< Job 37 >
1 At this my heart trembleth, And leapeth out of its place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Hear, O hear, the thunder of his voice, And the noise which goeth forth from his mouth!
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 He directeth it under the whole heaven, And his lightning to the ends of the earth.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 After it the thunder roareth; He thundereth with his voice of majesty, And restraineth it not, when his voice is heard.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 God thundereth with his voice marvellously; Great things doeth he, which we cannot comprehend.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 For he saith to the snow, “Be thou on the earth!” To the shower also, even the showers of his might.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 He sealeth up the hand of every man, That all men whom he hath made may acknowledge him.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Then the beasts go into dens, And abide in their caverns.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Out of the south cometh the whirlwind, And cold out of the north.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 By the breath of God ice is formed, And the broad waters become narrow,
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Yea, with moisture he burdeneth the clouds; He spreadeth abroad his lightning-clouds.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 They move about by his direction, To execute all his commands throughout the world;
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Whether he cause them to come for punishment, Or for the land, or for mercy.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Give ear to this, O Job! Stand still, and consider the wondrous works of God!
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Dost thou know when God gave commandment to them, And caused the lightning of his cloud to flash?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Dost thou understand the balancing of the clouds, The wondrous works of Him that is perfect in knowledge?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 How thy garments become warm, When he maketh the earth still by the south wind?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Canst thou like him spread out the sky, Which is firm like a molten mirror?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Teach us what we shall say to him! For we cannot set in order our words by reason of darkness.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Shall it be told him that I would speak? Shall a man speak, that he may be consumed?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 For now men do not look upon the light, When it is bright in the skies, When the wind hath passed over them, and made them clear.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 From the north cometh gold; But with God is terrible majesty!
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 The Almighty, we cannot find him out; Great is he in power and justice, Abundant in righteousness; he doth not oppress.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Therefore let men fear him! Upon none of the wise in heart will he look.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”