< Job 6 >

1 Then Job answered and said:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 O that my grief were weighed thoroughly! That my calamities were put together in the balance!
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
3 Surely they would be heavier than the sand of the sea; On this account were my words rash.
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arrows of the Almighty have pierced me; Their poison drinketh up my spirit; The terrors of God set themselves in array against me.
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
5 Doth the wild ass bray in the midst of grass? Or loweth the ox over his fodder?
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
6 Can that which is unsavory be eaten without salt? Is there any taste in the white of an egg?
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
7 That which my soul abhorreth to touch Hath become my loathsome food.
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
8 O that I might have my request, And that God would grant me that which I long for!
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
9 That it would please God to destroy me; That he would let loose his hand, and make an end of me!
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
10 Yet it should still be my consolation, Yea, in unsparing anguish I would exult, That I have not denied the commands of the Holy One.
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11 What is my strength, that I should hope? And what mine end, that I should be patient?
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
12 Is my strength the strength of stones? Or is my flesh brass?
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
13 Alas, there is no help within me! Deliverance is driven from me!
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
14 To the afflicted, kindness should be shown by a friend; Else he casteth off the fear of the Almighty.
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
15 But my brethren are faithless like a brook; Like streams of the valley that pass away;
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
16 Which are turbid by reason of the ice, And the snow, which hideth itself in them.
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
17 As soon as they flow forth, they vanish; When the heat cometh, they are dried up from their place.
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
18 The caravans turn aside to them on their way; They go up into the desert, and perish.
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
19 The caravans of Tema look for them; The companies of Sheba expect to see them;
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
20 They are ashamed that they have relied on them; They come to their place, and are confounded.
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
21 So ye also are nothing; Ye see a terror, and shrink back.
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
22 Have I said, Bring me gifts? Or, Give a present for me out of your substance?
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
23 Or, Deliver me from the enemy's hand? Or, Rescue me from the hand of the violent?
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
24 Convince me, and I will hold my peace; Cause me to understand wherein I have erred.
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
25 How powerful are the words of truth! But what do your reproaches prove?
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
26 Do ye mean to censure words? The words of a man in despair are but wind.
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
27 Truly ye spread a net for the fatherless; Ye dig a pit for your friend.
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
28 Look now upon me, I pray you; For to your very face can I speak falsehood?
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
29 Return, I pray, and let there be no unfairness; Yea, return; —still is my cause righteous.
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
30 Is there iniquity on my tongue? Cannot my taste discern what is sinful?
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?

< Job 6 >