< Luke 4 >
1 And Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led in the Spirit in the wilderness
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 forty days, tempted by the Devil. And he ate nothing in those days; and when they were ended, he was hungry.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 And the Devil said to him, If thou art the Son of God, command this stone that it become a loaf of bread.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 And Jesus answered him, It is written, “Not on bread alone shall man live.”
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 And taking him up, he showed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 And the Devil said to him, All this power will I give thee, and their glory; because to me it hath been delivered, and I give it to whomever I will.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 If thou then wilt worship me, it shall all be thine.
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 And Jesus answering said to him, It is written, “Thou shalt worship the Lord thy God, and him only shalt thou serve.”
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 And he brought him to Jerusalem, and set him on the pinnacle of the temple, and said to him, If thou art the Son of God, cast thyself down from hence;
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 for it is written, “He will give his angels charge concerning thee, to guard thee;
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 and in their hands they will bear thee up, that thou mayst not dash thy foot against a stone.”
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 And Jesus answering said to him, It hath been said, “Thou shalt not make trial of the Lord thy God.”
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 And when he had brought every temptation to an end, the Devil departed from him for a season.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 And Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee; and there went out a report concerning him through all the surrounding country
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 And he taught in their synagogues, honored by all.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 And he came to Nazara, where he had been brought up, and, as his custom was, he went into the synagogue on the sabbath-day; and stood up to read.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 And there was delivered to him the book of the prophet Isaiah; and unrolling the book, he found the place where it was written,
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 “The Spirit of the Lord is upon me, because he anointed me to preach glad tidings to the poor; he hath sent me to proclaim deliverance to the captives, and recovering of sight to the blind, to set at liberty the oppressed,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 to proclaim the acceptable year of the Lord.”
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 And rolling up the book, he gave it back to the attendant, and sat down; and the eyes of all in the synagogue were fixed upon him.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 And he began to say to them, To-day hath this scripture been fulfilled in your ears.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 And they all spoke in his praise, and wondered at the words of grace which proceeded from his mouth; and they said, Is not this Joseph's son?
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 And he said to them, Ye will doubtless say to me this proverb, “Physician, heal thyself;” whatever things we have heard of as having been done in Capernaum, do here too in thy own country.
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 And he said, Truly do I say to you, No prophet is acceptable in his own country.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 But I tell you in truth, that there were many widows in Israel in the days of Elijah, when the heaven was shut up three years and six months, and there was a great famine throughout all the land;
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 and yet to none of them was Elijah sent, but to Sarepta in Sidonia, to a woman that was a widow.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 And there were many lepers in Israel in the time of Elisha the prophet; and not one of them was cleansed, but only Naaman the Syrian.
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 And all in the synagogue, when they heard this, were filled with wrath.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 And they rose up, and forced him out of the city and took him to the brow of the hill on which their city was built, to cast him down headlong;
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 but he, passing through the midst of them, went away.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 And he came down to Capernaum, a city of Galilee, and was teaching them on the sabbath.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 And they were astonished at his teaching; for his word was with authority.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 And in the synagogue there was a man having a spirit of an unclean demon, and he cried out with a loud voice,
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 Ha! what have we to do with thee, Jesus of Nazareth? Thou hast come to destroy us. I know who thou art, the Holy One of God.
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 And Jesus rebuked him, saying, Be silent, and come out of him. And the demon threw him down in the midst, and came out of him, having done him no hurt.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 And all were amazed; and they spoke with one another, saying, What kind of word is this, that with authority and power he commandeth the unclean spirits, and they come out?
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 And there went out a report concerning him into every place of the surrounding country.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 And he arose and went from the synagogue into the house of Simon. And Simon's wife's mother was seized with a great fever; and they besought him for her.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 And standing over her, he rebuked the fever, and it left her. And immediately she arose and waited on them.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 And when the sun was setting, all who had any sick with divers diseases brought them to him; and he laid his hands on every one of them, and healed them.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 And demons also came out from many, crying out, and saying, Thou art the Son of God. And he rebuked them, and did not suffer them to speak, because they knew that he was the Christ.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 And when it was day, he went out, and betook himself to a desert place; and the multitudes went in search of him; and they came to him, and would have prevented him from leaving them.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 But he said to them, I must publish the good tidings of the kingdom of God to the other cities also; because for this I was sent forth.
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 And he continued to preach in the synagogues of Galilee.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.