< Jeremiah 24 >
1 Jehovah showed me this vision. Behold, two baskets of figs were set before the temple of Jehovah. This was after Nebuchadnezzar, king of Babylon, had carried away captive Jeconiah, the son of Jehoiakim, king of Judah, and the princes of Judah, and the artificers, and the smiths, from Jerusalem, and had led them to Babylon.
Bwana alinionyeshea kitu. Tazama, vikapu viwili vya tini viliwekwa mbele ya hekalu la Bwana. (Maono haya yalitokea baada ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, kumchukua mateka Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, maofisa wa Yuda, mafundi na wafua vyuma kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babeli.)
2 One of the baskets contained very good figs, like those which are first ripe. The other contained very bad figs, so bad that they could not be eaten.
Kikapu kimoja cha tini kilikuwa nzuri sana, kama tini za kwanza zilizoiva, lakini kikapu kingine cha tini zilizokuwa mbaya sana zisizoweza kuliwa.
3 And Jehovah said to me, What seest thou, Jeremiah? And I said: Figs; the good figs, exceedingly good; and the bad, exceedingly bad, so bad that they cannot be eaten.
Bwana akaniambia, “Unaona nini Yeremia?” Nikasema, “Tini. Tini ambazo ni nzuri sana na tini ambazo ni mbaya sana haziwezi kuliwa.”
4 Then came the word of Jehovah to me, saying:
Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,
5 Thus saith Jehovah, the God of Israel: As these good figs, so will I regard the captives of Judah, whom I have sent out of this place into the land of Chaldaea for their good;
“Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi: nitawaangalia mateka wa Yuda kwa manufaa yao, kama vile tini hizi nzuri, nilipowatoa mateka kutoka hapa mpaka nchi ya Wakaldayo.
6 yea, I will set my eyes upon them for good, and I will bring them again to this land; and I will build them up, and not pull them down; and I will plant them, and not pluck them up.
Nitaweka macho yangu kwao wapate mema na kuwarejeshea nchi hii. Nitawajenga, wala sitawaangamiza.
7 And I will give them a heart to know me, that I am Jehovah; and they shall be my people, and I will be their God; for they shall return to me with their whole heart.
Nitawapanda, wala sitawang'oa. Ndipo nitawapa moyo wa kunijua; kwa kuwa mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu na mimi nitakuwa Mungu wao, hivyo watanirudia kwa moyo wao yote.
8 And as the bad figs, which are so bad that they cannot be eaten, saith Jehovah, so will I make Zedekiah, the king of Judah, and his princes, and the residue of Jerusalem, those that are left in this land, and those that dwell in the land of Egypt;
Lakini kama vile tini mbaya ambazo ni hazifai kuliwa - asema Bwana - nitatenda hivi kwa Sedekia, mfalme wa Yuda, pamoja na viongozi wake, na pamoja na wengine wa Yerusalemu ambao wanabaki katika nchi hii au kwenda kukaa katika nchi ya Misri.
9 and I will give them up to oppression and affliction in all the kingdoms of the earth; yea, to be a reproach and a proverb, a taunt and a curse, in all places whither I shall drive them.
Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha, wapate maafa, mbele ya falme zote duniani, aibu na somo kwa mithali, matusi, na laana mahali pote nitakapowafukuza.
10 And I will send the sword, the famine, and the pestilence among them, till they be consumed from the land, which I gave to them and to their fathers.
Nitatuma upanga, njaa, na tauni dhidi yao watapotelea mbali kutoka kwenye nchi niliyowapa wao na baba zao.”