< John 7 >

1 After these things Jesus walked in Galilee; for he would not walk in Judaea, because the Jews sought to kill him.
Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Hakutaka kwenda Uyahudi kwa sababu Wayahudi huko walitaka kumuua.
2 Now the feast of the Jews, the feast of tabernacles, was at hand.
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3 His brothers therefore said to him, Depart hence, and go into Judaea, that thy disciples also may see thy works which thou art doing.
Hivyo ndugu zake Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende Uyahudi ili wanafunzi Wako wapate kuona miujiza unayofanya.
4 For no one doeth anything in secret, and yet himself seeketh to be known openly. If thou doest these things, manifest thyself to the world.
Mtu anayetaka kujulikana hafanyi mambo yake kwa siri. Kama unafanya mambo haya, jionyeshe kwa ulimwengu.”
5 For even his brothers did not believe in him.
Hata ndugu zake mwenyewe hawakumwamini.
6 Jesus saith to them, My time is not yet come; but your time is always ready.
Yesu akawaambia, “Wakati wangu bado haujawadia, lakini wakati wenu upo siku zote.
7 The world cannot hate you; but me it hateth, because I testify of it, that its works are evil.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini unanichukia mimi kwa sababu ninawashuhudia kwamba matendo yao ni maovu.
8 Go ye up to the feast; I go not up to this feast; for my time is not yet fully come.
Ninyi nendeni kwenye Sikukuu, lakini mimi sitahudhuria Sikukuu hii kwa sababu wakati wangu haujawadia.”
9 Having said these things, he remained in Galilee.
Akiisha kusema hayo, akabaki Galilaya.
10 But when his brothers had gone up to the feast, then he also went up, not openly, but as it were in secret.
Lakini ndugu zake walipokwisha kuondoka kwenda kwenye Sikukuu, yeye pia alikwenda lakini kwa siri.
11 The Jews therefore sought him at the feast, and said, Where is that man?
Wayahudi walikuwa wakimtafuta huko kwenye Sikukuu na kuulizana, “Yuko wapi huyu mtu?”
12 And there was much debating among the multitude concerning him. Some said, He is a good man; others said, Nay, but he deceiveth the multitude.
Kulikuwa na minongʼono iliyoenea kumhusu Yesu katika umati wa watu, wakati wengine wakisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walikuwa wakisema, “La, yeye anawadanganya watu.”
13 No one, however, spoke openly of him, for fear of the Jews.
Lakini hakuna mtu yeyote aliyemsema waziwazi kumhusu kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi.
14 But when it was now the midst of the feast, Jesus went up into the temple and taught.
Ilipokaribia katikati ya Sikukuu, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
15 The Jews therefore marveled, saying, How knoweth this man letters, having never learned?
Wayahudi wakastaajabia mafundisho yake wakasema, “Mtu huyu amepataje kujua mambo haya bila kufundishwa?”
16 Jesus therefore answered them, and said, My teaching is not mine, but his that sent me.
Ndipo Yesu akawajibu, “Mafundisho yangu si yangu mwenyewe, bali yanatoka kwake yeye aliyenituma.
17 If any one is desirous to do his will, he will know concerning the teaching, whether it is from God, or whether I speak from myself.
Mtu yeyote akipenda kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu au ninasema kwa ajili yangu mwenyewe.
18 He that speaketh from himself seeketh his own glory; but he that seeketh the glory of him that sent him, he is true, and in him is no unrighteousness.
Wale wanenao kwa ajili yao wenyewe hufanya hivyo kwa kutaka utukufu wao wenyewe. Lakini yeye atafutaye utukufu wa yule aliyemtuma ni wa kweli, wala hakuna uongo ndani yake.
19 Hath not Moses given you the Law? and none of you keepeth the Law! Why do ye seek to kill me?
Je, Mose hakuwapa ninyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja wenu anayeishika hiyo sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
20 The multitude answered, Thou hast a demon! Who seeketh to kill thee?
Ule umati wa watu ukamjibu, “Wewe una pepo mchafu! Ni nani anayetaka kukuua?”
