< John 17 >

1 When Jesus had thus spoken, he lifted up his eyes to heaven, and said, Father! the hour is come; glorify thy Son, that the Son may glorify thee;
Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
2 according as thou gavest him authority over all flesh, that he should give everlasting life to all whom thou hast given him. (aiōnios g166)
Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios g166)
3 And this is the everlasting life, to know thee, the only true God, and Jesus Christ whom thou didst send. (aiōnios g166)
Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
4 I have glorified thee on the earth, having finished the work which thou gavest me to do;
Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
5 and now, Father! do thou glorify me with thyself, with the glory which I had with thee before the world was.
Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
6 I manifested thy name to the men whom thou gavest me out of the world. Thine they were, and thou gavest them to me; and they have kept thy word.
“Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
7 Now they know that all things whatever thou hast given me are from thee;
Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
8 for I have given to them the words which thou hast given me; and they received them, and knew surely that I came forth from thee, and believed that thou didst send me.
kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
9 I pray for them; I pray not for the world, but for those whom thou hast given me; for they are thine;
Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
10 and all things that are mine are thine, and thine are mine; and I am glorified in them.
Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
11 And I am no longer in the world; and they are in the world, and I come to thee. Holy Father! keep them in thy name which thou hast given me, that they may be one, even as we are.
Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
12 While I was with them, I kept them in thy name which thou hast given me, and guarded them; and no one of them is lost except the son of perdition, that the Scripture may be fulfilled.
Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
13 But now I come to thee; and these things I speak in the world, that they may have my joy made full in them.
“Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
14 I have given them thy word; and the world hath hated them, because they are not of the world, even as I am not of the world.
Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
15 I do not pray thee to take them out of the world, but to keep them from evil.
Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
16 They are not of the world, even as I am not of the world.
Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
17 Sanctify them in thy truth; thy word is truth.
Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
18 As thou didst send me into the world, I also sent them into the world.
Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
19 And in their behalf I sanctify myself, that they also may be sanctified in the truth.
Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
20 Yet not for these alone do I pray, but also for those who believe in me through their word;
“Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
21 that they all may be one; as thou, Father, art in me and I in thee, that they also may be in us, that the world may believe that thou didst send me.
ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
22 And the glory which thou hast given me, I have given them, that they may be one, even as we are one;
Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
23 I in them, and thou in me, that they may be made perfect in one, that the world may know that thou hast sent me, and hast loved them, as thou hast loved me.
Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
24 Father! as to that which thou hast given me, I desire that they also be with me where I am, that they may behold my glory which thou hast given me; for thou lovedst me before the foundation of the world.
“Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
25 Righteous Father! and yet the world knew thee not! but I knew thee, and these knew that thou didst send me.
“Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
26 And I made known to them thy name, and will make it known; that the love wherewith thou hast loved me may be in them, and I in them.
Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”

< John 17 >