< Philemon 1 >
1 Paul, a prisoner of Christ Jesus, and Timothy the brother, to Philemon our beloved friend and fellow-laborer,
Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
2 and to the beloved Apphia, and to Archippus our fellow-soldier, and to the church in thy house:
na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
3 Grace be to you, and peace, from God our Father and the Lord Jesus Christ.
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
4 I thank my God at all times, making mention of thee in my prayers,
Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
5 hearing of thy love and faith, which thou hast toward the Lord Jesus and toward all the saints;
maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
6 that the fellowship of thy faith may become effectual in the knowledge of every good thing which is in us, for Christ Jesus.
Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
7 For we have great thankfulness and comfort on account of thy love, because the hearts of the saints have been refreshed by thee, brother.
Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
8 Wherefore, though I have much boldness in Christ to enjoin upon thee that which is befitting,
Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
9 yet for love's sake I beseech thee rather; being such a one as Paul an old man, and now also a prisoner of Christ Jesus,
Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
10 I beseech thee for my child, whom I begot in my bonds, Onesimus;
Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
11 who in time past was unprofitable to thee, but is now profitable to thee and to me;
Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
12 whom I have sent back; and do thou [[receive]] him, that is, my own flesh.
Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13 Whom I would have retained with me, that in thy stead he might minister to me in the bonds of the gospel;
Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
14 but I chose to do nothing without thy consent, that thy benefit may be not as from necessity, but willingly.
Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
15 For perhaps he was separated from thee for a season to this end, that thou shouldst receive him back as thine for ever; (aiōnios )
Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios )
16 no longer as a bond-servant, but above a bond-servant, a brother beloved, especially to me, but how much more to thee, both in the flesh, and in the Lord!
Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
17 If thou then regardest me as a partner, receive him as myself.
Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18 And if he wronged thee in anything, or oweth thee, put that to my account.
Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
19 I Paul have written it with my own hand, I will repay it; not to say to thee, that to me thou owest even thy own self besides.
Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
20 Yea, brother, let me have joy of thee in the Lord; refresh my heart in Christ.
Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
21 Having confidence in thy obedience I have written to thee, knowing that thou wilt do even more than I say.
Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
22 And at the same time make ready a lodging for me; for I hope that through your prayers I shall be granted to you.
Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
23 Epaphras, my fellow-prisoner in Christ Jesus,
Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
24 Mark, Aristarchus, Demas, Luke, my fellow-laborers, salute thee.
Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
25 The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit.
Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.