< Matthew 19 >

1 And it came to pass, that when Jesus had ended these sayings, he removed from Galilee, and came into the borders of Judaea, beyond the Jordan.
Yesu alipomaliza kusema maneno haya, aliondoka Galilaya, akaenda sehemu za Uyahudi, ngʼambo ya Mto Yordani.
2 And great multitudes followed him; and he healed them there.
Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akawaponya huko.
3 And the Pharisees came to him, trying him, and saying, Is it lawful for a man to put away his wife for every cause?
Baadhi ya Mafarisayo wakamjia ili kumjaribu, wakamuuliza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”
4 And he answering said, Have ye not read, that he who made them at the beginning, made them male and female?
Akawajibu, “Je, hamkusoma kwamba hapo mwanzo Muumba aliwaumba mwanaume na mwanamke,
5 And He said: “For this cause shall a man leave father and mother, and cleave to his wife; and the two shall become one flesh.”
naye akasema, ‘Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’?
6 So they are no longer two, but one flesh. What therefore God joined together, let not man put asunder.
Hivyo si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
7 They say to him, Why then did Moses ordain that a man may give his wife a writing of divorcement, and put her away?
Wakamuuliza, “Kwa nini basi Mose aliagiza mtu kumpa mkewe hati ya talaka na kumwacha?”
8 He saith to them, Moses, on account of your hardness of heart, allowed you m put away your wives; but in the beginning it was not so.
Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo.
9 And I say to you, Whoever putteth away his wife, except for fornication, and marrieth another, committeth adultery.
Mimi nawaambia, yeyote amwachaye mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati naye akaoa mke mwingine, anazini. Naye amwoaye yule mwanamke aliyeachwa pia anazini.”
10 The disciples say to him, If such be the case of a man with his wife, it is not good to marry.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Kama hali ndiyo hii kati ya mume na mke, ni afadhali mtu asioe!”
11 But he said to them, All cannot receive this saying, but they only to whom it is given.
Yesu akawaambia, “Si watu wote wanaoweza kupokea neno hili, isipokuwa wale tu waliojaliwa na Mungu.
12 For there are eunuchs, who were so born from their mother's womb; and there are eunuchs, who were made eunuchs by men; and there are eunuchs, who made themselves eunuchs for the sake of the kingdom of heaven. He that is able to receive it, let him receive it.
Kwa maana wengine ni matowashi kwa sababu wamezaliwa hivyo; wengine wamefanywa matowashi na wanadamu; na wengine wamejifanya matowashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.”
13 Then there were brought to him children, that be might lay his hands on them, and pray; and the disciples rebuked them.
Kisha watoto wadogo wakaletwa kwa Yesu ili aweke mikono yake juu yao na awaombee. Lakini wanafunzi wake wakawakemea wale waliowaleta.
14 But Jesus said to them, Suffer the children, and forbid them not to come to me; for to such belongeth the kingdom of heaven.
Yesu akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mbinguni ni wa wale walio kama hawa.”
15 And he laid his hands on them, and departed thence.
Naye akaweka mikono yake juu yao, na akaondoka huko.
16 And lo! one came to him and said, Teacher, what good thing shall I do, that I may have everlasting life? (aiōnios g166)
Mtu mmoja akamjia Yesu na kumuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
17 And he said to him, Why dost thou ask me concerning what is good? There is but one who is good. But if thou wilt enter into life, keep the commandments.
Yesu akamjibu, “Mbona unaniuliza habari ya mema? Aliye mwema ni Mmoja tu. Lakini ukitaka kuingia uzimani, zitii amri.”
18 Which? saith he. And Jesus said, These: “Thou shalt not kill; Thou shalt not commit adultery; Thou shalt not steal; Thou shalt not bear false witness;
Yule mtu akamuuliza, “Amri zipi?” Yesu akamjibu, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,
19 Honor thy father and thy mother;” and, “Thou shalt love thy neighbor as thyself.”
waheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama nafsi yako.”
20 The young man saith to him, All these things have I kept; in what am I still wanting?
Yule kijana akasema, “Hizi zote nimezishika. Je, bado nimepungukiwa na nini?”
21 Jesus said to him, If thou wilt be perfect, go, sell what thou hast, and give to the poor, and thou shalt have treasure in heaven; and come, follow me.
Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze vitu vyote ulivyo navyo, na hizo fedha uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
22 But the young man, on hearing this went away sorrowful; for he had great possessions.
Yule kijana aliposikia hayo, akaenda zake kwa huzuni, kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Then Jesus said to his disciples, Truly do I say to you, it will be hard for a rich man to enter the kingdom of heaven.
Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Amin, nawaambia, itakuwa vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mbinguni.
24 And again I say to you, It is easier for a camel to go through the eye of a needle, than for a rich man to enter the kingdom of heaven.
Tena nawaambia, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
25 And the disciples, hearing this, were exceedingly amazed, saying, Who then can be saved?
Wanafunzi wake waliposikia haya, walishangaa sana na kuuliza, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
26 But Jesus, fixing his eyes on them, said, With men this is impossible; but with God all things are possible.
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
27 Then Peter answering said to him, Lo! we left all, and followed thee; what then shall we have?
Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, sisi tumeacha kila kitu na kukufuata! Tutapata nini basi?”
28 And Jesus said to them, Truly do I say to you, that, in the renovation when the Son of man sitteth on the throne of his glory, ye who have followed me shall also yourselves sit on twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel.
Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, wakati wa kufanywa upya vitu vyote, Mwana wa Adamu atakapoketi kwenye kiti chake kitukufu cha enzi, ninyi mlionifuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi na viwili, mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
29 And every one who hath left brothers, or sisters, or father, or mother, or children, or lands, or houses, for the sake of my name, will receive many fold more, and will inherit everlasting life. (aiōnios g166)
Kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu zake wa kiume au wa kike, baba au mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi ya hayo, na ataurithi uzima wa milele. (aiōnios g166)
30 But many who are first will be last, and the last first.
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.

< Matthew 19 >