< Jeremiah 25 >
1 The word which came to Jeremiah concerning all the people of Judah in the fourth year of Jehoiakim, the son of Josiah, king of Judah, which was the first year of Nebuchadnezzar, king of Babylon;
Neno likamjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.
2 which Jeremiah the prophet spake to all the people of Judah, and to all the inhabitants of Jerusalem, saying: —
Hivyo nabii Yeremia akawaambia watu wote wa Yuda na wale wote waishio Yerusalemu:
3 From the thirteenth year of Josiah, the son of Amon, king of Judah, even to this day, for three and twenty years, the word of Jehovah hath come to me, and I have spoken to you, rising early and speaking; but ye have not hearkened.
Kwa miaka ishirini na mitatu, kuanzia mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda, hadi siku hii ya leo, neno la Bwana limekuwa likinijia, nami nimesema nanyi mara kwa mara, lakini hamkusikiliza.
4 Also Jehovah hath sent to you all his servants the prophets, rising early and sending them; but ye have not hearkened, nor inclined your ear to hear.
Ingawa Bwana amewatuma watumishi wake wote hao manabii kwenu mara kwa mara, hamkusikiliza wala hamkujali.
5 “Turn ye now,” said they, “every one from your evil way, and from your evil doings, and ye shall dwell in the land which Jehovah gave to you and to your fathers for ever and ever.
Walisema, “Geukeni sasa, kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya na matendo yake maovu, ndipo mtaweza kukaa katika nchi ambayo Bwana aliwapa ninyi na baba zenu milele.
6 And go not after strange gods to serve them, and to worship them, and provoke me not to anger with the work of your hands; and I will do you no hurt.”
Msiifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Msinikasirishe kwa vitu ambavyo mmevitengeneza kwa mikono yenu.”
7 But ye have not hearkened to me, saith Jehovah, that ye might provoke me to anger with the works of your hands to your own hurt.
“Lakini ninyi hamkunisikiliza mimi, tena mkanikasirisha kwa vitu mlivyovitengeneza kwa mikono yenu, nanyi mmejiletea madhara juu yenu wenyewe,” asema Bwana.
8 Therefore thus saith Jehovah of hosts: Because ye have not hearkened to my words,
Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asema hivi: “Kwa sababu hamkuyasikiliza maneno yangu,
9 behold, I will send and take all the nations of the North, saith Jehovah, and Nebuchadnezzar, the king of Babylon, my servant, and will bring them against this land and its inhabitants, and against all these nations round about, and will utterly destroy them, and make them an astonishment, and a hissing, and a perpetual desolation.
nitayaita mataifa yote ya kaskazini na mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli,” asema Bwana. “Nitawaleta waishambulie nchi hii na wakazi wake wote, na dhidi ya mataifa yote yanayowazunguka. Nitawaangamiza kabisa na kuwafanya kitu cha kuchukiwa na kudharauliwa, na kuwa magofu daima.
10 Yea, I will take from them the voice of mirth, and the voice of gladness, the voice of the bridegroom and the voice of the bride, the sound of the mill-stones, and the light of the lamp.
Nitawaondolea sauti ya shangwe na furaha, sauti ya bibi na bwana arusi, sauti ya mawe ya kusagia, na mwanga wa taa.
11 And this whole land shall be a desolation and an astonishment; and these nations shall serve the king of Babylon seventy years.
Nchi hii yote itakuwa ukiwa na isiyofaa kitu, nayo mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babeli kwa miaka sabini.”
12 But when seventy years shall have passed, I will punish the king of Babylon and his nation for their iniquity, saith Jehovah, and the land of the Chaldaeans, and I will make it a perpetual desolation.
“Lakini miaka sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na taifa lake na nchi ya Wakaldayo kwa ajili ya hatia yao,” asema Bwana. “Nitaifanya kuwa ukiwa milele.