21 Jesus answered and said to them, I have done one good work, and ye are all wondering.
Yesu akawajibu, “Nimefanya muujiza mmoja na nyote mkastaajabu.
22 Moses hath given you circumcision, (not that it is from Moses, but from the fathers; ) and ye on the sabbath circumcise a man.
Lakini kwa kuwa Mose aliwaamuru tohara (ingawa kwa kweli haikutoka kwa Mose bali kwa baba zenu wakuu), mnamtahiri mtoto hata siku ya Sabato.
23 If a man receive circumcision on the sabbath, that the law of Moses may not be broken, are ye angry at me, because I have restored soundness to the whole body of a man on the sabbath?
Ikiwa mtoto aweza kutahiriwa siku ya Sabato kusudi sheria ya Mose isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia kwa kumponya mtu mwili wake wote siku ya Sabato?
24 Judge not according to the appearance, but judge righteous judgment.
Acheni kuhukumu mambo kwa jinsi mnavyoona tu, bali hukumuni kwa haki.”
25 Then some of the men of Jerusalem said, Is not this he whom they seek to kill?
Ndipo baadhi ya watu wa Yerusalemu wakawa wanasema, “Tazameni, huyu si yule mtu wanayetaka kumuua?
26 and see! he speaketh boldly, and they say nothing to him. Have the rulers discovered certainly that this man is the Christ?
Mbona yuko hapa anazungumza hadharani na wala hawamwambii neno lolote? Je, inawezekana viongozi wanafahamu kuwa huyu ndiye Kristo?
27 Still, as to this man, we know whence he is; but when the Christ cometh, no one knoweth whence he is.
Tunafahamu huyu mtu anakotoka, lakini Kristo atakapokuja, hakuna yeyote atakayejua atokako.”
28 Jesus therefore cried aloud, teaching in the temple and saying, Ye both know me, and ye know whence I am; and I have not come of myself, but there is in truth one who sent me, whom ye know not.
Ndipo Yesu, akaendelea kufundisha Hekaluni, akisema, “Ninyi mnanifahamu na kujua nitokako. Mimi sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, bali yeye aliyenituma ni wa kweli na ninyi hammjui.
29 I know him, because I am from him, and he hath sent me.
Mimi namjua kwa kuwa nimetoka kwake, naye ndiye alinituma.”
30 Therefore they sought to take him; but no one laid hands on him, because his hour had not yet come.
Ndipo wakatafuta kumkamata, lakini hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumshika kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijawadia.
31 But of the multitude many believed in him, and said, When the Christ cometh, will he do more signs than these which this man doeth?
Nao watu wengi wakamwamini, wakasema, “Je, Kristo atakapokuja, atafanya miujiza mikuu zaidi kuliko aliyoifanya mtu huyu?”
32 The Pharisees heard the multitude thus debating concerning him; and the chief priest and the Pharisees sent officers to seize him.
Mafarisayo wakasikia watu wakinongʼona mambo kama hayo kuhusu Yesu, ndipo wao pamoja na viongozi wa makuhani wakatuma walinzi wa Hekalu waende kumkamata.
33 Jesus therefore said, Yet a little while I am with you, and then I go to him that sent me.
Yesu akasema, “Mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo, kisha nitarudi kwake yeye aliyenituma.
34 Ye will seek me and not find me; and where I am, ye cannot come.
Mtanitafuta lakini hamtaniona, nami niliko ninyi hamwezi kuja.”
35 The Jews therefore said among themselves, Whither will this man go, that we shall not find him? Will he go to the dispersed among the Greeks, and teach the Greeks?
Wayahudi wakaulizana wao kwa wao, “Huyu mtu anataka kwenda wapi ambako hatuwezi kumfuata? Je, anataka kwenda kwa Wayunani ambako baadhi ya watu wetu wametawanyikia, akawafundishe Wayunani?
36 What meaneth this which he said, Ye will seek me, and not find me; and where I am, ye cannot come?
Yeye ana maana gani anaposema, ‘Mtanitafuta lakini hamtaniona,’ na, ‘nami niliko ninyi hamwezi kuja’?”
