< Luke 1 >
1 Inasmuch as many have undertaken to arrange a narrative of those things which are fully believed among us,
Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2 even as they were delivered to us by those who were eye-witnesses from the beginning and became ministers of the word,
Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3 it seemed good to me also, having accurately traced up all things from the first, to write to thee a connected account, most excellent Theophilus,
Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4 that thou mightst know the exact truth with regard to those things in which thou wast instructed.
ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, king of Judaea, a certain priest named Zachariah, of the course of Abijah; and he had a wife of the daughters of Aaron, and her name was Elizabeth.
Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6 And they were both righteous in the sight of God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7 And they had no child, because Elizabeth was barren, and they were both far advanced in years.
Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 And it came to pass, that, while he was serving as priest before God in the order of his course,
Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9 according to the custom of the priesthood the lot fell to him to go into the temple of the Lord and burn the incense.
Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10 And the whole multitude of the people was praying without at the time of the incense.
Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11 And there appeared to him an angel of the Lord, standing on the right of the altar of incense.
Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12 And Zachariah was troubled at the sight, and fear fell upon him.
Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13 But the angel said to him, Fear not, Zachariah; for thy prayer was heard, and thy wife Elizabeth shall bear thee a son; and thou shalt call his name John.
Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14 And thou wilt have joy and gladness, and many will rejoice for his birth.
Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 For he will be great in the sight of the Lord; and will drink neither wine nor strong drink; and he will be filled with the Holy Spirit from his very birth.
Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 And many of the sons of Israel will he turn to the Lord their God.
Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17 And he will go before his face in the spirit and power of Elijah, to turn the hearts of fathers to children, and the disobedient to the wisdom of the righteous, to make ready for the Lord a prepared people.
Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
18 And Zachariah said to the angel, Whereby shall I know this? for I am an old man, and my wife is far advanced in years.
Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
19 And the angel answering said to him, I am Gabriel, who stand in the presence of God; and I was sent to speak to thee, and to tell thee these glad tidings.
Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20 And lo! thou shalt be silent, and not able to speak, until the day when these things shall come to pass, because thou didst not believe my words, which will be fulfilled in their season.
Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
21 And the people were looking for Zachariah, and wondering that he remained so long in the temple.
Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22 And on coming out, he was not able to speak to them; and they perceived that he had seen a vision in the temple; and he was beckoning to them, and remained speechless.
Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23 And it came to pass, when the days of his ministration were completed, that he returned to his house.
Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24 And after those days his wife Elizabeth conceived, and hid herself five months, saying,
Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25 Thus hath the Lord dealt with me in the days wherein he looked on me to take away my reproach among men.
“Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
26 And in her sixth month the angel Gabriel was sent from God to a city of Galilee, called Nazareth,
Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27 to a virgin betrothed to a man whose name was Joseph, of the house of David; and the virgin's name was Mary.
kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28 And the angel came in to her and said, Hail, thou that art highly favored! the Lord is with thee.
Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
29 And she was troubled at the words, and was considering what this salutation could mean.
Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30 And the angel said to her, Fear not, Mary; for thou hast found favor with God.
Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31 And lo! thou shalt conceive in thy womb, and hear a son, and shalt call his name Jesus.
Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32 He shall be great, and shall be called the Son of the Most High; and the Lord God will give to him the throne of David his father;
Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33 and he shall reign over the house of Jacob for ever; and of his kingdom there shall be no end. (aiōn )
Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
34 Then said Mary to the angel, How shall this be, since I know not a man?
Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
35 And the angel answering said to her, The Holy Spirit will come upon thee, and the power of the Most High will overshadow thee; wherefore the holy one that is to be born will be called the Son of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36 And lo! Elizabeth, thy kinswoman, she also hath conceived a son in her old age; and this is the sixth month with her who is called barren.
Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37 For nothing will be impossible with God.
Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
38 And Mary said, Lo, the handmaid of the Lord! May it be to me according to thy word. And the angel departed from her.
Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
39 And Mary arose and went in those days into the hill-country with haste, into a city of Judah.
Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40 And she entered the house of Zachariah, and saluted Elizabeth.
Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41 And it came to pass, when Elizabeth heard the salutation of Mary, that the babe leaped in her womb; and Elizabeth was filled with the Holy Spirit,
Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42 and cried out with a loud voice, and said, Blessed art thou among women; and blessed is the fruit of thy womb!
akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43 And whence is this to me, that the mother of my Lord should come to me?
Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 For lo! as soon as the voice of thy salutation came to my ears, the babe leaped in my womb in exultation.
Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 And blessed is she who hath believed that there will be an accomplishment of those things which were told her from the Lord.
Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
46 And Mary said, My soul magnifieth the Lord,
Naye Maria akasema,
47 and my spirit hath exulted in God my Saviour;
“Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48 for he hath looked upon the low estate of his handmaiden. For lo! from this time all generations will call me blessed;
Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49 for the Mighty One hath done great things for me; and holy is his name;
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50 and his mercy is from generation to generation on them that fear him.
Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51 He hath wrought mightily with his arm; he hath scattered the proud in the device of their heart.
Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52 He hath cast down princes from thrones, and exalted men of low degree.
amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53 The hungry he hath filled with good things, and the rich he hath sent away empty.
Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54 He hath given help to Israel his servant, in remembrance of his mercy
Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55 toward Abraham and his offspring for ever, as he spoke to our fathers. (aiōn )
Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn )
56 And Mary abode with her about three months, and returned to her own house.
Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57 Now Elizabeth's full time came that she should be delivered; and she brought forth a son.
Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58 And her neighbors and her kinsfolk heard that the Lord had showed great mercy toward her; and they rejoiced with her.
Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59 And it came to pass that on the eighth day they came to circumcise the child; and they were about to call him Zachariah, after the name of his father.
Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60 And his mother answering said, Not so; but he shall be called John.
Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
61 And they said to her, There is no one of thy kindred that is called by this name.
Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62 And they made signs to his father, how he would have him named.
Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63 And he asked for a writing-tablet, and wrote, saying, His name is John. And they all marveled.
Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64 And his mouth was opened immediately, and his tongue was loosed; and he spoke, blessing God.
Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And fear came on all that dwelt around them; and all these things were talked of throughout the whole of the hill-country of Judaea.
Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66 And all that heard them laid them up in their hearts, saying, What then will this child be? For the hand of the Lord was with him.
Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67 And Zachariah his father was filled with the Holy Spirit, and prophesied, saying,
Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68 Blessed be the Lord, the God of Israel! for he hath visited and redeemed his people,
“Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69 and hath raised up a horn of salvation for us in the house of David his servant, —
Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70 as he spoke by the mouth of his holy prophets of old, (aiōn )
Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn )
71 salvation from our enemies, and from the hand of all that hate us,
kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 to accomplish his mercy toward our fathers, and to remember his holy covenant,
Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73 the oath which he swore to Abraham our father,
Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74 to grant to us, that being delivered from the hand of our enemies, we might worship him without fear,
tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75 in holiness and righteousness before him, all our days.
kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76 And thou, child, shalt be called a prophet of the Most High; for thou shalt go in advance before the face of the Lord to prepare his ways,
Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77 to give knowledge of salvation to his people in the remission of their sins
kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78 through the tender mercy of our God, whereby the day-spring from on high hath visited us,
Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79 to give light to those sitting in darkness and the shadow of death, to guide our feet into the way of peace.
na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
80 And the child grew, and waxed strong in spirit; and was in the deserts till the day of his manifestation to Israel.
Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.