< Job 8 >
1 Then answered Bildad the Shuhite, and said:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 How long wilt thou speak such things? How long shall the words of thy mouth be like a strong wind?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 Will God pervert judgment? Or will the Almighty pervert justice?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 As thy children sinned against him, He hath given them up to their transgression.
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 But if thou wilt seek early to God, And make thy supplication to the Almighty, —
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 If thou wilt be pure and upright, Surely he will yet arise for thee, And prosper thy righteous habitation;
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 So that thy beginning shall be small, And thy latter end very great.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 For inquire, I pray thee, of the former age, And mark what hath been searched out by their fathers;
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 (For we are of yesterday and know nothing, Since our days upon the earth are but a shadow; )
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 Will not they instruct thee, and tell thee, And utter words from their understanding?
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 “Can the paper-reed grow up without mire? Can the bulrush grow without water?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 While it is yet in its greenness, and is not cut down, It withereth before any other herb.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 Such is the fate of all who forget God; So perisheth the hope of the ungodly.
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 His confidence shall come to nought, And his trust shall prove a spider's web.
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 He shall lean upon his house, and it shall not stand; He shall lay fast hold on it, but it shall not endure.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 He is in full green before the sun, And his branches shoot forth over his garden;
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 His roots are entwined about the heap, And he seeth the place of stones;
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 When he shall be destroyed from his place, It shall deny him, saying, 'I never saw thee.'
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Lo! such is the joy of his course! And others shall spring up from his place”
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 Behold, God will not cast away an upright man; Nor will he help the evil-doers.
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 While he filleth thy mouth with laughter, And thy lips with gladness,
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 They that hate thee shall be clothed with shame, And the dwelling-place of the wicked shall come to nought.
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.