< Mark 3 >

1 And he entered again into a synagogue; and there was a man there having a withered hand;
Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
2 and they watched him, whether he would heal him on the sabbath, that they might accuse him.
Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
3 And he saith to the man having the withered hand, Stand up in the midst.
Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
4 And he saith to them, Is it lawful to do good on the sabbath, or to do evil? to save life, or to kill? But they were silent.
Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
5 And looking round on them with anger, being grieved for the hardness of their hearts, he saith to the man, Stretch forth thy hand. And he stretched it forth; and his hand was restored.
Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
6 And the Pharisees went forth, and immediately had a consultation with the Herodians against him, how they might destroy him.
Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
7 And Jesus withdrew with his disciples to the lake; and a great multitude from Galilee, and from Judaea followed;
Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
8 and from Jerusalem, and from Idumaea, and from beyond the Jordan, and the people about Tyre and Sidon, a great multitude, when they heard what great things he was doing, came to him.
na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
9 And he gave direction to his disciples, that a boat should be in readiness for him because of the multitude, that they might not throng him.
Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
10 For he had healed many, so that as many as had plagues pressed upon him to touch him.
Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
11 And the unclean spirits, when they saw him, fell down before him, and cried out, saying, Thou art the Son of God.
Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
12 And he strictly charged them that they should not make him known.
Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
13 And he goeth up into the mountain, and calleth to him whom he would; and they came to him.
Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
14 And he appointed twelve to be with him, and whom he might send forth to preach,
Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
15 and to have authority to cast out demons. And he appointed the twelve,
na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
16 and Simon he surnamed Peter;
Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
17 and James the son of Zebedee, and John the brother of James; and he surnamed them Boanerges, that is, Sons of thunder;
Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
18 and Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and James the son of Alphaeus, and Thaddaeus, and Simon of Cana,
na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
19 and Judas Iscariot, who betrayed him. And he cometh into the house.
na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
20 And again a multitude cometh together, so that they could not so much as eat bread.
Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
21 And his relations hearing of it went out to lay hold of him; for they said, He is beside himself.
Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
22 And the scribes who came down from Jerusalem said, He hath Beelzebul; and, He casteth out the demons through the prince of the demons.
Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
23 And calling them to him, he said to them in parables: How can Satan cast out Satan?
Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
24 And if a kingdom be divided against itself, that kingdom cannot stand;
Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
25 and if a house be divided against itself, that house will not be able to stand;
Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 and if Satan rise up against himself, he is divided, and cannot stand, but hath an end.
Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
27 Moreover, no one can enter into a strong man's house, and plunder his goods, unless he first bind the strong man; and then he will plunder his house.
Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
28 Truly do I say to you, All sins will be forgiven the sons of men, and the blasphemies wherewith they shall blaspheme;
Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
29 but he that shall blaspheme against the Holy Spirit hath no forgiveness forever, but is exposed to everlasting sin.— (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Because they said, He hath an unclean spirit.
Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
31 And his mother and his brothers came; and, standing without, sent to him, to call him.
Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
32 And a multitude was sitting about him; and they say to him, Lo! thy mother and thy brothers and thy sisters are without, seeking for thee.
Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
33 And he answering saith to them, Who is my mother, and my brothers?
Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
34 And looking round on those who sat about him, he saith, Behold my mother and my brothers.
Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
35 Whoever shall do the will of God, he is my brother, and sister, and mother.
Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.

< Mark 3 >