transgressors shall destroy them.
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
4 Riches do not profit in the day of wrath; But righteousness delivereth from death.
Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5 The righteousness of the good man maketh his way plain; But the wicked falleth through his wickedness.
Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
6 The righteousness of the upright delivereth them; But transgressors are ensnared in their own mischief.
Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
7 When the wicked man dieth, his hope cometh to an end; Yea, the expectation of the unjust cometh to an end.
Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
8 The righteous man is delivered from trouble, And the wicked cometh into it in his stead.
Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
9 By his mouth the vile man destroyeth his neighbor; But by the knowledge of the righteous are men delivered.
Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
10 When it goeth well with the righteous, the city rejoiceth; And when the wicked perish, there is shouting.
Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
11 By the blessing of the upright the city is exalted; But it is overthrown by the mouth of the wicked.
Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
12 He who despiseth his neighbor is void of understanding; A man of discernment holdeth his peace.
Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
13 He who goeth about as a tale-bearer revealeth secrets; But he who is of a faithful spirit concealeth a matter.
Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
14 Where there is no counsel, the people fall; But in a multitude of counsellors there is safety.
Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
15 He that is surety for another shall smart for it; But he that hateth suretyship is sure.
Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
16 A graceful woman obtaineth honor, Even as strong men obtain riches.
Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
17 He that doeth good to himself is a man of kindness; But he that tormenteth his own flesh is cruel.
Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
18 The wicked toileth for deceitful wages; But he who soweth righteousness shall have a sure reward.
Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
19 As righteousness tendeth to life, So he who pursueth evil pursueth it to his death.
Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
20 The perverse in heart are the abomination of the LORD; But the upright in their way are his delight.
Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
21 From generation to generation the wicked shall not go unpunished; But the posterity of the righteous shall be delivered.
Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
22 As a jewel of gold in a swine's snout, So is a beautiful woman who is without discretion.
Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
23 The desire of the righteous is only good; But the expectation of the wicked is wrath.
Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
24 There is that scattereth, and yet increaseth; And there is that withholdeth more than is right, yet he cometh to want.
Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
25 The bountiful man shall be enriched, And he that watereth shall himself be watered.
Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
26 Him that keepeth back corn the people curse; But blessing shall be upon the head of him that selleth it.
Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
27 He, who earnestly seeketh good, seeketh favor; But he that seeketh mischief, it shall come upon him.
Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
28 He who trusteth in his riches shall fall; But the righteous shall flourish as a leaf.
Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29 He that harasseth his household shall inherit wind; And the fool shall be the servant of the wise.
Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
30 The fruit of a righteous man is a tree of life; And the wise man winneth souls.
Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
31 Behold, the righteous man is requited on the earth; Much more the wicked man and the sinner!
Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

< Proverbs 11 >