< Job 5 >

1 Call now, see if any will answer thee! And to which of the holy ones wilt thou look?
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
2 Verily grief destroyeth the fool, And wrath consumeth the weak man.
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
3 I have seen an impious man taking root, But soon I cursed his habitation.
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
4 His children are far from safety; They are oppressed at the gate, and there is none to deliver them.
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
5 His harvest the hungry devour, Carrying it even through the thorns; And a snare gapeth after his substance.
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
6 For affliction cometh not from the dust, Nor doth trouble spring up from the ground;
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
7 Behold, man is born to trouble, As the sparks fly upward.
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
8 I would look to God, And to God would I commit my cause,
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
9 Who doeth great things and unsearchable; Yea, marvellous things without number;
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
10 Who giveth rain upon the earth, And sendeth water upon the fields;
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
11 Who placeth the lowly in high places, And restoreth the afflicted to prosperity;
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
12 Who disappointeth the devices of the crafty, So that their hands cannot perform their enterprises;
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
13 Who taketh the wise in their own craftiness, And bringeth to nought the counsel of the artful.
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
14 They meet with darkness in the daytime; They grope at noon as if it were night.
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
15 So he saveth the persecuted from their mouth; The oppressed from the hand of the mighty.
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
16 So the poor hath hope, And iniquity stoppeth her mouth.
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
17 Behold, happy is the man whom God correcteth; Therefore despise not thou the chastening of the Almighty.
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
18 For he bruiseth, and bindeth up; He woundeth, and his hands make whole.
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
19 In six troubles will he deliver thee; Yea, in seven shall no evil touch thee.
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
20 In famine he will redeem thee from death, And in war from the power of the sword.
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
21 Thou shalt be safe from the scourge of the tongue, And shalt not be afraid of destruction, when it cometh.
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
22 At destruction and famine thou shalt laugh, And of the wild beasts of the land shalt thou not be afraid.
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
23 For thou shalt be in league with the stones of the field; Yea, the beasts of the forest shall be at peace with thee.
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
24 Thou shalt find that thy tent is in peace; Thou shalt visit thy dwelling, and not be disappointed.
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
25 Thou shalt see thy descendants numerous, And thine offspring as the grass of the earth.
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
26 Thou shalt come to thy grave in full age, As a shock of corn gathered in its season.
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
27 Lo! this we have searched out; so it is: Hear it, and lay it up in thy mind!
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”

< Job 5 >