< Jeremiah 51 >

1 Thus saith Jehovah: Behold, I will raise up against Babylon, And against them that dwell in the midst of mine adversaries, A destroying wind;
Yahwe asema hivi: Tazama, ninakwenda kuleta upepo wa maangamizi dhidi ya Babeli na dhidi yao waishio ndani ya Leb Kamei.
2 And I will send against Babylon winnowers, And they shall winnow her, and empty her land; For they shall come against her on every side.
Nitawatuma Babeli wageni. Watamtawanya na wataifanya ukiwa nchi yake, maana watakuja kinyume chake kutoka pote siku ya madhara.
3 Against him that bendeth, let the archer bend his bow, And against him that lifteth himself up in his brigandine! And spare ye not her young men; Destroy ye utterly her whole host!
Msiwaache wapiga mishale wakapinda pinde zao; msiwache wakavaa silaha zao. Msiwahifadhi vijana wake wa kiume; litengeni jeshi lake lote kwa maangamizi.
4 Thus shall they fall down slain in the land of the Chaldaeans, And thrust through in her streets.
Maana watu waliojeruhiwa wataanguka katika nchi ya Wakaldayo; waliouawa wataanguka katika mitaa yake.
5 For Israel is not forsaken, nor Judah abandoned of his God, of Jehovah of hosts; For their land is full of guilt against the Holy One of Israel.
Maana Israeli na Yuda hawajaachwa na Mungu wao, na Yahwe wa majeshi, japokuwa nchi yao imejaa na maasi yaliyotendwa kinyume cha Mmoja aliye Mtakatifu wa Israeli.
6 Flee ye out of Babylon, And save ye every man his life, That ye be not cut off in her punishment! For this is the time of Jehovah's vengeance; He will render to her a recompense.
Kimbieni kutoka Babeli; kila mtu na ajiokoe mwenyewe. Msiangamie katika maasi yake. Maana ni wakati wa kisasi cha Yahwe. Atamlipa kwa yote.
7 Babylon has been a golden cup in the hand of Jehovah, That made all the earth drunken; The nations have drunken of her wine, Therefore the nations are mad.
Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yahwe kilichoinywesha nchi yote; mataifa walikunywa mvinyo wake wakawa wendawazimu.
8 Babylon is suddenly fallen, and broken; Howl ye over her; Bring ye balm for her wounds, If so be she may be healed.
Babeli utaanguka ghafla na kuangamizwa. Mwombolezeeni! mpeni dawa kwa maumivu yake; pengine aweza kupona.
9 “We would have healed Babylon, But she cannot be healed. Forsake her, and let us go every one to his own country! For her punishment reacheth to the heavens, And ascendeth even to the skies.”
Tulinuia kumponya Babeli, lakini hajaponywa, haya na tumwache twende, katika nchi yetu. Maana hatia yake imefika juu mbinguni; imerundikwa kufika mawinguni.
10 Jehovah hath brought forth our deliverance; Come ye, and let us declare in Zion The work of Jehovah our God.
Yahwe ametamka kwamba sisi hatuna hatia. Njooni, teseme katika Sayuni matendo ya Yahwe Mungu wetu.'
11 Make sharp the arrows; put on the shields! Jehovah hath roused up the spirit of the kings of the Medes; For his purpose is against Babylon, to destroy it; For this is the vengeance of Jehovah, The vengeance for his temple.
Noweni mishale na kuchukua ngao. Yahwe anaiimiza roho ya mfalme wa Umedi katika mpango wa kuiangamiza Babeli. Hii ni kwa kisasi cha Yahwe, kisasi kwa maangamizi ya hekalu lake.
12 Against the walls of Babylon set up a standard, Make strong the guard, appoint the watchmen, prepare the ambush! For Jehovah deviseth and doeth that which he spake Against the inhabitants of Babylon.
Inueni bendela juu ya kuta za Babeli; wekeni walinzi. Wekeni waangalizi; wekeni askari waviziao ili kumkamata kila akimbiliaye mjini, maana Yahwe atafanya kile alichokipanga. Atafanya alichokisema juu ya wakaao Babeli.
13 O thou that dwellest by great waters, That aboundest in treasures, Thine end is come; The measure of thy rapaciousness is full!
