< Job 40 >

1 Moreover Jehovah spake to Job, and said:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Will the censurer of the Almighty contend with him? Will the reprover of God answer?
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Then Job answered Jehovah, and said:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Behold, I am vile! what can I answer thee? I will lay my hand upon my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Once have I spoken, but I will not speak again; Yea, twice, but I will say no more.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Then spake Jehovah to Job out of the whirlwind, and said:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Gird up now thy loins like a man! I will ask thee, and do thou instruct me!
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Wilt thou even disannul my right? Wilt thou condemn me, that thou mayst be righteous?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Hast thou an arm like God's? Or canst thou thunder with thy voice like him?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Deck thyself with grandeur and majesty, And array thyself in splendor and glory!
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Send forth the fury of thy wrath! Look upon every proud one, and abase him!
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Look upon every proud one, and bring him low; Yea, tread down the wicked in their place!
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Hide them in the dust together; Shut up their faces in darkness!
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Then, indeed, will I give thee the praise, That thine own right hand can save thee.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Behold the river-horse, which I have made as well as thyself; He feedeth on grass like the ox.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Behold, what strength is in his loins! And what force in the muscles of his belly!
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 He bendeth his tail, like the cedar, And the sinews of his thighs are twisted together.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones are pipes of brass, And his limbs are bars of iron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He is chief among the works of God; He that made him gave him his sword.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 For the mountains supply him with food, Where all the beasts of the field play.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 He lieth down under the lote-plants, In the covert of reeds, and in the fens.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 The lote-plants cover him with their shadow, And the willows of the brook compass him about.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Lo! the stream overfloweth, but he starteth not; He is unmoved though Jordan rush forth even to his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Can one take him before his eyes, Or pierce his nose with hooks?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >