< Matthew 6 >
1 But take heed that ye do not your righteousness before men, to be seen by them; otherwise ye have no reward with your Father who is in heaven.
“Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo.
2 Therefore when thou doest alms, do not sound a trumpet before thee, as the hypocrites do in the synagogues and in the streets, that they may have glory of men. Truly do I say to you, They have received their reward.
“Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
3 But when thou doest alms, let not thy left hand know what thy right hand doeth;
Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya hivyo kwamba hata rafiki yako asijue ufanyalo.
4 that thine alms may be in secret; and thy Father, who seeth in secret, will reward thee.
Toa msaada wako kwa siri, na Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
5 And when ye pray, ye shall not be as the hypocrites are; for they love to pray standing in the synagogues and in the corners of the streets, that they may be seen by men. Truly do I say to you, They have received their reward.
“Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
6 But do thou, when thou prayest, enter into thy closet, and, when thou hast shut thy door, pray to thy Father who is in secret; and thy Father, who seeth in secret, will reward thee.
Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
7 But when ye pray, use not vain repetitions, as the heathen do; for they think that they shall be heard for the multitude of their words.
“Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.
8 Be not ye therefore like them; for your Father knoweth what things ye have need of, before ye ask him.
Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba.
9 After this manner therefore pray ye: —Our Father, who art in heaven, hallowed be thy name;
Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
10 thy kingdom come; thy will be done on earth as it is in heaven;
Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
11 give us this day our daily bread;
Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
12 and forgive us our debts, as we also have forgiven our debtors;
Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
13 and lead us not into temptation, but deliver us from evil.
Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
14 For if ye forgive men their trespasses, your heavenly Father will also forgive you;
“Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
15 but if ye do not forgive men, neither will your Father forgive your trespasses.
Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
16 Moreover, when ye fast, be not, as the hypocrites, of a sad countenance; for they disfigure their faces, that they may appear to men to be fasting. Truly do I say to you, They have received their reward.
“Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga. Nawaambieni hakika, hao wamekwisha pata tuzo lao.
17 But do thou, when thou fastest, anoint thy head, and wash thy face;
Wewe lakini unapofunga, paka kichwa chako mafuta, nawa uso wako,
18 that thou appear not to men to be fasting, but to thy Father who is in secret; and thy Father, who seeth in secret, will reward thee.
ili mtu yeyote asijue kwamba unafunga, ila ujulikane tu kwa Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika atakutuza.
19 Lay not up for yourselves treasures on earth, where the moth and rust consume, and where thieves break through and steal;
“Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.
20 but lay up for yourselves treasures in heaven, where neither moth nor rust consumeth, and where thieves do not break through nor steal.
Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba.
21 For where thy treasure is, there will thy heart be also.
Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
22 The eye is the lamp of the body. If thine eye he clear, thy whole body will be in light;
“Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga.
23 but if thine eye be disordered, thy whole body will be in darkness. If then the light that is within thee is darkness, how great that darkness!
Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga ulioko ndani yako ni giza, basi, hilo ni giza la kutisha mno.
24 No one can serve two masters; for either he will hate one, and love the other; or else he will cleave to one, and despise the other. Ye cannot serve God and mammon.
“Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
25 Therefore I say to you, Be not anxious for your life, what ye shall eat; nor yet for your body, what ye shall put on. Is not the life more than food, and the body than raiment?
“Ndiyo maana nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula na kinywaji mnavyohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu. Je, maisha ni chakula tu au zaidi? Na mwili, je, si zaidi ya mavazi?
26 Behold the birds of the air, that they sow not, nor reap, nor gather into barns; and your heavenly Father feedeth them. Are not ye of much greater value than they?
Waangalieni ndege wa mwituni: hawapandi, hawavuni, wala hawana ghala yoyoye. Hata hivyo, Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani kuliko hao?
27 But who of you by anxious thought can add to his life one cubit?
Ni nani miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi sana anaweza kuuongeza muda wa maisha yake?
28 And why are ye anxious about raiment? Consider the lilies of the field, how they grow. They toil not, neither do they spin;
“Na kuhusu mavazi, ya nini kuwa na wasiwasi? Tazameni maua ya porini jinsi yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayasokoti.
29 and yet I say to you, that not even Solomon in all his glory was arrayed like one of these.
Lakini nawaambieni, hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
30 And if God so clothes the herbage of the field, which today is, and tomorrow is cast into an oven, will he not much more clothe you, O ye of little faith?
Ikiwa basi Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatafanya zaidi kwenu ninyi? Enyi watu wenye imani haba!
31 Therefore be not anxious, saying, What shall we eat, or what shall we drink, or wherewith shall we he clothed?
“Basi, msiwe na wasiwasi: Tutakula nini, tutakunywa nini, tutavaa nini!
32 For after all these things do the gentiles seek; for your heavenly Father knoweth that ye have need of all these things.
Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote.
33 But seek first his kingdom, and his righteousness; and all these things will also be given you.
Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada.
34 Be not then anxious about the morrow; for the morrow will be anxious about itself. Sufficient for the day is the evil thereof.
Basi, msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.