Enyi mwishio kati ya chemchemi nyingi za maji, ninyi mlio na wingi wa hazina, mwisho wenu umefika. upindo wa maisha yenu umepunguzwa.
14 Jehovah of hosts hath sworn by himself, [[saying, ]] Surely I will fill thee with men, as with caterpillars, Who shall raise the war-shout against thee.
Yahwe wa majeshi ameapa kwa maisha yake, 'nitakujaza na adui zako, kama pigo la nzige; watainua kelele za vita juu yako.'
15 He made the earth by his power, He established the world by his wisdom, And by his understanding he spread out the heavens.
Ameifanya dunia kwa nguvu zake; akaiweka dunia mahali kwa hekima yake. Kwa ufahamu wake alizitanda mbingu.
16 When he uttereth his voice there is an abundance of water in the heavens; He causeth clouds to ascend from the ends of the earth; He bringeth the wind from his storehouses.
Anapovuma, kunakuwa na mvumo wa maji mbinguni, maana huleta umande kutoka miisho ya dunia. Hufanya radi kwa ajili ya mvua na kuituma na kuutuma upepo kutoka katika maghala ya nyumba zake.
17 Brutish is every man who hath not this knowledge; By his images is every founder put to shame; For his molten work is deceit; There is no breath in it.
Kila mtu anakuwa kama mnyama asiye na akili; kila mfua chuma ameaibishwa na sanamu zake. Maana mwonekano wake unadanganya; maana hakuna uzima ndani yake.
18 They are vanity, deceptive work; In the time of their punishment shall they perish.
Hazifai, kazi ya wafanya mzaa; wataangamizwa wakati wa kuadhibiwa kwao.
19 Not like them is he who is the portion of Jacob; He is the former of all things, And Israel is his allotted inheritance. Jehovah of hosts is his name.
Lakini Mungu, urithi wa Yakobo, siyo kama hawa, maana yeye ndiye afanyaye vitu vyote. Israeli ni kabila ya urithi wake; Yahwe wa majeshi ni jina lake.
20 Thou hast been to me my battle-hammer, My weapon of war. And with thee I broke in pieces the nations, And with thee I destroyed the kingdoms.
Wewe ni nyundo ya vita yao, silaha ya vita yangu. Kwa wewe nitawaponda mataifa na kuharibu falme.
21 And with thee I broke in pieces the horse and his rider, And with thee I broke in pieces the chariot and its driver.
Kwa wewe nitaponda farasi na wawapandao; kwa wewe nitaponda vibandawazi na madereva wake.
22 With thee I broke in pieces man and woman, And with thee I broke in pieces the old and the young, And with thee I broke in pieces the young man and the maiden.
Kwa wewe nitawafutilia mbali mme na mke; kwa wewe nitafutilia mbali mzee na kijana. Kwa wewe nitafutilia mbali kijana wa kiume na wasichana bikra.
23 With thee I broke in pieces the shepherd and his flock, And with thee I broke in pieces the husbandman and his team; And with thee I broke in pieces prefects and governors.
Kwa wewe nitafutilia mbali wachungaji na makundi yao; kwa wewe nitawafutilia mbali wakulima na jozi zao za kulimia. kwa wewe nitawafutilia mbali watawala na maafsa.
24 But now before your eyes will I repay to Babylon, And to all the inhabitants of Chaldaea, All the evil which they have done in Zion, saith Jehovah.
Maana mbele yako nitamlipa Babeli na wote wakaao Ukaldayo kwa maovu yote waliyoyafanya huko Sayuni - hili ni tamko la Yahwe.
25 O thou destroying mountain, that destroyest the whole earth, Behold, I am against thee, saith Jehovah! And I will stretch out my hand against thee, And roll thee down from the rocks, And make thee a burnt mountain,
Tazama, mimi ni kinyume chako, ewe mlima, wewe unayewaharibu watu wengine - hili ni tamko la Yahwe - kuiharibu dunia yote. Nitakupiga na mikono yangu na kuvingirisha chini kutoka ukingo wa kilima. Kisha nitakufanya mlima ulioteketezwa kabisa kwa moto.
26 So that none shall take from thee a corner-stone, or a foundation-stone; But thou shalt be a perpetual desolation, saith Jehovah.
