< Ezekiel 37 >

1 The hand of Jehovah was upon me, and he carried me out in the spirit of Jehovah, and set me in the midst of a valley, which was full of bones,
Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu, na akanitoa kwa Roho wa Bwana Yahwe na kuniweka chini katikati ya bonde; lilikuwa limejaa mifupa.
2 and caused me to pass by them round about; and behold, there were very many upon the surface of the valley, and lo, they were very dry.
Kisha akanifanya kupita kati yao kuizunguka pande zote. Tazama! Mingi yao mikubwa ilikuwa katika bonde! Ilikuwa mikavu sana.
3 And he said to me, Son of man, can these bones live? And I answered, O Lord Jehovah, thou knowest!
Akanambia, “Mwanadamu, Je! Hii mifupa inaweza kuishi kinyume?” Hivyo nikasema, “Bwana Yahwe, wajua wewe pekee.”
4 Then he said to me, Prophesy to these dry bones, and say to them, O ye dry bones, hear the word of Jehovah!
Kisha akanambia, “Tabiri juu ya hii mifupa na iambie, 'Mifupa mikavu. Lisikilizeni neno la Yahwe.
5 Thus saith the Lord Jehovah to these bones: Behold, I will cause breath to enter into you, and ye shall live;
Bwana Yahwe asema hivi kwenye hii mifupa: Tazama! nakaribia kuweka pumzi juu yenu, nanyi mtaishi.
6 and I will lay sinews upon you, and will bring up flesh upon you, and cover you with skin, and put breath into you, and ye shall live; and ye shall know that I am Jehovah.
Nitaweka mishipa juu yenu na kuleta nyama juu yenu. Nitawafunika kwa ngozi na kuweka pumzi ndani yenu hivyo mtaishi. Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
7 So I prophesied, as I was commanded; and as I prophesied, a voice was heard, and behold, a shaking, and the bones came together, bone to its bone.
Hivyo nimetoa unabii kama nilivyokuwa nimeamriwa: nimetabiri, tazama, sauti ikaja, iliyokuwa ya mtetememo. Kisha mifupa ikasogeleana pamoja-mfupa juu ya mfupa.
8 And when I looked, behold, there were sinews upon them, and the flesh grew, and the skin covered them above; but there was no breath in them.
Nikatazama na, kumbe, mishipa ilikuwa juu sasa, na nyama ikatoka juu na ngozi ikazifunika. Lakini hapakuwa na pumzi juu yao.
9 Then said he to me, Prophesy to breath, prophesy, O son of man, and say to breath, Thus saith the Lord Jehovah: Come from the four winds, O breath, and breathe upon these slain, that they may live!
Kisha Yahwe akanambia, “Itabirie pumzi, tabiri, mwanadamu, na iambie pumzi, 'Bwana Yahwe asema hivi: Pumzi, hutoka pepo nne, na pumzi juu ya hawa walioawa, hivyo wanaweza kuishi.”'
10 So I prophesied, as he commanded me; and the breath came into them, and they lived and stood on their feet, an exceedingly great host.
Hivyo nimetabiri kama nilivyokuwa nimeamriwa; pumzi ikawajilia na wakaishi. Kisha wakasimama kwa miguu yao, jeshi moja kubwa sana.
11 And he said to me, Son of man, these bones denote the whole house of Israel. Behold, they say, “Our bones are dried, and our hope is lost, and we are cut off.”
Kisha Yahwe akanambia, “Mwanadamu, mifupa hii yote ni ya nyumba ya Israeli. Tazama! Wanasema, 'Mifupa yetu imekauka, na tumaini letu limepotea. Tumekatwa.'
12 Therefore prophesy, and say to them, Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I will open your graves, and cause you to come up out of your graves, O my people, and bring you into the land of Israel.
Kwa hiyo tabiri na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nitayafunua makabiri yenu na kuwapandisha kutoka kwayo, watu wangu. Nitakurudisha hata katika nchi ya Israeli.
13 And ye shall know that I am Jehovah, when I open your graves, and cause you to come up out of your graves, O my people,
Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapo yafunua makaburi yenu na kuwatoa kutoka kwao, watu wangu.
14 and put my breath within you, and ye live, and I place you in your own land; then shall ye know that I, Jehovah, have spoken it, and done it, saith Jehovah.
