< John 4 >
1 When therefore Jesus knew that the Pharisees had heard that Jesus made and baptized more disciples than John,
Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2 (though Jesus himself did not baptize, but his disciples, )
(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3 he left Judaea, and went again to Galilee.
Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4 And he must necessarily pass through Samaria.
na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5 He cometh therefore to a city of Samaria, called Sychar, near the piece of land which Jacob gave to his son Joseph.
Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6 And Jacob's well was there. Jesus therefore, being wearied with the journey, was sitting thus by the well. It was about the sixth hour.
Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 There cometh a woman of Samaria to draw water. Jesus saith to her, Give me to drink.
Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.”
8 For his disciples had gone away into the city to buy food.
(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 The Samaritan woman saith to him, How is it that thou, who art a Jew, askest drink of me, who am a Samaritan woman? For Jews have no dealings with Samaritans.
Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10 Jesus answered and said to her, If thou hadst known the gift of God, and who it is that saith to thee, Give me to drink, thou wouldst have asked of him, and he would have given thee living water.
Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”
11 The woman saith to him, Sir, thou hast nothing to draw with, and the well is deep. Whence hast thou the living water?
Huyo mama akasema, “Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12 Art thou greater than our father Jacob, who gave us the well, and drank thereof himself, and his sons, and his cattle?
Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
13 Jesus answered and said to her, Every one that drinketh of this water, will thirst again;
Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14 but whoever drinketh of the water that I will give him, will never thirst; but the water that I will give him will become within him a well of water springing up to everlasting life. (aiōn , aiōnios )
Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn , aiōnios )
15 The woman saith to him, Sir, give me this water, that I may not thirst, nor come hither to draw.
Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
16 He saith to her, Go, call thy husband, and come hither.
Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
17 The woman answered, I have no husband. Jesus saith to her, Thou saidst well, that thou hast no husband.
Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
18 For thou hast had five husbands; and he whom thou now hast is not thy husband; in this thou hast spoken truly.
Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
19 The woman saith to him, Sir, I perceive that thou art a prophet.
Huyo Mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20 Our fathers worshipped on this mountain; and ye say, that in Jerusalem is the place where men ought to worship.
Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu.”
21 Jesus saith to her, Believe me, woman, the hour is coming, when ye shall neither on this mountain, nor in Jerusalem, worship the Father.
Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 Ye worship that which ye know not; we worship that which we know; for salvation is from the Jews.
Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 But the hour is coming, and now is, when the true worshippers will worship the Father in spirit and in truth; for such worshippers the Father seeketh.
Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24 God is a spirit; and they who worship must worship in spirit and in truth.
Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake.”
25 The woman saith to him, I know that Messiah cometh (who is called Christ); when he hath come, he will tell us all things.
Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
26 Jesus saith to her, I who speak to thee am he.
Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
27 And upon this his disciples came, and marveled that he was talking with a woman. Yet no one said, What dost thou seek? or, Why dost thou talk with her?
Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
28 The woman then left her water-pot, and went away into the city, and saith to the men,
Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29 Come, see a man who told me all things which I have done. Is this the Christ?
“Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
30 They went out of the city, and came to him.
Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31 In the mean while the disciples asked him, saying, Rabbi, eat.
Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
32 But he said to them, I have food to eat that ye know not of.
Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 The disciples therefore said to one another, Hath any one brought him anything to eat?
Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
34 Jesus saith to them, My food is to do the will of him that sent me, and to finish his work.
Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35 Do ye not say, There are yet four months, and the harvest cometh? Lo! I say to you, lift up your eyes, and look on the fields, that they are white for harvest.
Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36 Already is the reaper receiving wages, and gathering fruit unto everlasting life; that both the sower and the reaper may rejoice together. (aiōnios )
Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios )
37 And herein is fulfilled the true saying, One soweth, and another reapeth.
Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38 I have sent you to reap that whereon ye have not labored. Others have labored, and ye have entered into their labor.
Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
39 And many of the Samaritans of that city believed in him because of the words of the woman, who testified, He told me all things which I have done.
Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.”
40 When therefore the Samaritans came to him, they besought him to remain with them; and he remained there two days.
Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41 And many more believed on account of his word;
Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42 and said to the woman, No longer do we believe on account of what thou hast told us; for we have ourselves heard him, and know that this is in truth the Saviour of the world.
Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
43 And after the two days he went from that place into Galilee.
Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44 For Jesus himself testified, that a prophet hath no honor in his own country.
Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.”
45 When therefore he came into Galilee, the Galilaeans received him, having seen all that he did in Jerusalem at the feast; for they also went to the feast.
Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46 So he came again into Cana of Galilee, where he made the water wine. And there was a certain nobleman, whose son was sick, at Capernaum.
Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47 He, having heard that Jesus had come out of Judaea into Galilee, went to him, and asked him to go down and heal his son; for he was at the point of death.
Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48 Then Jesus said to him, Unless ye see signs and wonders, ye will not believe.
Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”
49 The nobleman saith to him, Sir, come down before my child die.
Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.”
50 Jesus saith to him, Go; thy son liveth. The man believed the word that Jesus spoke to him, and went away.
Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao yu mzima.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51 And as he was now going down, the servants met him, and brought word that his child was living.
Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52 Then he inquired of them the hour when he began to mend. And they said to him, Yesterday at the seventh hour the fever left him.
Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.”
53 So the father knew that it was in the same hour in which Jesus said to him, Thy son is living. And he himself believed, and his whole house.
Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao yu mzima.” Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54 This again, a second sign, Jesus wrought, when he had come out of Judaea into Galilee.
Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.