13 And I will bring upon that land all my words which I have pronounced against it, all that is written in this book, which Jeremiah hath prophesied against all the nations.
Nitaleta juu ya nchi hiyo mambo yote niliyosema dhidi yake, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki, na kutolewa unabii na Yeremia dhidi ya mataifa yote.
14 For they, even they, shall be brought into subjection to many nations and great kings. I will render to them according to their deeds, and according to the works of their own hands.
Wao wenyewe watakuwa watumwa wa mataifa mengi na wafalme wakuu. Nitawalipizia sawasawa na matendo yao na kazi ya mikono yao.”
15 For thus hath Jehovah, the God of Israel, said to me: Take this cup of the wine of wrath from my hand; and let all the nations to which I shall send thee drink of it.
Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, aliloniambia: “Chukua kutoka mkononi mwangu kikombe hiki kilichojaa divai ya ghadhabu yangu, na kuyanywesha mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
16 Let them drink, and stagger, and become mad because of the sword which I am about to send among them.
Watakapoinywa, watapepesuka na kukasirika sana kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka katikati yao.”
17 So I took the cup from the hand of Jehovah, and gave it to all the nations to drink, to which Jehovah sent me;
Hivyo nikakichukua kikombe kutoka mkononi mwa Bwana, na kuyafanya mataifa yote aliyonituma kwao kukinywa:
18 to Jerusalem and to the cities of Judah, and to the kings thereof, and the princes thereof, to make them a desolation, and an astonishment, and a hissing, and a curse; [[as it is this day.]]
Yaani Yerusalemu na miji ya Yuda, wafalme wake na maafisa wake, kuwafanya magofu na kuwa kitu cha kuchukiza, cha dhihaka na laana, kama walivyo leo;
19 To Pharaoh, king of Egypt, and to his servants, and to his princes, and to all his people,
pia Farao mfalme wa Misri, watumishi wake, maafisa wake na watu wake wote,
20 and all the allied people; and to all the kings of the land of Uz, and to all the kings of the land of the Philistines, and to Askelon, and to Gaza, and to Ekron, and to the remnant of Ashdod;
pia wageni wote walioko huko; wafalme wote wa nchi ya Usi; wafalme wote wa Wafilisti (wale wa Ashkeloni, Gaza, Ekroni na watu walioachwa huko Ashdodi);
21 to Edom, and to Moab, and to the children of Ammon;
Edomu, Moabu na Amoni;
22 and to all the kings of Tyre, and to all the kings of Sidon, and to the kings of the lands which are beyond the sea;
wafalme wote wa Tiro na Sidoni; wafalme wa nchi za pwani ngʼambo ya bahari;
23 to Dedan, and to Tema, and to Buz, and to all that shave the cheek;
Dedani, Tema, Buzi na wote walio maeneo ya mbali;
24 and to all the kings of Arabia, and to all the kings of the allied people who dwell in the desert;
wafalme wote wa Arabuni na wafalme wote wa watu wageni wanaoishi katika jangwa;
25 and to all the kings of Zimri, and to all the kings of Elam, and to all the kings of Media;
wafalme wote wa Zimri, Elamu na Umedi;
26 and to all the kings of the North, those that are near, and those that are afar off with respect to each other, and to all the kingdoms of the earth which are upon the face of the ground; and the king of Sheshach shall drink after them.
na wafalme wote wa pande za kaskazini, wa karibu na wa mbali, mmoja baada ya mwingine; yaani falme zote juu ya uso wa dunia. Baada ya hao wote, mfalme wa Sheshaki atakunywa pia.
27 And say to them, Thus saith Jehovah of hosts, the God of Israel: Drink ye and be drunken, and vomit, and fall to rise no more because of the sword which I am about to send among you.
“Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kunyweni, mlewe na mtapike; angukeni, wala msiinuke tena kwa sababu ya upanga nitakaotuma miongoni mwenu.’
