< Job 42 >
1 Then Job answered Jehovah, and said:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
2 I know that thou canst do every thing, And that no purpose of thine can be hindered.
“Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
3 Who is he that darkeneth counsel by words without knowledge? Thus have I uttered what I understood not; Things too wonderful for me, which I knew not:
Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
4 Hear thou, then, I beseech thee, and I will speak! I will ask thee, and do thou instruct me!
“Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
5 I have heard of thee by the hearing of the ear; But now hath mine eye seen thee.
Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako, lakini sasa macho yangu yamekuona.
6 Wherefore I abhor myself, And repent in dust and ashes.
Kwa hiyo najidharau mwenyewe, na kutubu katika mavumbi na majivu.”
7 And when Jehovah had spoken these words unto Job, he said to Eliphaz the Temanite: “My wrath is kindled against thee, and against thy two friends; for ye have not spoken concerning me that which is right, as hath my servant Job.
Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.
8 Take ye, therefore, seven bullocks and seven rams, and go to my servant Job, and offer for yourselves a burnt-offering, and my servant Job shall pray for you; for to him alone will I have regard; that I deal not with you according to your folly. For ye have not spoken concerning me that which is right, as hath my servant Job.”
Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.”
9 So Eliphaz the Temanite, and Bildad the Shuhite, and Zophar the Naamathite, went and did as Jehovah commanded them; and Jehovah had regard to Job.
Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.
10 And Jehovah turned the captivity of Job, when he prayed for his friends, and Jehovah gave him twice as much as he had before.
Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.
11 Then came to him all his brethren, and all his sisters, and all his former acquaintances, and ate bread with him in his house; and condoled with him, and comforted him over all the evil which Jehovah had brought upon him; and every one gave him a piece of money [[a kesita]], and every one a ring of gold.
Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
12 Thus Jehovah blessed the latter end of Job more than the beginning; for he had fourteen thousand sheep, six thousand camels, a thousand yoke of oxen, and a thousand she-asses.
Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja.
13 He had also seven sons, and three daughters.
Tena alikuwa na wana saba na binti watatu.
14 And he called the name of the first Jemima, of the second Kezia, and of the third Kerenhappuch.
Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki.
15 And in all the land were no women found so fair as the daughters of Job; and their father gave them an inheritance among their brethren.
Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.
16 And Job lived after this a hundred and forty years, and saw his sons, and his sons' sons, even four generations.
Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne.
17 Then Job died, being old and satisfied with days.
Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.