Hivyo hawatachukua kwako jiwe lolote ili kujengea pembe ya nyumba au msingi; kwani utakuwa ukiwa wa milele - hili ni tamko la Yahwe.
27 Set ye up a standard in the land, Sound a trumpet among the nations; Enlist the nations against Babylon, Call together against her the kingdoms of Ararat, Minni, and Ashchenaz; Appoint captains against her, Cause the horses to come up like the bristled locusts!
Inua bendela ya vita juu ya nchi. Piga tarumbeta katika mataifa. Yaite mataifa yamshambuliye: Ararati, Mini na Ashkenazi. Teua majemedari wa kumshambulia; leta farasi kama nzige warukao.
28 Enlist ye against her the nations, The kings of the Medes, and their prefects, And all their governors, And all the lands under their dominion,
Waandae mataifa kumshambulia: wafalme wa Umedi na magavana wao, maafsa wake wote na nchi yake yete.
29 So that the earth shall tremble and quake! For the purpose of Jehovah against Babylon is to be fulfilled, To make the land of Babylon a desolation, without an inhabitant.
Maana nchi itatikisika na kudhoofika, kwa kuwa mipango ya Yahwe inaendelea juu ya Babeli, kuifanya nchi ya Babeli kuwa nchi isiyofaa mahali pasipo na mtu.
30 The mighty men of Babylon refuse to fight; They remain in their stronghold; Their strength hath failed; They have become women; Her habitations are burned; Her bars are broken.
Maaskari wameacha kupigana huko Babeli; wamekaa katika ngome zao. Nguvu zao zimeshindwa; wamekuwa wanawake - nyumba zake zipo motoni, makomeo ya malango yake yamevunjika.
31 Courier runs to meet courier, And messenger to meet messenger, To make known to the king of Babylon, That his city is taken from end to end;
Mjumbe hukimbia ili amwambie mjumbe mwingine, na mtoa habari humwambia mtoa habari mwingine ili amwambie mfalme wa Babeli kwamba mji wake umetwaliwa kutoka mwisho hata mwisho.
32 That the passages are taken, That the reeds are burned with fire, And that the men of war are struck with terror.
Hivyo vivuko katika mito vimekamatwa; adui anaunguza mafunjo ya bwawa, na wapiganaji wa Babeli wamechanganyikiwa.
33 For thus saith Jehovah of hosts, the God of Israel: The daughter of Babylon shall be like a thrashing-floor when it is thrashed; Yet a little while, and the time of harvest for her shall come.
Maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria. Ni muda wa kumkanyaga. Ni kitambo kidogo wakati wa mavuno utakuja juu yake.
34 Nebuchadnezzar, the king of Babylon, hath devoured us; He hath made an end of us; He hath made us empty vessels; He hath swallowed us up like a dragon; He hath filled his maw with our delicacies; He hath cast us out.
Yerusalemu husema, 'Nebukadneza mfalme wa Babeli amenirarua. Amenikausha na amenifanya kuwa mtungi mtupu. Amenimeza kama joka. Alijishibisha kwa chakula changu chema. Amenitupa mbali.'
35 “The violence done to me and to my flesh be upon Babylon!” Shall the inhabitant of Zion say; And, “My blood be upon the inhabitants of Chaldaeans!” shall Jerusalem say.
Wenyeji wa Sayuni watasema, 'Gasia nilizofanyiwa na mwili wangu na ziwe kwa Babeli.' Yerusalem atasema, Damu yangu na iwe juu ya wakaao Ukaldayo.'
36 Therefore, thus saith Jehovah: Behold, I will maintain thy cause, And take vengeance for thee; And I will dry up her sea, And make her springs dry.
Kwa hiyo Yahwe asema hivi: Tazama, nikotayari kulitetea shitaka lako na kuleta kisasi kwa ajili yako. Maana nitayakausha maji ya Babeli na kufanya vyanzo vyake kukauka.
37 And Babylon shall become heaps, The dwelling-place of jackals, An astonishment and a hissing, Without an inhabitant.
Babeli utakuwa rundo la magofu, pango la mbwea, sehemu itishayo, kitu cha kutoa sauti ya nyoka, pasipo na watu.