28 And if they refuse to take the cup from thy hand to drink, then say to them, Thus saith Jehovah of hosts: Ye shall surely drink!
Lakini kama wakikataa kupokea kikombe kutoka mikononi mwako na kunywa, waambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Ni lazima mnywe!
29 For behold, upon the city which is called by my name I begin to bring evil; and shall ye go wholly unpunished? Ye shall not go unpunished; for I am about to call the sword upon all the inhabitants of the earth, saith Jehovah of hosts.
Tazama, nimeanza kuleta maafa juu ya mji ulio na Jina langu, na je, kweli ninyi mtaepuka kuadhibiwa? Hamwezi kuepuka kuadhibiwa, kwa maana nitaleta vita juu ya wote waishio duniani, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
30 Therefore, prophesy against them all these words, and say to them: —Jehovah shall roar from on high, From his holy habitation shall he utter his voice; He shall roar aloud against his dwelling-place; A shout like that of vintagers shall he raise Against all the inhabitants of the earth.
“Basi sasa toa unabii kwa maneno haya yote dhidi yao, uwaambie: “‘Bwana atanguruma kutoka juu; atatoa sauti ya ngurumo kutoka makao yake matakatifu na kunguruma kwa nguvu sana dhidi ya nchi yake. Atapiga kelele kama wao wakanyagao zabibu, atapiga kelele dhidi ya wote waishio duniani.
31 An outcry shall reach to the ends of the earth; For Jehovah hath a controversy with the nations; He entereth into judgment with all flesh; The wicked will he give up to the sword, saith Jehovah.
Ghasia zitasikika hadi miisho ya dunia, kwa maana Bwana ataleta mashtaka dhidi ya mataifa; ataleta hukumu juu ya wanadamu wote na kuwaua waovu wote,’” asema Bwana.
32 Thus saith Jehovah of hosts: Behold, evil shall go forth from nation to nation, And a great whirlwind shall be raised up from the extremities of the earth.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Tazama! Maafa yanaenea kutoka taifa moja hadi jingine; tufani kubwa inainuka kutoka miisho ya dunia.”
33 At that day shall the slain of Jehovah lie From one end of the earth to the other end of the earth; They shall not be lamented, nor gathered, nor buried; They shall be dung upon the ground.
Wakati huo, hao waliouawa na Bwana watatapakaa kila mahali, kuanzia mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine. Hawataombolezewa wala kukusanywa au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyoenea juu ya ardhi.
34 Howl, O ye shepherds, and cry! Roll yourselves in the dust, ye leaders of the flock, For your time to be slaughtered has come! And I will scatter you, and ye shall fall like a goodly vessel.
Lieni na kuomboleza, enyi wachungaji, mgaagae mavumbini, ninyi viongozi wa kundi. Kwa maana wakati wenu wa kuchinjwa umewadia; mtaanguka na kuvunjavunjwa kama vyombo vizuri vya udongo.
35 The shepherds shall have no way to flee, Nor the leaders of the flock to escape.
Wachungaji hawatakuwa na mahali pa kukimbilia, viongozi wa kundi hawatapata mahali pa kutorokea.
36 [[Hark!]] the voice of the cry of the shepherds, And the wailing of the leaders of the flock, Because Jehovah layeth waste their pasture!
Sikia kilio cha wachungaji, maombolezo ya viongozi wa kundi, kwa maana Bwana anayaharibu malisho yao.
37 Yea, the peaceful pastures are destroyed Because of the fierce anger of Jehovah.
Makao yao ya amani yataharibiwa kwa sababu ya hasira kali ya Bwana.
38 He hath left, like a lion, his covert; For their land is become desolate, Because of the wrath of the destroying sword, And because of the fierceness of his anger.
Kama simba ataacha pango lake, nchi yao itakuwa ukiwa kwa sababu ya upanga wa mdhalimu, na kwa sababu ya hasira kali ya Bwana Mungu.