< Isaiah 48 >
1 Hear this, O house of Jacob! Ye that are called by the name of Israel; Ye that have come forth from the fountain of Judah; Ye that swear by the name of Jehovah, And praise the God of Israel, But not in truth and sincerity!
“Sikilizeni hili, ee nyumba ya Yakobo, ninyi mnaoitwa kwa jina la Israeli, na mnaotoka katika ukoo wa Yuda, ninyi mnaoapa kwa jina la Bwana, mnaomwomba Mungu wa Israeli, lakini si katika kweli au kwa haki;
2 For they call themselves of the holy city, And stay themselves on the God of Israel, Whose name is Jehovah of hosts: —
ninyi mnaojiita raiya wa mji mtakatifu, na kumtegemea Mungu wa Israeli, Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:
3 What hath happened I declared to you long ago; From my mouth it proceeded, and I made it known; On a sudden I effected it, and it came to pass.
Nilitoa unabii mambo ya kwanza tangu zamani, kinywa changu kiliyatangaza na kuyafanya yajulikane; kisha ghafula nikayatenda, nayo yakatokea.
4 Because I knew that thou art obstinate, And that thy neck is a bar of iron, And that thy brow is brass,
Kwa kuwa nalijua jinsi ulivyokuwa mkaidi; mishipa ya shingo yako ilikuwa chuma, kipaji chako cha uso kilikuwa shaba.
5 I declared it to thee long ago; Before it came to pass, I made it known to thee; Lest thou shouldst say, My idol effected it, And my graven image, and my molten image ordained it.
Kwa hiyo nilikuambia mambo haya tangu zamani, kabla hayajatokea nilikutangazia ili usije ukasema, ‘Sanamu zangu zilifanya hayo; kinyago changu cha mti na mungu wangu wa chuma aliyaamuru.’
6 Thou hast heard it; now see it all! And will ye not confess it? From this time I make you hear a new thing, Even a hidden thing, which thou hast not known.
Umesikia mambo haya; yaangalie hayo yote. Je, hutayakubali? “Kuanzia sasa na kuendelea nitakueleza mambo mapya, juu ya mambo yaliyofichika usiyoyajua.
7 It is produced now, and not long ago; Before this day thou hast not heard of it, Lest thou shouldst say, Behold, I knew it.
Yameumbwa sasa, wala si tangu zamani; hukupata kuyasikia kabla ya siku ya leo. Hivyo huwezi kusema, ‘Naam, niliyajua hayo.’
8 Yea, thou heardest it not; yea, thou knewest it not; Yea, it was not disclosed to thee long ago; For I knew that thou wast wholly faithless, And wast called rebellious from thy birth.
Hujayasikia wala kuyaelewa, tangu zamani sikio lako halikufunguka. Ninafahamu vyema jinsi ulivyo mdanganyifu, uliitwa mwasi tangu kuzaliwa kwako.
9 For the sake of my name I will defer my anger, And for the sake of my praise I will restrain it from thee, That I may not utterly cut thee off.
Kwa ajili ya Jina langu mwenyewe ninaichelewesha ghadhabu yangu, kwa ajili ya sifa zangu nimeizuia isikupate, ili nisije nikakukatilia mbali.
10 Behold, I have melted thee, and found no silver; I have tried thee in the furnace of affliction.
Tazama, nimekusafisha, ingawa si kama fedha, nimekujaribu katika tanuru ya mateso.
11 For mine own sake will I do it; For how would my name be blasphemed? And my glory will I not give to another.
Kwa ajili yangu mwenyewe, kwa ajili yangu mwenyewe, nafanya hili. Jinsi gani niliache Jina langu lichafuliwe? Sitautoa utukufu wangu kwa mwingine.
12 Hearken to me, O Jacob, And Israel, whom I have called! I am He, I am the first, and I the last.
“Ee Yakobo, nisikilize mimi, Israeli, ambaye nimekuita: Mimi ndiye; mimi ndimi mwanzo na mwisho.
13 Yea, my hand hath founded the earth, And my right hand hath spread out the heavens; I called them; they stood forth together.
Mkono wangu mwenyewe uliweka misingi ya dunia, nao mkono wangu wa kuume umezitanda mbingu; niziitapo, zote husimama pamoja.
14 Assemble yourselves, all of you, and hear! Who among you hath declared these things? He whom Jehovah loveth will execute his pleasure upon Babylon, And his power upon the Chaldaeans.
“Kusanyikeni, ninyi nyote, msikilize: Ni ipi miongoni mwa hizo sanamu ambayo imetabiri vitu hivi? Watu wa Bwana waliochaguliwa na kuungana watatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli; mkono wa Mungu utakuwa dhidi ya Wakaldayo.
15 I, even I, have spoken; yea, I have called him; I have brought him, and his way shall be prosperous.
Mimi, naam, Mimi, nimenena; naam, nimemwita yeye. Nitamleta, naye atafanikiwa katika lile nililomtuma.
16 Draw near to me, and hear ye this! I spake not in secret from the beginning; And since it began to be, I have been there; And now hath the Lord Jehovah sent me with his spirit.
“Nikaribieni na msikilize hili: “Tangu tangazo la kwanza sikusema kwa siri; wakati litokeapo, nitakuwako hapo.” Sasa Bwana Mwenyezi amenituma, kwa Roho wake.
17 Thus saith Jehovah, thy Redeemer, the Holy One of Israel; I am Jehovah, thy God, who teacheth thee what will profit thee; Who leadeth thee in the way thou shouldst go.
Hili ndilo asemalo Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuiendea.
18 O that thou wouldst hearken to my commandments! Then shall thy peace be as a river, And thy prosperity as the waves of the sea;
Laiti ungesikiliza kwa makini maagizo yangu, amani yako ingekuwa kama mto, haki yako kama mawimbi ya bahari.
19 Then shall thy posterity be as the sand, And the fruit of thy body as the offspring of the sea; Thy name shall not be cut off, nor destroyed before me.
Wazao wako wangekuwa kama mchanga, watoto wako kama chembe zake zisizohesabika; kamwe jina lao lisingefutiliwa mbali, wala kuangamizwa kutoka mbele zangu.”
20 Come ye forth from Babylon, flee ye from the land of the Chaldaeans with the voice of joy! Publish ye this, and make it known; Let it resound to the ends of the earth! Say: “Jehovah hath redeemed his servant Jacob;
Tokeni huko Babeli, kimbieni kutoka kwa Wakaldayo! Tangazeni hili kwa kelele za shangwe na kulihubiri. Lipelekeni mpaka miisho ya dunia; semeni, “Bwana amemkomboa mtumishi wake Yakobo.”
21 They thirst not in the deserts through which he leadeth them; Waters from the rock he causeth to flow for them; He cleaveth the rock, and the waters gush forth.
Hawakuona kiu alipowaongoza kupita jangwani; alifanya maji yatiririke kutoka kwenye mwamba kwa ajili yao; akapasua mwamba na maji yakatoka kwa nguvu.
22 There is no peace, saith Jehovah, for the wicked.”
“Hakuna amani kwa waovu,” asema Bwana.