38 Together shall they roar like lions; They shall yell like lions' whelps.
Wababeli wataunguruma kwa pamoja kama wanasimba. Watanguruma kama watoto wa simba.
39 In their heat I will prepare them a drink, And will make them drunk, so that they shall rejoice, And then sleep an everlasting sleep, And awake no more, saith Jehovah.
wanapopashwa moto kwa hasira, nitawafanyia sherehe; nitawalewesha hata wafurahi, na kisha kulala usingizi usio na mwisho hata wasiamke - hili ni tamko la Yahwe -
40 I will bring them down like lambs to the slaughter, Like rams with he-goats.
nitawapeleka chini kama wanakondoo kwa mchinjaji, kama kondoo dume pamoja na mbuzi majike.
41 How is Sheshach taken! How is the praise of the whole earth fallen! How is Babylon become an astonishment among the nations!
Jinsi Babeli ulivyotekwa! Hivyo fahari ya dunia yote imekamatwa. Jinsi Babeli ulivyofanyika sehemu yenye magofu kati ya mataifa.
42 The sea is come up over Babylon; With the roaring of its waves is she covered.
Bahari imekuja juu ya Babeli! Amefunikwa na mawimbi yavumayo.
43 Her cities have become a desolation, A dry land and a desert, A land in which no man dwelleth, And which no son of man passeth through.
Miji yake imekuwa ukiwa, sehemu kame na nyika, nchi isiyo na watu, na hakuna mtu apitaye hapo.
44 I will punish Bel at Babylon, And bring forth from his mouth that which he hath swallowed, And the nations shall flow to him no more; Even the wall of Babylon shall fall.
Hivyo nitamwadhibu Beli huko Babeli; nitakitoa kinywani mwake alichokimeza, na mataifa hawatamminikia tena pamoja na wazao wao. Kuta za Babeli zitaanguka.
45 Go ye out of her, my people, And save ye every man his life From the fierce anger of Jehovah!
Tokeni kati yake, enyi watu wangu. Kila mmoja wenu aokowe maisha yake kutoka katika hasira ya gadhabu yangu.
46 And let not your heart faint, And fear ye not on account of the rumors which are heard in the land, When in one year a rumor cometh, And after it in another year another rumor, And violence is in the land, Ruler against ruler.
Msiache mioyo yenu ikaogopa au kuhofu habari iliyosikiwa nchini, maana habari itakuja siku moja. Baada yake mwaka unaofuata kutakuwa na habari, na ghasia zitakuwa nchini. Mtawala atakuwa kinyume cha mtawala.
47 Therefore, behold the days come When I will punish the graven images of Babylon, And her whole land shall be confounded; And all her slain shall fall in the midst of her.
Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja nitakapoadhibu sanamu za Babeli. Nchi yake yote itaaibika, na wote waliochinjwa wataanguka ndani yake.
48 Then the heavens shall shout over Babylon, And the earth and all that is therein; For out of the North come spoilers against her, saith Jehovah.
Kisha mbingu na nchi, na vyote vilivyomo ndani yake vitafurahi juu ya Babeli. Maana mwalibifu atamwijia kutoka kaskazini - hili ni tamko la Yahwe.
49 As Babylon caused the slain of Israel to fall, So at Babylon shall fall the slain of all the land.
“Kama Babeli alivyowafanya waliouawa wa Israeli kuanguka, hivyo waliouawa katika nchi yake wataanguka katika Babeli.
50 Ye that have escaped her sword, go! Tarry not! Remember Jehovah afar off, And let Jerusalem come into your mind!
Ondokeni!, manusura wa vita, Msikawiye. Mkumbukeni Yahwe tokea mbali; Yerusalemu na ikumbukwe.
51 We have been confounded, because we have heard reproach; Shame hath covered our faces, For strangers have come into the sanctuaries of the house of Jehovah.
Tumeaibika, maana tumesikia matusi; dhihaka imefunika nyuso zetu, maana wageni wameingia mahali patakatifu pa nyumba ya Yahwe.
52 Therefore, behold, the days come, saith Jehovah, When I will punish her graven images, And through all her land shall the wounded groan.
Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - nitakapoziadhibu sanamu zake, na waliojeruhiwa watanung'unika kwa maumivu katika nchi yake yote.
