< Job 16 >
1 But Job answered and said:
Kisha Ayubu akajibu:
2 Of such things as these I have heard enough! Miserable comforters are ye all!
“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
3 Will there ever be an end to words of wind? What stirreth thee up, that thou answerest?
Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
4 I also might speak like you, If ye were now in my place; I might string together words against you, And shake my head at you.
Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
5 I would strengthen you with my mouth, And the consolation of my lips should sustain you.
Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
6 If I speak, my grief is not assuaged; And if I forbear, it doth not leave me.
“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
7 For now He hath quite exhausted me; Thou hast desolated all my house!
Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
8 Thou hast seized hold of me, and this is a witness against me; My leanness riseth up and testifieth against me to my face.
Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
9 His anger teareth my flesh, and pursueth me; He gnasheth upon me with his teeth; My adversary sharpeneth his eyes upon me.
Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
10 They gape for me with their mouths; In scorn they smite me on the cheek; With one consent they assemble against me.
Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
11 God hath given me a prey to the unrighteous, And delivered me into the hands of the wicked.
Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
12 I was at ease, but he hath crushed me; He hath seized me by the neck, and dashed me in pieces; He hath set me up for his mark.
Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
13 His archers encompass me around; He pierceth my reins, and doth not spare; He poureth out my gall upon the ground.
wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
14 He breaketh me with breach upon breach; He rusheth upon me like a warrior.
Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
15 I have sewed sackcloth upon my skin, And thrust my horn into the dust.
“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
16 My face is red with weeping, And upon my eyelids is deathlike darkness.
Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
17 Yet is there no injustice in my bands. And my prayer hath been pure.
Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
18 O earth! cover not thou my blood, And let there be no hiding-place for my cry!
“Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
19 Yet even now, behold, my witness is in heaven, And he who knoweth me is on high.
Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
20 My friends have me in derision, But my eye poureth out tears unto God.
Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
21 O that one might contend for a man with God, As a man contendeth with his neighbor!
kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
22 For when a few years shall have passed, I shall go the way whence I shall not return.
“Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.