< Ezekiel 43 >

1 Then he brought me to the gate, even to the gate that looketh toward the east.
Yule mtu kisha akanileta hata kwenye lango lililokuwa linaelekea mashariki.
2 And behold, the glory of the God of Israel came from the east; and the sound thereof was as the sound of great waters, and the earth shone with his glory.
Tazama! Utukufu wa Mungu wa Israeli ukaja kutoka mashariki; sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi, na nchi iling'aa kwa utukufu wake.
3 And the appearance was like the vision which I saw, like the vision which I saw when I came to destroy the city; it was a vision like the vision which I saw at the river Chebar. And I fell upon my face.
Yalikuwa yanalingana na sura ya ono nililolona, kulingana na ono nililokuwa nimeliona wakati alipokuja kuuteketeza mji, na maono yalikuwa kama maono ambayo niliyokuwa nimeyaona Keberi Kanali nikaanguka kifudi fudi.
4 And the glory of Jehovah came into the house by way of the gate, whose prospect was toward the east.
Hivyo utukufu wa Yahwe ukaja kwenye nyumba ya karibu na njia ya lango lililokuwa wazi kwa upande wa magharibi.
5 Then the spirit took me up and brought me into the inner court; and behold, the glory of Jehovah filled the house.
Kisha Roho akanichukua na kunileta kwenye ua wa ndanni. Tazama! Utukufu wa Yahwe ulikuwa umeijaza nyumba.
6 And I heard one speaking to me out of the house, and a man was standing by me.
Mtu alisimama karibu na mimi, na nikamsikia mtu mwingine akizungumza na mimi kutoka kwenye nyumba.
7 And he said to me: Son of man, this is the place of my throne, and the place of the soles of my feet, where I will dwell in the midst of the sons of Israel forever; and the house of Israel shall no more pollute my holy name, neither they nor their kings, by their fornication, and by the dead bodies of their kings in their sepulchres;
Akanambia, “Mwanadamu, hapa ndipo mahali pangu pa enzi na mahali kwa ajili ya ya miguu yangu, ambapo nitaishi kati ya watu wa Israeli milele. Nyumba ya Israeli haitalikufuru tena jina langu takatifu-wao au wafalme wao katika mahali patakatifu pao.
8 in that they set their threshold by my threshold, and their post near my post, so that there was only a wall between me and them, and defiled my holy name by the abominations which they committed; wherefore I have consumed them in my anger.
Hawatalikufuru tena jina langu takatifu kwa kuweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu, na nguzo yao ya lango karibu na nguzo yangu ya lango, bila kitu lakini ukuta kati yangu na wao. Wamelikufuru jina langu kwa matendo yao machafu, hivyo nimewala kwa hasira yangu.
9 Now let them remove far away from me their fornication, and the carcasses of their kings; and I will dwell in the midst of them forever.
Sasa waache waondoe udanganyifu wao na maiti za wafalme wao kutoka kwangu, na nitaishi katikati yao milele.
10 And thou, son of man, show this house to the house of Israel, that they may be ashamed of their iniquities, and that they may measure the pattern.
Mwanadamu, wewe mwenyewe utaiambia nyumba ya Israeli kuhusu nyumba hii hivyo watajiskia aibu ya uovu wao. Wanaweza kutafakari kuhusu haya maelezo.
11 And if they be ashamed of all which they have done, let them know the form of the house and the fashion thereof, and the passages for going out and coming in, and all the forms thereof, and all the statutes thereof, and all the laws thereof, and write it in their sight, that they may keep the whole form thereof, and all the statutes thereof, and do them.
Kwa kuwa wameaibika kwa yote waliyoyafanya, kisha waonyeshe mchoro wa nyumba, maelezo yake, matokeo yake, maingio yake, na mchoro wake, sheria zake zote na kanuni. Kisha andika hivi chini mbele ya macho yao ili waweze kutunza michoro yote na kanuni zake zote, hivyo kama wazitiivo.
12 This is the law of the house. Upon the top of the mountain, all within its limits shall be most holy. Behold, this is the law of the house.
Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba: Kutoka kwenye kilele cha mlima hata mpaka wote unaoizunguka, patakuwa patakatifu sana. Tazama! Hii ndiyo sheria kwa ajili ya nyumba.
13 And these are the measures of the altar by cubits; each cubit being a cubit and a hand-breadth. The bottom shall be a cubit high and a cubit broad; and the border thereof, by the edge thereof round about, shall be a span; and this shall be the outer part of the altar.
Hivi vitakuwa vipimo vya madhabahu katika dhiraa-hiyo dhiraa kuwa dhiraa ya kawaida na urefu wa kiganja. Hivyo mfereji ulio uzunguka madhabahu utakuwa dhiraa moja chini, na upana wake pia utakuwa dhiraa moja. Mpaka wa karibu uizungukayo machinjio shubiri moja. Hii itakuwa kitako cha madhabahu.