53 Though Babylon should mount up to the heavens, And make inaccessible the height of her strength, Yet from me shall spoilers come upon her, saith Jehovah.
Maana hata kama Babeli angepanda mbinguni au kujenga ngome zake ndefu, aharibuye kutoka kwangu angemwendea - hili ni tamko la Yahwe.
54 Hark! a cry from Babylon, Of great destruction from the land of the Chaldaeans!
Kelele ya maangamizi ilitoka Babeli, anguko kubwa kutoka nchi ya Wakaldayo.
55 For Jehovah destroyeth Babylon, And bringeth to silence her loud tumult; Their waves roar like great waters; Their tumultuous noise resounds.
Maana Yahwe anaiharibu Babeli. Anaifanya kelele ya sauti yake kuisha. Adui zake wanaunguruma kama mawimbi ya maji mengi; kelele yao imekuwa na nguvu.
56 For the spoiler is come upon her, upon Babylon; And their mighty men are taken, And all their bows are broken; For Jehovah is a God of retribution; He will surely requite.
Maana aharibuye amekuja kinyume chake - kinyume cha Babeli! - na shujaa wake wametekwa. Pinde zao zimevunjwa, maana Yahwe ni Mungu wa kisasi; atatekeleza kisasi hiki.
57 And I will make drunk her princes, and her wise men, Her prefects, and her governors, and her mighty men; And they shall sleep an everlasting sleep, And shall no more awake, saith the King, Whose name is Jehovah of hosts.
Maana nitawafanya wana wafalme wake, wenye hekima wake, maofsa wake, na maaskari wake kulewa, nao watalala usingizi kwa usingizi usioisha na bila kuamka - hili ni tamko la mfalme: Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
58 Thus saith Jehovah of hosts: The broad walls of Babylon shall be razed to the foundations, And her high gates shall be burned with fire; So that nations shall have labored for naught, And kingdoms have wearied themselves for fire.
Yahwe wa majeshi asema hivi: Ukuta mnene wa Babeli utaangushwa kabisa, na malango marefu yataunguzwa. Kisha watu wanaokuja kumsaidia watafanya kazi isiyofaa; kila mataifa wanachojaribu kikifanya kwa ajili yake kitateketezwa kwa moto.”
59 The word which Jeremiah the prophet commanded Seraiah, the son of Neriah, the son of Maaseiah, when he went with Zedekiah, the king of Judah, into Babylon, in the fourth year of his reign. This Seraiah was chief chamberlain.
Hili ndilo neno Yeremia nabii alilomwamru Seraya mwana wa Neria mwana wa Makseya alipokwenda na Sedekia mfalme wa Yuda huko Babeli katika mwaka wa nne wa kutawala kwake. Basi Seraya alikuwa afsa mwandamizi.
60 And Jeremiah wrote all the evil that was to come upon Babylon in one book, all these words that are written concerning Babylon.
Maana Yeremia alikuwa ameandika katika gombo kuhusu madhara yote yeliyokuwa yakienda kutendeka juu ya Babeli - maneno haya yote yaliyokuwa yameandikwa juu ya Babeli
61 And Jeremiah said to Seraiah, When thou comest to Babylon, see that thou read all these words,
Yeremia akamwambia Seraya, “Unapokwenda Babeli, hakikisha unayasoma maneno haya yote.
62 and say, O Jehovah, thou hast spoken against this place to destroy it, so that none shall remain in it, neither man nor beast, but that it shall remain desolate forever!
Nawe utasema, 'Yahwe, wewe! - wewe mwenyewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa. Hapatakuwa na wa kukaa, kwamba ni watu au wanyama. Patakuwa nchi isiyofaa daima.'
63 And when thou hast made an end of reading this book, bind a stone upon it, and cast it into the midst of the Euphrates,
Kisha mtakapomaliza kusoma gombo hili, funga jiwe kubwa juu yake na ulitupe katikati ya Frati.
64 and say: So shall Babylon sink, and shall not rise again from the evil which I bring upon her. And they shall utterly fail. Thus far the words of Jeremiah.
Sema, 'Babeli utazama kama hivi. Hautainuka kwa sababu ya mabaya ninayoyapeleka juu yake, nao wataanguka.” Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.

< Jeremiah 51 >