< James 3 >
1 My brethren, be not many teachers, knowing that we shall receive the greater condemnation.
Ndugu zangu, msiwe walimu wengi, kwa maana mnafahamu kwamba sisi tufundishao tutahukumiwa vikali zaidi.
2 For in many things we all offend. If any one offend not in speech, the same is a perfect man, able to bridle the whole body also.
Sisi sote tunajikwaa katika mambo mengi. Ikiwa mtu yeyote hakosei kamwe katika yale anayosema, yeye ni mkamilifu, naye anaweza kuuzuia pia na mwili wake wote.
3 For when we put the bits into the horses' mouths, that they may obey us, we turn about also their whole body.
Tunapotia lijamu kwenye vinywa vya farasi ili kuwafanya watutii, tunaweza kuigeuza miili yao yote.
4 Behold also the ships, which, though they are so great, and driven by fierce winds, are yet turned about with a very small rudder, whithersoever the steersman chooseth.
Au angalia pia meli, ingawa ni kubwa sana, nazo huchukuliwa na upepo mkali, lakini hugeuzwa kwa usukani mdogo sana, kokote anakotaka nahodha.
5 So also the tongue is a little member, and boasteth great things. Behold, how great a forest a little fire kindleth!
Vivyo hivyo ulimi ni kiungo kidogo sana katika mwili, lakini hujivuna majivuno makuu. Fikirini jinsi moto mdogo unavyoweza kuteketeza msitu mkubwa!
6 And the tongue is a fire, a world of iniquity! The tongue among our members is that which defileth the whole body, and setteth on fire the wheel of life, and is itself set on fire by hell. (Geenna )
Ulimi pia ni moto, ndio ulimwengu wa uovu kati ya viungo vya mwili. Ulimi huutia mwili wote wa mtu unajisi na kuuwasha moto mfumo mzima wa maisha yake, nao wenyewe huchomwa moto wa jehanamu. (Geenna )
7 For every kind of beasts and of birds, of creeping things and things in the sea, is tamed and hath been tamed by mankind;
Kwa maana kila aina ya wanyama, ndege, wanyama watambaao na viumbe vya baharini vinafugika na vimefugwa na binadamu,
8 but the tongue can no man tame; it is a restless evil, full of deadly poison.
lakini hakuna mtu awezaye kuufuga ulimi. Ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 Therewith bless we the Lord and Father, and therewith curse we men, who have been made after the likeness of God;
Kwa ulimi tunamhimidi Bwana, yaani Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu walioumbwa kwa mfano wa Mungu.
10 out of the same mouth proceedeth blessing and cursing. My brethren, these things ought not so to be.
Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haistahili kuwa hivyo.
11 Doth a fountain from the same opening send forth sweet water and bitter?
Je, chemchemi yaweza kutoa katika tundu moja maji matamu na maji ya chumvi?
12 Can a fig-tree, my brethren, bear olives, or a vine, figs? Neither can salt water yield fresh.
Je, ndugu zangu, mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Wala chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.
13 Who is wise and endued with knowledge among you P let him show out of a good course of conduct his works in meekness of wisdom.
Ni nani aliye na hekima na ufahamu miongoni mwenu? Basi na aionyeshe hiyo kwa maisha yake mema na kwa matendo yake yaliyotendwa kwa unyenyekevu utokanao na hekima.
14 But if ye have bitter rivalry and strife in your hearts, do not glory and lie against the truth.
Lakini ikiwa mna wivu na ni wenye chuki na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu kwa ajili ya hayo wala msiikatae kweli.
15 This wisdom is not that which descendeth from above, but earthly, sensual, devilish.
Hekima ya namna hiyo haishuki kutoka mbinguni, bali ni ya kidunia, isiyo ya kiroho, na ya kishetani.
16 For where there is rivalry and strife, there is confusion and every evil work.
Kwa maana panapokuwa na wivu na ubinafsi, ndipo penye machafuko na uovu wa kila namna.
17 But the wisdom from above is first pure, then peaceable, gentle, easy to be entreated, full of mercy and good fruits, without partiality, without hypocrisy.
Lakini hekima itokayo mbinguni kwanza ni safi, kisha inapenda amani, tena ni ya upole, iliyo tayari kusikiliza wengine kwa unyenyekevu, iliyojaa huruma na matunda mema, isiyopendelea mtu, tena isiyokuwa na unafiki.
18 And the fruit of righteousness is sown in peace by those who make peace.
Mavuno ya haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.