< Luke 3 >

1 Now in the fifteenth year of the reign of Tiberius Caesar, Pontius Pilate being governor of Judaea, and Herod tetrarch of Galilee, and his brother Philip tetrarch of Ituraea and of the region of Trachonitis, and Lysanias tetrarch of Abilene,
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 when Annas and Caiaphas were high-priests, the word of God came to John, the son of Zachariah, in the wilderness.
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 And he came into all the country about the Jordan, preaching the baptism of repentance for the remission of sins;
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 as it is written in the book of the words of Isaiah the prophet: “The voice of one crying in the wilderness, Prepare the way of the Lord, make straight his paths!
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 Every valley shall be filled, and every mountain and hill shall be made low; and the crooked places shall be made straight, and the rough ways smooth;
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 and all flesh shall see the salvation of God.”
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 He said therefore to the multitudes that came forth to be baptized by him, Brood of vipers, who warned you to flee from the coming wrath?
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 Bring forth therefore fruits worthy of repentance; and begin not to say within yourselves, We have Abraham for our father; for I say to you, that God is able out of these stones to raise up children to Abraham.
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 And already also is the axe lying at the root of the trees; every tree therefore that beareth not good fruit is to be cut down, and cast into the fire.
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 And the multitudes asked him, saying, What then must we do?
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 He answered and said to them, He that hath two coats, let him impart to him that hath none; and he that hath food, let him do likewise.
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 And there came also publicans to be baptized, and said to him, Teacher, what must we do?
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 And he said to them, Exact no more than hath been ordered you.
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 And soldiers also asked him, saying, And what must we do? And he said to them, Do violence to no one, accuse no one falsely, and be content with your wages.
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 And while the people were in expectation, and all were considering in their hearts concerning John, whether he were the Christ,
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 John answered and said to them all, I indeed baptize you with water; but he who is mightier than I is coming, the latchet of whose sandals I am not worthy to loose; he will baptize you in the Holy Spirit and in fire.
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 His winnowing-shovel is in his hand to thoroughly cleanse his threshing-floor, and gather the wheat into his garner; but the chaff he will burn up with unquenchable fire.
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 And giving many other exhortations he published the glad tidings to the people.
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 But Herod the tetrarch, being reproved by him on account of Herodias the wife of his brother, and on account of all the evil deeds which Herod had done,
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 added this also to them all, that he shut up John in prison.
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 And it came to pass, when all the people had been baptized, and Jesus also had been baptized, and was praying, that the heaven was opened,
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 and the Holy Spirit descended upon him in a bodily shape as a dove; and a voice came from heaven: “Thou art my beloved Son; with thee I am well pleased.”
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 And Jesus himself was, when he began, about thirty years of age, being, as was supposed, the son of Joseph, who was the son of Heli,
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 who was the son of Matthath, who was the son of Levi, who was the son of Melchi, who was the son of Jannai, who was the son of Joseph,
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 who was the son of Mattathias, who was the son of Amos, who was the son of Nahum, who was the son of Esli, who was the son of Naggai,
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 who was the son of Maath, who was the son of Mattathias, who was the son of Shimei, who was the son of Josech, who was the son of Joda,
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 who was the son of Joanan, who was the son of Rhesa, who was the son of Zerubbabel, who was the son of Shealtiel, who was the son of Neri,
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 who was the son of Melchi, who was the son of Addi, who was the son of Kosam, who was the son of Elmadam, who was the son of Er,
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 who was the son of Jesus, who was the son of Eliezer, who was the son of Jorim, who was the son of Matthath, who was the son of Levi,
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 who was the son of Simeon, who was the son of Judah, who was the son of Joseph, who was the son of Jonam, who was the son of Eliakim,
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 who was the son of Melea, who was the son of Menna, who was the son of Mattatha, who was the son of Nathan, who was the son of David,
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 who was the son of Jesse, who was the son of Obed, who was the son of Boaz, who was the son of Salma, who was the son of Nahshon,
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 who was the son of Amminadab, who was the son of Admin, who was the son of Arni, who was the son of Hezron, who was the son of Pharez, who was the son of Judah,
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 who was the son of Jacob, who was the son of Isaac, who was the son of Abraham, who was the son of Terah, who was the son of Nahor,
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 who was the son of Serug, who was the son of Reu, who was the son of Peleg, who was the son of Eber, who was the son of Shelah,
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 who was the son of Cainan, who was the son of Arphaxad, who was the son of Shem, who was the son of Noah, who was the son of Lamech,
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 who was the son of Methuselah, who was the son of Enoch, who was the son of Jared, who was the son of Mahalaleel, who was the son of Cainan,
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 who was the son of Enos, who was the son of Seth, who was the son of Adam, who was the son of God.
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< Luke 3 >