< Mark 15 >

1 And as soon as it was morning, the chief priests, having held a consultation with the elders and the scribes, and the whole council, bound Jesus, and carried him away, and delivered him up to Pilate.
Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
2 And Pilate asked him, Art thou the king of the Jews? And he answering saith to him, I am.
Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 And the chief priests brought many charges against him.
Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
4 And Pilate asked him again, Dost thou make no answer? See what things they are testifying against thee!
Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
5 But Jesus made no further answer; so that Pilate marveled.
Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
6 Now at the feast he was wont to release to them one prisoner, whom they might ask.
Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
7 And there was one named Barabbas, who lay bound with insurgents who had committed murder in the insurrection.
Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
8 And the multitude, coming up, began to ask him to do as he had been wont to do for them.
Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
9 And Pilate answered them, saying, Will ye that I release to you the king of the Jews?
Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he knew that for envy the chief priests had delivered him up.
Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
11 But the chief priests stirred up the multitude, that he should rather release to them Barabbas.
Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
12 And Pilate answering again said to them, What then would ye have me do with him whom ye call the king of the Jews?
Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 And they cried out again, Crucify him!
Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
14 Then Pilate said to them, Why, what evil hath he done? And they cried out the more, Crucify him!
Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
15 And Pilate, wishing to satisfy the multitude, released to them Barabbas; and, when he had scourged Jesus, delivered him up to be crucified.
Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
16 And the soldiers led him away into the court, which is the Praetorium; and they call together the whole band.
Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 And they clothe him with purple, and having platted a crown of thorns, they put it on him.
Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
18 And they began to salute him: Hail, king of the Jews!
Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
19 And they struck him on the head with a reed, and spit upon him, and kneeling down, did him homage.
Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
20 And after they had made sport of him, they stripped him of the purple robe, and put his own garments on him. And they lead him out to crucify him.
Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
21 And they compel one Simon a Cyrenaean, who was passing by, coming from the country, the father of Alexander and Rufus, to carry his cross.
Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
22 And they bring him to the place Golgotha; which is, when interpreted, Place of a Skull.
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
23 And they gave him wine mingled with myrrh; but he did not take it.
Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
24 And they crucify him, and divide his garments, casting lots for them, what each should take.
Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
25 And it was the third hour when they crucified him.
Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 And on the cross the inscription of the charge against him was written: “The king of the Jews.”
Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 And with him they crucify two robbers; one on his right hand, and one on his left.
Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
29 And they that passed by reviled him, wagging their heads, and saying, Ha! thou that destroyest the temple, and buildest it up in three days,
Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
30 save thyself, and come down from the cross.
basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
31 In like manner also the chief priests, with the scribes, making sport among themselves, said, He saved others, cannot he save himself?
Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
32 Let the Christ, the king of Israel, come down now from the cross, that we may see and believe. And they that were crucified with him were reviling him.
Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
33 And when the sixth hour had come, there was darkness over the whole land until the ninth hour.
Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
34 And at the ninth hour Jesus cried with a loud voice, Eloi, Eloi, lema sabachthani? which is, when interpreted, My God, my God, why hast thou forsaken me?
Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
35 And some of those who stood by, when they heard it, said, See! he is calling for Elijah.
Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
36 And one ran and filled a sponge with vinegar, and put it on a reed, and gave it to him to drink, saying, Hold! Let us see whether Elijah will come to take him down.
Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
37 And Jesus, having uttered a loud cry, expired.
Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
38 And the veil of the temple was rent in two from the top to the bottom.
Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
39 And the centurion who stood over against him, seeing that he so expired, said, Truly this man was the Son of God.
Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 There were also women looking on from a distance; among whom was Mary the Magdalene, and Mary the mother of James the less and of Joses, and Salome;
Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
41 who, when he was in Galilee, followed him, and rendered him their services; and many other women who came up with him to Jerusalem.
Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
42 And evening having now come, because it was the preparation, that is, the day before the sabbath,
Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
43 Joseph of Arimathaea, an honorable councilor, who was himself waiting for the kingdom of God, came, and boldly went in to Pilate, and asked for the body of Jesus.
Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
44 And Pilate wondered that he was already dead; and calling to him the centurion, he asked him whether he had been long dead.
Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
45 And having been informed by the centurion, he gave the body to Joseph.
Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
46 And having bought fine linen, he took him down, and wrapped him in the linen, and laid him in a tomb which was hewn out of a rock, and rolled a stone to the door of the tomb.
Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
47 And Mary the Magdalene and Mary the mother of Joses saw where he was laid.
Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.

< Mark 15 >