< Job 3 >
1 At length Job opened his mouth, and cursed the day of his birth.
Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
2 And Job spake and said:
Akasema,
3 Perish the day in which I was born, and the night which said, “A man-child is conceived!”
“Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
4 Let that day be darkness; Let not God seek it from above; Yea, let not the light shine upon it!
Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
5 Let darkness and the shadow of death redeem it; Let a cloud dwell upon it; Let whatever darkeneth the day terrify it!
Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
6 As for that night, let darkness seize upon it; Let it not rejoice among the days of the year; Let it not come into the number of the months!
Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
7 O let that night be unfruitful! Let there be in it no voice of joy;
Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
8 Let them that curse the day curse it, Who are skilful to stir up the leviathan!
Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
9 Let the stars of its twilight be darkened; Let it long for light, and have none; Neither let it see the eyelashes of the morning!
Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
10 Because it shut not up the doors of my mother's womb, And hid not trouble from mine eyes.
kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
11 Why died I not at my birth? Why did I not expire when I came forth from the womb?
Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
12 Why did the knees receive me, And why the breasts, that I might suck?
kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
13 For now should I lie down and be quiet; I should sleep; then should I be at rest,
Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
14 With kings and counsellors of the earth, Who built up for themselves—ruins!
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
15 Or with princes that had gold, And filled their houses with silver;
Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
16 Or, as a hidden untimely birth, I had perished; As infants which never saw the light.
Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
17 There the wicked cease from troubling; There the weary are at rest.
Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
18 There the prisoners rest together; They hear not the voice of the oppressor.
Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
19 The small and the great are there, And the servant is free from his master.
Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
20 Why giveth He light to him that is in misery, And life to the bitter in soul,
Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
21 Who long for death, and it cometh not, And dig for it more than for hid treasures;
ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
22 Who rejoice exceedingly, Yea, exult, when they can find a grave?
Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
23 Why is light given to a man from whom the way is hid, And whom God hath hedged in?
Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
24 For my sighing cometh before I eat, And my groans are poured out like water.
Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
25 For that which I dread overtaketh me; That at which I shudder cometh upon me.
Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
26 I have no peace, nor quiet, nor respite: Misery cometh upon me continually.
Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”