14 And from the bottom upon the ground to the lower ledge shall be two cubits, and the breadth one cubit; and from the lesser ledge to the greater ledge shall be four cubits, and the breadth a cubit.
Usawa wa kutoka kwenye mferji hadi kwenye machinijo ya chini ya madhabahu itakuwa dhiraa mbili, na hiyo machinjio yenyewe itakuwa dhiraa moja upana. Kisha kutoka machinjio madogo hadi kwenye machinjio makubwa ya madhabahu, itakuwa dhiraa nne, na machinjio makubwa yatakuwa dhraa moja upana.
15 And the altar shall be four cubits; and from the altar upward shall be four horns.
Meko juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa ni dhiraa nne juu, na kuna pembe nne zilizoelekea juu kwenye meku.
16 And the altar shall be twelve cubits long by twelve broad; square on the four sides thereof.
Meku ina dhiraa kumi na moja urefu na dhiraa kumi na mbili upana, za mraba.
17 And the ledge shall be fourteen cubits long by fourteen broad on the four sides thereof; and the border about it shall be half a cubit; and the bottom thereof shall be a cubit round about; and its steps shall look toward the east.
Mpaka wake ni dhiraa kumi na nne urefu na dhiraa kumi na nne upana pande zake zote nne, na ukingo wake ni nusu dhiraa upana. Mfereji ni dhiraa moja upana kuzuka kote pamoja na ngazi zielekeazo mashariki.”
18 And he said to me, Son of man, thus saith the Lord Jehovah: These are the statutes of the altar, in the day when it is made, to offer burnt-offerings thereon, and to sprinkle blood thereon.
Kisha akanambia, “Mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Hizi ndizo sheria kwa ajili ya madhabahu katika siku watakayoitengeza, kwa ajili kutoa sadaka ya kuteketezwa kwenye hiyo, na kwa jili ya kunyunyiza damu juu yake.
19 To the priests, the sons of Levi, of the race of Zadok, that come near to me, saith the Lord Jehovah, to minister to me, thou shalt give a young bullock for a sin-offering.
Utatoa ng'ombe kutoka kwenye kundi kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya Walawi makuhani ambao ni uzao wa Zadoki, wale wajao karibu nami kunitumikia-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
20 And thou shalt take of the blood thereof, and put it on its four horns, and on the four corners of the ledge, and on the border round about, and thus cleanse and purge it.
Kisha utachukua baadhi ya damu yake na kuiweka juu pembe nne za madhabahu na pande nne za machinjio na kuuzunguka ukingo; utaitakasa na kufanya upatanisho kwa ajili yake.
21 And thou shalt take the bullock of the sin-offering, and it shall be burned in the appointed place of the house, without the sanctuary.
Kisha chukua ng'ombe kama sadaka ya dhambi na iteketezwe katika eneneo lililotengwa la nje ya patakatifu.
22 And on the second day thou shalt offer a he-goat without blemish for a sin-offering; and they shall cleanse the altar, as they cleansed it with the bullock.
Kisha katika siku ya pili utatoa mbuzi dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini kama sadaka ya dhambi; makuhani wataisafisha madhabahu kama walivyoisafisha kwa ng'ombe.
23 And when thou hast made an end of cleansing it, thou shalt offer a young bullock without blemish, and a ram out of the flock without blemish.
Utakapomaliza kusafisha, toa ng'ombe asiyekuwa na dosari kutoka kwenye mifugo na kondoo dume asiyekuwa na dosari kutoka kundini.
24 And thou shalt offer them before Jehovah, and the priests shall cast salt upon them, and offer them up for a burnt-offering to Jehovah.
Watoe mbele ya Yahwe; makuhani watanyunyiza chumvi juu yao na kuwainua juu kama sadaka ya kutekezwa kwa Yahwe.
25 Seven days shalt thou sacrifice daily a goat for a sin-offering; they shall also sacrifice a young bullock, and a ram out of the flock without blemish.
Utaandaa mbuzi dume kama sadaka ya dhambi kila siku kwa mda wa siku saba, na makuhani pia wataandaa ng'ombe asiye na dosari kutoka kwenye kundi na kondoo dume kutoka kwenye kundi.
26 Seven days shall they purge the altar, and purify it, and consecrate themselves.
Wataipatanisha madhabahu kwa siku saba na kuitakasa, wataitakasa kwa njia hii.
27 And when they have finished these days, it shall be that on the eighth day and forward the priests shall present your burnt-offerings and your thank-offerings upon the altar, and I will accept you, saith the Lord Jehovah.
Watamaliza hizi siku saba, na katika siku ya nane na kuendelea itakuwa kwamba makuhani wataandaa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani kwenye madhabahu, ndipo nitakapowakubali-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 43 >