< Job 31 >
1 I made a covenant with mine eyes; How then could I gaze upon a maid?
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 For what is the portion appointed by God from above, And the inheritance allotted by the Almighty from on high?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Is not destruction for the wicked, And ruin for the workers of iniquity?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Doth He not see my ways, And number all my steps?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 If I have walked with falsehood, And if my foot hath hasted to deceit,
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 Let him weigh me in an even balance; Yea, let God know my integrity!
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 If my steps have turned aside from the way, And my heart gone after mine eyes, Or if any stain hath cleaved to my hand,
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 Then I may sow, and another eat; And what I plant, may it be rooted up!
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 If my heart hath been enticed by a woman, Or if I have watched at my neighbor's door,
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 Then let my wife grind for another, And let other men lie with her!
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 For this were a heinous crime, Even a transgression to be punished by the judges;
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 Yea, it were a fire that would consume to destruction, And root out all my increase.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 If I have refused justice to my man-servant or maid-servant, When they had a controversy with me,
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 Then what shall I do when God riseth up? And when he visiteth, what shall I answer him?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Did not He that made me in the womb make him? Did not one fashion us in the womb?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 If I have refused the poor their desire, And caused the eyes of the widow to fail;
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 If I have eaten my morsel alone, And the fatherless hath not partaken of it;
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 (Nay, from my youth he grew up with me as with a father, And I have helped the widow from my mother's womb; )
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 If I have seen any one perishing for want of clothing, Or any poor man without covering;
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 If his loins have not blessed me, And he hath not been warmed with the fleece of my sheep;
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 If I have shaken my hand against the fatherless, Because I saw my help in the gate, —
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Then may my shoulder fill from its blade, And my fore-arm be broken from its bone!
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 For destruction from God was a terror to me, And before his majesty I could do nothing.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 If I have made gold my trust, Or said to the fine gold, Thou art my confidence;
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 If I have rejoiced, because my wealth was great, And my hand had found abundance;
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 If I have beheld the sun in his splendor, Or the moon advancing in brightness,
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 And my heart hath been secretly enticed, And my mouth hath kissed my hand,
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 This also were a crime to be punished by the judge; For I should have denied the God who is above.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 If I have rejoiced at the destruction of him that hated me, And exulted when evil came upon him;
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 (Nay, I have not suffered my mouth to sin, By asking with curses his life; )
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 If the men of my tent have not exclaimed, “Who is there that hath not been satisfied with his meat?”
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 The stranger did not lodge in the street; I opened my doors to the traveller.
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 Have I, after the manner of men, hidden my transgression, Concealing my iniquity in my bosom,
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 Then let me be confounded before the great multitude! Let the contempt of families cover me with shame! Yea, let me keep silence! let me never appear abroad!
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 O that there were one who would hear me! Behold my signature! let the Almighty answer me. And let mine adversary write down his charge!
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Truly I would wear it upon my shoulder; I would bind it upon me as a crown.
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 I would disclose to him all my steps; I would approach him like a prince.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 If my land cry out against me, And its furrows bewail together;
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 If I have eaten of its fruits without payment, And wrung out the life of its owners,
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Let thorns grow up instead of wheat, And noxious weeds instead of barley. The words of Job are ended.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.