< Jeremiah 38 >
1 And Shephatiah, the son of Mattan, and Gedaliah, the son of Pashur, and Jucal, the son of Shelemiah, and Pashur, the son of Malchiah, heard the words which Jeremiah spoke to all the people, saying,
Shefatia mwana wa Matani, na Gedalia mwana wa Pashuri, na Yehukali mwana wa Shelemia, na Pashuri mwana wa Malkiya wakasikia kile Yeremia alichokuwa akiwaambia watu wote wakati aliposema,
2 “Thus saith Jehovah: He that remaineth in this city shall die by the sword, by famine, and by pestilence; but he that goeth forth to the Chaldaeans shall live, and he shall retain his life as a prey, and shall live.
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Yeyote akaaye ndani ya mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni, lakini yeyote atakayejisalimisha kwa Wakaldayo ataishi. Atakayeyatoa maisha yake kama nyara, ataishi.’
3 Thus saith Jehovah: This city shall surely be given into the hand of the army of the king of Babylon, and he shall take it.”
Tena hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mji huu kwa hakika utatiwa mikononi mwa jeshi la mfalme wa Babeli, ambaye atauteka.’”
4 Then said the princes to the king, “We beseech thee, let this man be put to death! for thus he weakeneth the hands of the men of war that remain in this city, and the hands of all the people, in speaking such words to them; for this man seeketh not the welfare of this people, but their hurt.”
Ndipo maafisa wakamwambia mfalme, “Mtu huyu imempasa kuuawa. Anawakatisha tamaa askari waliobaki katika mji huu, vivyo hivyo na watu wote pia, kwa ajili ya mambo anayowaambia. Mtu huyu hawatakii mema watu hawa, bali maangamizi yao.”
5 Then Zedekiah the king said, “Behold, he is in your hand; for the king is not one that can do anything in opposition to you.”
Mfalme Sedekia akajibu, “Yeye yuko mikononi mwenu! Mfalme hawezi kufanya lolote kuwapinga ninyi.”
6 Then took they Jeremiah, and cast him into the dungeon of Malchiah, the son of Hammelech, which was in the court of the prison; and they let down Jeremiah with cords. And in the dungeon there was no water, but only mire; and Jeremiah sunk in the mire.
Basi wakamchukua Yeremia na kumtia kwenye kisima cha Malkiya, mwana wa mfalme, kilichokuwa katika ua wa walinzi. Wakamteremsha Yeremia kwa kamba ndani ya kisima. Hakikuwa na maji ndani yake, ila tope tu, naye Yeremia akazama ndani ya matope.
7 And Ebedmelech, the Ethiopian, a eunuch, who was then in the king's house, heard that they had put Jeremiah into the dungeon; and the king was sitting in the gate of Benjamin.
Lakini Ebed-Meleki Mkushi, aliyekuwa afisa katika jumba la kifalme, akasikia kuwa walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya kisima. Wakati mfalme alipokuwa ameketi katika Lango la Benyamini,
8 Then Ebedmelech went forth out of the king's house, and spake to the king, saying,
Ebed-Meleki akatoka nje ya jumba la kifalme na kumwambia,
9 “My lord the king! these men have done evil in all that they have done to Jeremiah the prophet whom they have cast into the dungeon; for he was already almost dead in his place for hunger; for there is no more bread in the city.”
“Mfalme bwana wangu, watu hawa wamefanya uovu kwa yote waliomtendea nabii Yeremia. Wamemtupa ndani ya kisima, mahali ambapo atakufa kwa njaa wakati ambapo hakuna chakula popote katika mji.”
10 Then the king commanded Ebedmelech, the Ethiopian, saying, “Take along with thee thirty men from hence, and take up Jeremiah the prophet out of the dungeon, before he die.”
Basi mfalme akamwamuru Ebed-Meleki Mkushi, akisema, “Chukua watu thelathini kutoka hapa pamoja nawe, mkamtoe nabii Yeremia huko kwenye kisima kabla hajafa.”
11 And Ebedmelech took the men with him, and went into the king's house under the store-room, and took from thence torn rags and worn-out rags, and let them down by cords into the dungeon to Jeremiah.
Basi Ebed-Meleki akawachukua watu pamoja naye, wakaenda mpaka kwenye chumba kilichoko chini ya hazina ndani ya jumba la kifalme. Akachukua matambaa makuukuu pamoja na nguo zilizochakaa kutoka huko, na kumshushia Yeremia kwa kamba ndani ya kisima.
12 And Ebedmelech, the Ethiopian, said to Jeremiah, put now these torn and worn-out rags under thy knuckles under the cords. And Jeremiah did so.
Ebed-Meleki Mkushi akamwambia Yeremia, “Weka haya matambaa makuukuu na hizo nguo zilizochakaa makwapani ili kuzuia kamba.” Yeremia akafanya hivyo,
13 And they drew up Jeremiah with cords, and took him up out of the dungeon; and Jeremiah remained in the court of the prison.
nao wakamvuta juu kwa kamba na kumtoa katika kisima. Yeremia akakaa katika ua wa walinzi.
14 And King Zedekiah sent, and took Jeremiah the prophet to him into the third entrance, which is in the house of Jehovah; and the king said to Jeremiah, “I will ask thee a question; hide nothing from me!”