37 On the last day, which is the great day, of the feast, Jesus stood and cried aloud, saying, If any one thirst, let him come to me, and drink.
Siku ile ya mwisho ya Sikukuu, siku ile kuu, wakati Yesu akiwa amesimama huko, akapaza sauti yake akasema, “Kama mtu yeyote anaona kiu na aje kwangu anywe.
38 He that believeth in me, from within him, as the Scripture hath said, will flow rivers of living water.
Yeyote aniaminiye mimi, kama Maandiko yasemavyo, vijito vya maji ya uzima vitatiririka ndani mwake.”
39 But this he said of the Spirit, which those that believed in him were to receive; for the Spirit was not yet, because Jesus was not yet glorified.
Yesu aliposema haya alimaanisha Roho Mtakatifu ambaye wote waliomwamini wangempokea, kwani mpaka wakati huo, Roho alikuwa hajatolewa, kwa kuwa Yesu alikuwa bado hajatukuzwa.
40 Some of the multitude therefore, when they heard these words, said, This is in truth the prophet. Others said, This is the Christ.
Waliposikia maneno hayo, baadhi ya watu miongoni mwa ule umati wakasema, “Hakika huyu ndiye yule Nabii.”
41 Others said, Doth the Christ then come from Galilee?
Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine wakauliza, “Je, Kristo kwao ni Galilaya?
42 Hath not the Scripture said, that the Christ cometh from the seed of David, and from Bethlehem, the town where David was?
Je, Maandiko hayasemi kwamba Kristo atakuja kutoka jamaa ya Daudi na kutoka Bethlehemu, mji alioishi Daudi?”
43 So there was a division among the multitude because of him.
Kwa hiyo watu wakagawanyika kwa ajili ya Yesu.
44 And some of them wished to seize him; but no one laid hands on him.
Baadhi yao walitaka kumkamata, lakini hakuna aliyethubutu kumgusa.
45 The officers therefore came to the chief priests and Pharisees, who said to them, Why did ye not bring him?
Hatimaye wale walinzi wa Hekalu wakarudi kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo waliokuwa wamewatuma ili kumkamata Yesu, wakaulizwa, “Mbona hamkumkamata?”
46 The officers answered, Never man spoke like this man.
Wale walinzi wakajibu, “Kamwe hajanena mtu yeyote kama yeye anenavyo.”
47 The Pharisees answered them, Have ye also been deceived?
Mafarisayo wakajibu, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
48 Hath any one of the rulers believed in him? or of the Pharisees?
Je, kuna kiongozi yeyote au mmoja wa Mafarisayo ambaye amemwamini?
49 but this multitude that know not the Law are accursed.
Lakini huu umati wa watu wasiojua Sheria ya Mose, wamelaaniwa.”
50 Nicodemus saith to them, being one of them,
Ndipo Nikodemo, yule aliyekuwa amemwendea Yesu siku moja usiku, ambaye alikuwa mmoja wao akauliza,
51 Doth our law judge a man, unless it first hear from him, and know what he doeth?
“Je, sheria zetu zinaturuhusu kumhukumu mtu kabla ya kumsikiliza na kufahamu alilotenda?”
52 They answered and said to him, Art thou too from Galilee? Search and see that no prophet ariseth from Galilee.
Wakamjibu, “Je, wewe pia unatoka Galilaya? Chunguza nawe utaona kwamba hakuna nabii atokae Galilaya!” [
53 (Joh 7:53 - 8:12: This passage is omitted as ungenuine by Tischendorf and most critical editors of the Greek Testament. It is found in some manuscripts, but not in the most ancient. It is, however, very generally regarded as a genuine relic of the teaching of Christ, though not forming a part of the fourth Gospel. I give it in the text of Tregelles, omitting the words which he incloses in brackets. Tregelles, however, does not suppose it to be genuine.) [[And they went each to his house;
Kisha wakaondoka, kila mtu akarudi nyumbani kwake.

< John 7 >