< Job 32 >
1 So these three men ceased to answer Job, because he was righteous in his own eyes.
Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
2 Then was kindled the wrath of Elihu, the son of Barachel, the Buzite, of the family of Ram; against Job was his wrath kindled, because he accounted himself righteous rather than God.
Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
3 Against his three friends also was his wrath kindled, because they had not found an answer, and yet had condemned Job.
Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
4 Now Elihu had delayed to reply to Job, because they were older than himself.
Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
5 But when Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, his wrath was kindled.
Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
6 Then spake Elihu, the son of Barachel, the Buzite, and said: I am young, and ye are very old; Therefore I was afraid, And durst not make known to you my opinion.
Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
7 I said, “Days should speak, And the multitude of years should teach wisdom.”
Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
8 But it is the spirit in man, Even the inspiration of the Almighty, that giveth him understanding.
Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
9 Great men are not always wise, Nor do the aged always understand what is right.
Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
10 Therefore, I pray, listen to me: I also will declare my opinion.
“Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
11 Behold, I have waited for your words, I have listened to your arguments, Whilst ye searched out what to say;
Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
12 Yea, I have attended to you; And behold, none of you hath refuted Job, Nor answered his words.
niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
13 Say not, then, “We have found out wisdom; God must conquer him, not man.”
Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
14 He hath not directed his discourse against me, And with speeches like yours will I not answer him.
Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
15 They were confounded! they answered no more! They could say nothing!
“Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
16 I waited, but they spake not; They stood still; they answered no more!
Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
17 Therefore will I answer, on my part; I also will show my opinion.
Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
18 For I am full of matter; The spirit within me constraineth me.
Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
19 Behold, my bosom is as wine that hath no vent; Like bottles of new wine, which are bursting.
ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
20 I will speak, that I may be relieved; I will open my lips and answer.
Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
21 I will not be partial to any man's person, Nor will I flatter any man.
Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
22 For I know not how to flatter; Soon would my Maker take me away.
kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.