< John 3 >

1 And there was a man of the Pharisees, named Nicodemus, a ruler of the Jews.
Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
2 This man came to him by night, and said to him, Rabbi, we know that thou hast come as a teacher from God; for no one can do these signs which thou doest, unless God be with him.
Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
3 Jesus answered and said to him, Truly, truly do I say to thee, Unless a man be born again, he cannot see the kingdom of God.
Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
4 Nicodemus saith to him, How can a man be born when he is old? Can he enter his mother's womb a second time, and be born?
Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
5 Jesus answered, Truly, truly do I say to thee, Unless a man be born of water and of the Spirit, he cannot enter the kingdom of heaven.
Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
6 That which is born of the flesh, is flesh; and that which is born of the Spirit, is spirit.
Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
7 Marvel not that I said to thee, Ye must be born again.
Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’
8 The wind bloweth where it will; and thou hearest the sound thereof, but knowest not whence it cometh, and whither it goeth: so is every one that is born of the Spirit.
Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
9 Nicodemus answered and said to him, How can these things be?
Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
10 Jesus answered and said to him, Art thou the teacher of Israel, and understandest not these things?
Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
11 Truly, truly do I say to thee, We speak that which we know, and testify that which we have seen; and ye receive not our testimony.
Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
12 If I have told you earthly things, and ye believe not, how will ye believe if I tell you heavenly things?
Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
13 And no one hath ascended into heaven, but he who came down from heaven, even the Son of man.
Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.
14 And as Moses lifted up the serpent in the wilderness, so must the Son of man be lifted up
Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.
15 that every one who believeth in him may have everlasting life. (aiōnios g166)
Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
16 For God so loved the world, that he gave the only begotten Son, that every one who believeth in him may not perish, but may have everlasting life. (aiōnios g166)
“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
17 For God sent not the Son into the world to condemn the world, but that through him the world might be saved.
Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
18 He that believeth in him is not condemned; he that believeth not hath already been condemned, because he hath not believed in the name of the only begotten Son of God.
Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
19 And this is the condemnation, that the light hath come into the world, and men loved the darkness rather than the light; for their deeds were evil.
Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.
20 For every one that doeth evil hateth the light, and cometh not to the light, lest his deeds should be reproved.
Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
21 But he that doeth the truth cometh to the light, that his deeds may be made manifest, that they are wrought in God.
Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
22 After these things Jesus and his disciples came into the land of Judaea; and there he remained with them, and baptized.
Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.
23 And John also was baptizing in AEnon, near Salim, because there was much water there; and they came, and were baptized.
Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.
24 For John was not yet thrown into prison.
(Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).
25 Then there arose a question on the part of John's disciples with a Jew about purifying.
Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
26 And they came to John, and said to him, Rabbi, he who was with thee beyond the Jordan, to whom thou hast borne witness, behold, he baptizeth, and all men are going to him.
Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
27 John answered and said, A man can receive nothing, unless it be given him from heaven.
Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
28 Ye yourselves bear me witness, that I said, I am not the Christ, but that I was sent before that man.
Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, ila nimetumwa nimtangulie.’
29 He that hath the bride is the bridegroom; but the friend of the bridegroom, who standeth and heareth him, rejoiceth greatly because of the bridegroom's voice. This my joy then hath become full.
Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
30 He must increase, but I must decrease.
Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”
31 He that cometh from above is above all. He that is from the earth is earthly, and speaketh earthly things; he that cometh from heaven
“Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
32 testifieth what he hath seen and heard; and no one receiveth his testimony.
Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
33 He that hath received his testimony hath set his seal that God is true.
Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
34 For he whom God sent speaketh the words of God; for he giveth not the Spirit by measure.
Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo.
35 The Father loveth the Son, and hath given all things into his hand.
Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake.
36 He that believeth in the Son hath everlasting life; and he that disobeyeth the Son shall not see life, but the wrath of God abideth on him. (aiōnios g166)
Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios g166)

< John 3 >