< Job 33 >

1 Hear, therefore, my discourse, I pray thee, O Job! And attend unto all my words!
Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
2 Behold, I am opening my mouth; My tongue is now speaking in my palate.
Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
3 My words shall be in the uprightness of my heart; My lips shall utter knowledge purely.
Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
4 The spirit of God made me, And the breath of the Almighty gave me life.
Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
5 If thou art able, answer me; Set thyself in array against me; stand up!
Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
6 Behold, I, like thee, am a creature of God; I also was formed of clay.
Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
7 Behold, my terror cannot dismay thee, Nor can my greatness be heavy upon thee.
Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
8 Surely thou hast said in my hearing, I have heard the sound of thy words:
Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
9 “I am pure, and without transgression; I am clean, and there is no iniquity in me.
'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
10 Behold, He seeketh causes of hostility against me; He regardeth me as his enemy.
Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
11 He putteth my feet in the stocks; He watcheth all my paths.”
Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
12 Behold, in this thou art not right; I will answer thee; For God is greater than man.
Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
13 Why dost thou contend with Him? For he giveth no account of any of his doings.
Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
14 For God speaketh once, Yea, twice, when man regardeth it not.
Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
15 In a dream, in a vision of the night, When deep sleep falleth upon men, In slumber upon the bed;
Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
16 Then openeth he the ears of men, And sealeth up for them admonition;
basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
17 That he may turn man from his purpose, And hide pride from man.
kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
18 Thus he saveth him from the pit, Yea, his life from perishing by the sword.
Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
19 He is chastened also with pain upon his bed, And with a continual agitation of his bones,
Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
20 So that his mouth abhorreth bread, And his taste the choicest food;
ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
21 His flesh is consumed, that it cannot be seen, And his bones, that were invisible, are naked;
Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
22 Yea, his soul draweth near to the pit, And his life to the destroyers.
Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
23 But if there be with him a messenger, An interpreter, one of a thousand, Who may show unto man his duty,
Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
24 Then will God be gracious to him, and say, “Save him from going down to the pit: I have found a ransom.”
na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
25 His flesh shall became fresher than a child's; He shall return to the days of his youth.
kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
26 He shall pray to God, and he will be favorable to him, And permit him to see his face with joy, And restore unto man his righteousness.
Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
27 He shall sing among men, and say, “I sinned; I acted perversely; Yet hath he not requited me for it:
Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
28 He hath delivered me from going down to the pit, And my life beholdeth the light.”
Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
29 Lo! all these things doeth God Time after time with man,
Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
30 That he may bring him back from the pit, That he may enjoy the light of the living.
kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
31 Mark well, O Job! hearken to me! Keep silence, and I will speak.
Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
32 Yet if thou hast any thing to say, answer me! Speak! for I desire to pronounce thee innocent.
Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
33 But if not, do thou listen to me! Keep silence, and I will teach thee wisdom!
Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”

< Job 33 >