< Job 40 >
1 Moreover Jehovah spake to Job, and said:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Will the censurer of the Almighty contend with him? Will the reprover of God answer?
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Then Job answered Jehovah, and said:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Behold, I am vile! what can I answer thee? I will lay my hand upon my mouth.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Once have I spoken, but I will not speak again; Yea, twice, but I will say no more.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Then spake Jehovah to Job out of the whirlwind, and said:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Gird up now thy loins like a man! I will ask thee, and do thou instruct me!
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Wilt thou even disannul my right? Wilt thou condemn me, that thou mayst be righteous?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Hast thou an arm like God's? Or canst thou thunder with thy voice like him?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Deck thyself with grandeur and majesty, And array thyself in splendor and glory!
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Send forth the fury of thy wrath! Look upon every proud one, and abase him!
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Look upon every proud one, and bring him low; Yea, tread down the wicked in their place!
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Hide them in the dust together; Shut up their faces in darkness!
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Then, indeed, will I give thee the praise, That thine own right hand can save thee.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Behold the river-horse, which I have made as well as thyself; He feedeth on grass like the ox.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Behold, what strength is in his loins! And what force in the muscles of his belly!
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 He bendeth his tail, like the cedar, And the sinews of his thighs are twisted together.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 His bones are pipes of brass, And his limbs are bars of iron.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 He is chief among the works of God; He that made him gave him his sword.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 For the mountains supply him with food, Where all the beasts of the field play.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 He lieth down under the lote-plants, In the covert of reeds, and in the fens.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 The lote-plants cover him with their shadow, And the willows of the brook compass him about.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Lo! the stream overfloweth, but he starteth not; He is unmoved though Jordan rush forth even to his mouth.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Can one take him before his eyes, Or pierce his nose with hooks?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?