Ndipo Mfalme Sedekia akatuma watu wamwitie nabii Yeremia wamlete kwake kwenye ingilio la tatu la Hekalu la Bwana. Mfalme akamwambia Yeremia, “Ninataka kukuuliza jambo fulani, usinifiche kitu chochote.”
15 And Jeremiah said to Zedekiah, “When I have told thee, wilt thou not surely put me to death? and if I give thee counsel, thou wilt not hearken to me.”
Yeremia akamwambia Sedekia, “Nikikupa jibu, je, hutaniua? Hata kama nikikupa shauri, wewe hutanisikiliza.”
16 Then King Zedekiah swore to Jeremiah in secret, saying, “As Jehovah liveth, who made for us this soul, I will not put thee to death, neither will I give thee into the hand of these men that seek thy life.”
Lakini Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia kiapo hiki kwa siri, akisema, “Hakika kama aishivyo Bwana, ambaye ametupa pumzi, sitakuua wala sitakutia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wako.”
17 Then said Jeremiah to Zedekiah, “Thus saith Jehovah of hosts, the God of Israel: If thou wilt go forth to the chieftains of the king of Babylon, then shalt thou live; and this city shall not be burned with fire; and thou shalt live, thou and thine house.
Kisha Yeremia akamwambia Sedekia, “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Ikiwa utajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, maisha yako yatasalimika, na mji huu hautateketezwa kwa moto. Pia wewe na jamaa yako mtaishi.
18 But if thou wilt not go forth to the chieftains of the king of Babylon, then shall this city be given into the hand of the Chaldaeans, and they shall burn it with fire, and thou shalt not escape out of their hand.”
Lakini ikiwa hutajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, mji huu utatiwa mikononi mwa Wakaldayo na watauteketeza kwa moto, nawe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao.’”
19 And Zedekiah the king said to Jeremiah, “I am afraid of the Jews who have gone over to the Chaldaeans, lest I should be delivered into their hand, and they should mock me.”
Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia, “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbilia kwa Wakaldayo, kwa kuwa Wakaldayo wanaweza kunitia mikononi mwao, nao wakanitenda vibaya.”
20 And Jeremiah said, “Thou shalt not be delivered up to them. Obey, I beseech thee, the voice of Jehovah in what I speak to thee; so shall it be well with thee, and thou shalt live.
Yeremia akajibu, “Hawatakutia mikononi mwao. Mtii Bwana kwa kufanya kile ninachokuambia. Kisha utafanikiwa na maisha yako yatakuwa salama.
21 But if thou refuse to go forth, this is what Jehovah hath revealed to me.
Lakini ukikataa kujisalimisha, hili ndilo Bwana alilonifunulia:
22 Behold, all the women that are left in the house of the king of Judah shall be brought forth to the chieftains of the king of Babylon, and shall say, 'Thy friends have set thee on, and have prevailed against thee; thy feet are sunk in the mire; they go backward.'
Wanawake wote walioachwa katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda wataletwa mbele ya maafisa wa mfalme wa Babeli. Wanawake hao watakuambia: “‘Walikupotosha na kukushinda, wale rafiki zako uliowaamini. Miguu yako imezama matopeni; rafiki zako wamekuacha.’
23 And all thy wives and thy children shall they bring out to the Chaldaeans, and thou shalt not escape out of their hand, but by the hand of the king of Babylon shalt thou be taken; and thou shalt cause this city to be burned with fire.”
“Wake zako wote na watoto wataletwa na kutiwa mikononi mwa Wakaldayo. Wewe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao. Lakini utatekwa na mfalme wa Babeli, na mji huu utateketezwa kwa moto.”
24 Then said Zedekiah to Jeremiah, “Let no man know of these words, and thou shalt not die.
Kisha Sedekia akamwambia Yeremia, “Usiruhusu mtu yeyote ajue kuhusu haya mazungumzo, la sivyo utakufa.
25 But if the princes shall hear that I have talked with thee, and shall come to thee, and say to thee, 'Tell us, we pray thee, what thou hast said to the king; hide it not from us, and we will not put thee to death; and what the king hath said to thee';
Maafisa wakisikia kwamba nimezungumza nawe, nao wakakujia na kusema, ‘Tuambie kile ulichozungumza na mfalme na kile mfalme alichokuambia, usitufiche au sivyo tutakuua,’
26 then shalt thou say to them, 'I presented my supplication before the king, that he would not cause me to return to the house of Jonathan to die there.'”
basi waambie, ‘Nilikuwa ninamsihi mfalme asinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani nisije nikafia humo.’”
27 Then came all the princes to Jeremiah, and asked him; and he told them according to all those words which the king had commanded. And they said no more to him, for the matter was not known.
Maafisa wote wakamjia Yeremia na kumuuliza, naye Yeremia akawaambia kila kitu mfalme alichomwagiza kusema. Kisha hawakusema lolote zaidi na Yeremia kwa sababu hakuna yeyote aliyesikia mazungumzo yake na mfalme.
28 And Jeremiah remained in the court of the prison to the day when Jerusalem was taken.
Naye Yeremia akabaki katika ua wa walinzi hadi siku Yerusalemu ilipotekwa.