< Luke 4 >
1 And Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led in the Spirit in the wilderness
Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani,
2 forty days, tempted by the Devil. And he ate nothing in those days; and when they were ended, he was hungry.
mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.
3 And the Devil said to him, If thou art the Son of God, command this stone that it become a loaf of bread.
Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
4 And Jesus answered him, It is written, “Not on bread alone shall man live.”
Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’”
5 And taking him up, he showed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja.
6 And the Devil said to him, All this power will I give thee, and their glory; because to me it hath been delivered, and I give it to whomever I will.
Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka.
7 If thou then wilt worship me, it shall all be thine.
Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”
8 And Jesus answering said to him, It is written, “Thou shalt worship the Lord thy God, and him only shalt thou serve.”
Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’”
9 And he brought him to Jerusalem, and set him on the pinnacle of the temple, and said to him, If thou art the Son of God, cast thyself down from hence;
Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,
10 for it is written, “He will give his angels charge concerning thee, to guard thee;
kwa maana imeandikwa: “‘Atakuagizia malaika zake ili wakulinde;
11 and in their hands they will bear thee up, that thou mayst not dash thy foot against a stone.”
nao watakuchukua mikononi mwao, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’”
12 And Jesus answering said to him, It hath been said, “Thou shalt not make trial of the Lord thy God.”
Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”
13 And when he had brought every temptation to an end, the Devil departed from him for a season.
Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.
14 And Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee; and there went out a report concerning him through all the surrounding country
Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
15 And he taught in their synagogues, honored by all.
Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
16 And he came to Nazara, where he had been brought up, and, as his custom was, he went into the synagogue on the sabbath-day; and stood up to read.
Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
17 And there was delivered to him the book of the prophet Isaiah; and unrolling the book, he found the place where it was written,
naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
18 “The Spirit of the Lord is upon me, because he anointed me to preach glad tidings to the poor; he hath sent me to proclaim deliverance to the captives, and recovering of sight to the blind, to set at liberty the oppressed,
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
19 to proclaim the acceptable year of the Lord.”
na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
20 And rolling up the book, he gave it back to the attendant, and sat down; and the eyes of all in the synagogue were fixed upon him.
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
21 And he began to say to them, To-day hath this scripture been fulfilled in your ears.
Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”
22 And they all spoke in his praise, and wondered at the words of grace which proceeded from his mouth; and they said, Is not this Joseph's son?
Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
23 And he said to them, Ye will doubtless say to me this proverb, “Physician, heal thyself;” whatever things we have heard of as having been done in Capernaum, do here too in thy own country.
Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
24 And he said, Truly do I say to you, No prophet is acceptable in his own country.
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe.
25 But I tell you in truth, that there were many widows in Israel in the days of Elijah, when the heaven was shut up three years and six months, and there was a great famine throughout all the land;
Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
26 and yet to none of them was Elijah sent, but to Sarepta in Sidonia, to a woman that was a widow.
Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
27 And there were many lepers in Israel in the time of Elisha the prophet; and not one of them was cleansed, but only Naaman the Syrian.
Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
28 And all in the synagogue, when they heard this, were filled with wrath.
Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana.
29 And they rose up, and forced him out of the city and took him to the brow of the hill on which their city was built, to cast him down headlong;
Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali.
30 but he, passing through the midst of them, went away.
Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
31 And he came down to Capernaum, a city of Galilee, and was teaching them on the sabbath.
Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha.
32 And they were astonished at his teaching; for his word was with authority.
Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.
33 And in the synagogue there was a man having a spirit of an unclean demon, and he cried out with a loud voice,
Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema,
34 Ha! what have we to do with thee, Jesus of Nazareth? Thou hast come to destroy us. I know who thou art, the Holy One of God.
“Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
35 And Jesus rebuked him, saying, Be silent, and come out of him. And the demon threw him down in the midst, and came out of him, having done him no hurt.
Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru.
36 And all were amazed; and they spoke with one another, saying, What kind of word is this, that with authority and power he commandeth the unclean spirits, and they come out?
Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!”
37 And there went out a report concerning him into every place of the surrounding country.
Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.
38 And he arose and went from the synagogue into the house of Simon. And Simon's wife's mother was seized with a great fever; and they besought him for her.
Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie.
39 And standing over her, he rebuked the fever, and it left her. And immediately she arose and waited on them.
Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.
40 And when the sun was setting, all who had any sick with divers diseases brought them to him; and he laid his hands on every one of them, and healed them.
Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya.
41 And demons also came out from many, crying out, and saying, Thou art the Son of God. And he rebuked them, and did not suffer them to speak, because they knew that he was the Christ.
Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.
42 And when it was day, he went out, and betook himself to a desert place; and the multitudes went in search of him; and they came to him, and would have prevented him from leaving them.
Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke.
43 But he said to them, I must publish the good tidings of the kingdom of God to the other cities also; because for this I was sent forth.
Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.”
44 And he continued to preach in the synagogues of Galilee.
Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.