< Job 3 >
1 At length Job opened his mouth, and cursed the day of his birth.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 And Job spake and said:
Kisha akasema:
3 Perish the day in which I was born, and the night which said, “A man-child is conceived!”
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Let that day be darkness; Let not God seek it from above; Yea, let not the light shine upon it!
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Let darkness and the shadow of death redeem it; Let a cloud dwell upon it; Let whatever darkeneth the day terrify it!
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 As for that night, let darkness seize upon it; Let it not rejoice among the days of the year; Let it not come into the number of the months!
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 O let that night be unfruitful! Let there be in it no voice of joy;
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Let them that curse the day curse it, Who are skilful to stir up the leviathan!
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Let the stars of its twilight be darkened; Let it long for light, and have none; Neither let it see the eyelashes of the morning!
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 Because it shut not up the doors of my mother's womb, And hid not trouble from mine eyes.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Why died I not at my birth? Why did I not expire when I came forth from the womb?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Why did the knees receive me, And why the breasts, that I might suck?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 For now should I lie down and be quiet; I should sleep; then should I be at rest,
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 With kings and counsellors of the earth, Who built up for themselves—ruins!
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 Or with princes that had gold, And filled their houses with silver;
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Or, as a hidden untimely birth, I had perished; As infants which never saw the light.
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 There the wicked cease from troubling; There the weary are at rest.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 There the prisoners rest together; They hear not the voice of the oppressor.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 The small and the great are there, And the servant is free from his master.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Why giveth He light to him that is in misery, And life to the bitter in soul,
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 Who long for death, and it cometh not, And dig for it more than for hid treasures;
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Who rejoice exceedingly, Yea, exult, when they can find a grave?
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 Why is light given to a man from whom the way is hid, And whom God hath hedged in?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 For my sighing cometh before I eat, And my groans are poured out like water.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 For that which I dread overtaketh me; That at which I shudder cometh upon me.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 I have no peace, nor quiet, nor respite: Misery cometh upon me continually.
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”