< Luke 22 >
1 Now the feast of unleavened bread, which is called the passover, was drawing near;
Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2 and the chief priests and the scribes were seeking how they might kill him; for they feared the people.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3 And Satan entered into Judas called Iscariot, who was of the number of the twelve.
Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4 And he went away, and consulted with the chief priests and captains, how he might deliver him up to them.
Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5 And they were glad, and covenanted to give him money.
Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6 And he agreed with them, and sought a good opportunity to deliver him up to them in the absence of the multitude.
Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7 Then came the day of unleavened bread, when the passover must be killed;
Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8 and he sent Peter and John, saying, Go and make ready for us the passover, that we may eat it.
Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
9 And they said to him, Where wilt thou that we make it ready?
Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
10 And he said to them, Lo! when ye have entered the city, there will meet you a man bearing a pitcher of water; follow him into the house where he goeth in;
Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11 and ye shall say to the master of the house, The Teacher saith to thee, Where is the guest-chamber, where I may eat the passover with my disciples?
Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12 And he will show you a large upper room furnished; there make ready.
Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
13 And they went and found as he had said to them; and they made ready the passover.
Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14 And when the hour had come, he placed himself at table, and the apostles with him.
Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15 And he said to them, Earnestly have I desired to eat this passover with you, before I suffer.
Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16 For I say to you, that I shall eat it no more, until it be fulfilled in the kingdom of God.
Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
17 And he took a cup, and gave thanks, and said, Take this, and divide it among yourselves.
Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18 For I say to you, that I shall not drink henceforth of the fruit of the vine, until the kingdom of God shall have come.
Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
19 And he took a loaf, and gave thanks, and broke it, and gave it to them, saying, This is my body, which is given for you; this do in remembrance of me.
Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
20 And in like manner he took the cup after supper, saying, This cup is the new covenant in my blood, which is about to be shed for you.
Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21 But lo! the hand of him that betrayeth me is with me on the table.
“Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22 For the Son of man indeed goeth away, as it hath been determined; but woe to that man by whom he is betrayed.
Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
23 And they began to inquire among themselves, which of them it was that was about to do this.
Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24 And there arose also a contention among them, which of them should be accounted the greatest.
Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25 And he said to them, The kings of the nations rule as lords over them, and they who exercise authority over them are called benefactors.
Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26 But it is not to be so with you; but let the greatest among you be as the youngest; and he that is chief, as he that serveth.
Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27 For which is greater? he who reclineth at the table, or he who serveth? Is not he that reclineth at the table? But I am in the midst of you as he who serveth.
Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28 Ye however are they who have continued steadfastly with me in my trials.
“Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29 And I appoint to you a kingdom, as my Father appointed to me;
na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30 that ye may eat and drink at my table in my kingdom; and ye shall sit on thrones, judging the twelve tribes of Israel.
Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31 Simon, Simon, lo! Satan hath asked for you, that he may sift you as wheat.
“Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32 But I have prayed for thee, that thy faith fail not. And do thou, when thou hast returned to me, strengthen thy brethren.
Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
33 And he said to him, Lord, I am ready to go with thee both to prison and to death.
Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
34 And he said, I tell thee, Peter, a cock will not crow this day, till thou hast thrice denied that thou knowest me.
Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
35 And he said to them, When I sent you without purse, or bag, or sandals, were ye in need of anything? And they said, Of nothing. Then he said to them,
Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
36 But now, he that hath a purse, let him take it, and likewise a bag; and he that hath not, let him sell his garment, and buy a sword.
Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37 For I say to you, that this which is written must be accomplished in me: “And he was reckoned among transgressors.” For that which concerneth me also hath an end.
Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
38 And they said, Lord, behold, here are two swords. And he said to him, It is enough!
Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
39 And going out, he went, as he was wont, to the Mount of Olives; and the disciples followed him.
Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40 And when he was at the place, he said to them, Pray that ye may not enter into temptation.
Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
41 And he withdrew from them about a stone's throw; and kneeling down he prayed,
Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42 saying, Father, if thou art willing to remove this cup from me—yet not my will, but thine be done!
“Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
43 And there appeared to him an angel from heaven, strengthening him.
Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44 And being in an agony, he prayed more earnestly. And his sweat was as it were great drops of blood falling to the ground.
Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45 And rising up from prayer, he came to the disciples, and found them sleeping for sorrow,
Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46 and said to them, Why sleep ye? Rise, and pray that ye may not enter into temptation.
Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
47 While he was yet speaking, lo! a multitude, and he that was called Judas, one of the twelve, was at the head of them; and he drew near to Jesus to kiss him.
Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48 But Jesus said to him, Judas, dost thou betray the Son of man with a kiss?
Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
49 And they who were about him, seeing what would follow, said, Lord, shall we smite with the sword?
Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
50 And one of them smote the servant of the high-priest, and cut off his right ear.
Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51 But Jesus answering said, Permit thus far; and touched his ear, and healed him.
Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52 Then Jesus said to the chief priests and captains of the temple and elders who had come to him, Ye have come out as against a robber, with swords and clubs;
Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53 when I was daily with you in the temple, ye did not put forth your hands against me; but this is your hour, and the power of darkness.
Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
54 And they seized him, and led him away, and brought him into the house of the high-priest. And Peter followed afar off.
Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55 And when they had kindled a fire in the midst of the court, and had sat down together, Peter sat down among them.
Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56 But a certain maid-servant saw him sitting at the fire, and steadily looking at him said, This man also was with him.
Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
57 And he denied him, saying, Woman, I do not know him.
Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
58 And after a little while another saw him, and said, Thou also art one of them. And Peter said, Man, I am not.
Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
59 And in about one hour's time, another confidently affirmed, saying, In truth this man also was with him; for he is a Galilaean.
Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
60 And Peter said, Man, I know not what thou sayest. And immediately, while he was yet speaking, a cock crew.
Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61 And the Lord turned and looked upon Peter; and Peter remembered the word of the Lord, that he had said to him, Before a cock crows this day, thou wilt thrice deny me.
Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
62 And he went out, and wept bitterly.
Hapo akatoka nje, akalia sana.
63 And the men that held Jesus mocked him, and beat him;
Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64 and having blindfolded him, they asked him, saying, Prophesy, who is it that struck thee?
Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
65 And many other things did they scoffingly say against him.
Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66 And when it was day, the elders of the people, both chief priests and scribes, came together, and brought him before their council, saying,
Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67 If thou art the Christ, tell us. And he said to them, If I tell you, ye will not believe;
Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68 and if I ask, ye will not answer.
na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69 But from this time the Son of man will sit on the right hand of the power of God.
Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
70 Then they all said, Art thou then the Son of God? And he said to them, Ye say what is true; for I am.
Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
71 And they said, What further need have we of testimony? For we have ourselves heard from his own mouth.
Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”