Nitaweka Roho wangu ndani yenu hivyo mtaishi, na nitawafanya kupumzika katika nchi yenu mtakapojua yakwamba mimi ni Yahwe. Nasema na nitayafanya hayo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
15 And the word of Jehovah came to me, saying:
Kisha neno la Yahwe likanijia, likisema,
16 Son of man, take thee one stick, and write upon it, “For Judah, and for the sons of Israel, his companions”; and take another stick, and write upon it, “For Joseph, the stick of Ephraim, and the whole house of Israel, his companions.”
“Sasa wewe, mwanadamu, chukua fimbo moja kwa ajili yako na andika juu yake, 'Kwa ajili Yuda na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake,' Kisha fimbo nyingine andika juu yake, 'Kwa kuwa Yusufu, tawi la Efraimu, na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake.
17 Then join them one to another into one stick, that they may become one in thy hand.
Walete wote pamoja kwenye fimbo moja, ili wawe kitu kimoja katika mkono wako.
18 And when the sons of thy people say to thee. “Wilt thou not show us what thou meanest by these?”
Wakati watu wako watakapokwambia na kusema, 'Je! hutatuambia haya mambo yako yana maana gani?'
19 say to them, Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I will take the stick of Joseph, which is in the hand of Ephraim, and of the tribes of Israel, his companions, and will unite them and him with the stick of Judah, and make them one stick, and they shall be one in my hand.
kisha waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nalichukua tawi la Yusufu ambalo lipo kwenye mkono wa Efraimu na kabila za Israeli wenzake na kuungana nalo hata kwenye tawi la Yuda, ili kwamba wawe tawi moja, na watakuwa kitu kimoja katika mikono yangu.'
20 And let the sticks whereon thou writest be in thy hand before their eyes;
Shika kwenye mkono wako na matawi uliyoandika mbele ya macho yao.
21 and say thou to them, Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I will take the sons of Israel from among the nations whither they are gone, and will gather them from every side, and bring them into their own land.
Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! nakaribia kuwachukua watu wa Israeli kutoka miongoni mwa mataifa walipoenda. Nitawakusanya kutoka nchi zilizozunguka na nitawaleta kwenye nchi yao.
22 And I will make them one nation in the land, upon the mountains of Israel; and one king shall be king over them all; and they shall no more be two nations, and no more shall they be divided into two kingdoms.
Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi, juu ya milima ya Israeli, na kutakuwa na mfalme mmoja kama mfalme juu yao wote, na hawatakuwa mataifa mawili tena. Hawatagawanyika kwenye falme mbili tena.
23 Neither shall they defile themselves any more with their idols, nor with their abominations, nor with any of their transgressions; but I will save them from all their dwelling-places wherein they have sinned, and will cleanse them; and they shall be my people, and I will be their God.
Kisha hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao, mambo yao yachukizao, au dhambi zao nyingine. Kwa kuwa nitawaokoa kutoka matendo yao ya uongo ambayo wamefanya dhambi, na nitawatakasa, hivyo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
24 And my servant David shall be king over them, and they shall have one shepherd; and they shall walk in my commandments, and observe my statutes, and do them.
Daudi mtumishi wangu atakuwa mfalme juu yao. Hivyo kutakuwa na mchungaji mmoja juu yao wote, na wataishi kulingana na sheria zangu na watazitunza amri zangu na kuzitii.
25 And they shall dwell in the land which I gave to my servant Jacob, wherein your fathers dwelt; they shall dwell therein, and their sons and their son's sons forever; and David, my servant, shall be their prince forever.
Wataishi katika nchi niliwapatia watumishi wangu Yakobo, ambapo baba zenu walipoishi. Wataishi humo milele-wao, watoto wao, na wajukuu zao, kwa Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao milele.
26 And I will make with them a covenant of peace; it shall be an everlasting covenant with them. And I will place them [[in the land]], and multiply them, and set my sanctuary in the midst of them forever.
Nitaweka agano la amani pamoja nao. Litakuwa agano la milele pamoja nao. Nitawaweka na kuwazidisha na kupaweka mahali patakatifu pangu katikati yao milele.
27 And my dwelling-place shall be with them; yea, I will be their God, and they shall be my people;
Maskani yangu yatakuwa pamoja nao; Nitakuwa Mungu wao, na watakuwa watu wangu.
28 and the nations shall know that I, Jehovah, do sanctify Israel, when my sanctuary shall be in the midst of them forevermore.
Kisha mataifa watajua yakwamba mimi ni Yahwe niliyewatenga Israeli, wakati mahali pangu patakatifu patakapokuwa katikati yao milele.”

< Ezekiel 37 >