< Ezekiel 12 >
1 And the word of Jehovah came to me, saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Son of man, thou dwellest in the midst of a rebellious house; they have eyes to see, and see not; they have ears to hear, and hear not; for they are a rebellious house.
“Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi.
3 Therefore, thou son of man, prepare thee stuff for removing from the land; and remove by day in their sight, and remove from thy place to another place before their eyes. It may be they will consider, though they be a rebellious house.
“Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi.
4 And carry forth thy stuff, as stuff for removing, by day in their sight, and go forth at even in their sight, as they that go forth into captivity.
Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni.
5 Before their eyes break thou through the wall, and carry forth thereby.
Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo.
6 In their sight bear it upon thy shoulders, and carry it forth in the twilight. Cover thy face, so that thou see not the ground; for I have made thee a sign to the house of Israel.
Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.”
7 And I did as I was commanded, I carried forth my stuff, as stuff for removing from the land, by day; and in the evening I broke through the wall with my hand; I carried it forth in the twilight; I took it upon my shoulder before their eyes.
Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama.
8 And the word of Jehovah came to me in the morning, and said:
Asubuhi neno la Bwana likanijia kusema:
9 Son of man, hath not the house of Israel, the rebellious house, said to thee, “What doest thou?”
“Mwanadamu, je, nyumba ile ya kuasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’
10 Say to them, Thus saith the Lord Jehovah: This burden concerneth the prince in Jerusalem, and all the house of Israel that is therein.
“Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Neno hili linamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ambao wako huko.’
11 Say, I am your sign. As I have done, so shall it be done to them. They shall remove and go into captivity.
Waambie, ‘Mimi ndiye ishara kwenu.’ “Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Watakwenda uhamishoni kama mateka.
12 And the prince that is among them shall bear upon his shoulder in the twilight, and shall go forth. They shall break through the wall to carry forth thereby; he shall cover his face, that he see not the ground with his eyes.
“Naye mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani mwake kwenye giza la jioni na kuondoka na tundu litatobolewa ukutani kwa ajili yake ili kupitia hapo. Atafunika uso wake ili kwamba asiweze kuiona nchi.
13 I will also spread my net upon him, and he shall be taken in my snare, and I will bring him to Babylon, into the land of the Chaldaeans; yet he shall not see it, though he shall die there.
Nitatandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa kwenye mtego wangu, nitamleta mpaka Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko.
14 And all that are round about him to help him, and all his bands, will I scatter to every wind; and I will draw out the sword after them.
Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote, watumishi wake na majeshi yake yote, nami nitawafuatilia kwa upanga uliofutwa.
15 And they shall know that I am Jehovah, when I shall disperse them among the nations, and scatter them in the countries.
“Wao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote.
16 But I will leave a few men of them from the sword, from the famine, and from the pestilence; that they may declare all their abominations among the heathen, whither they come; and they shall know that I am Jehovah.
Lakini nitawaacha wachache wao waokoke na upanga, njaa na tauni, ili kwamba katika mataifa watakakokwenda waweze kutambua matendo ya machukizo waliotenda. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”
17 And the word of Jehovah came to me, saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
18 Son of man, eat thy bread with quaking, and drink thy water with trembling and with carefulness;
“Mwanadamu, tetemeka wakati ulapo chakula chako, tetemeka kwa hofu wakati unywapo maji yako.
19 and say to the people of the land: Thus saith the Lord Jehovah concerning the inhabitants of Jerusalem in the land of Israel; their bread shall they eat with carefulness, and their water shall they drink with astonishment; that their land may be desolate from all that is therein, because of the violence of them that dwell in it.
Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kuhusu hao wanaoishi Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyangʼanywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo.
20 And the inhabited cities shall be laid waste, and the land shall be desolate, that ye may know that I am Jehovah.
Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.’”
21 And the word of Jehovah came to me, saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
22 Son of man, what meaneth that proverb which ye have in the land of Israel, saying, “The days are delayed, and every vision faileth”?
“Mwanadamu, ni nini hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia?’
23 Therefore say to them, Thus saith the Lord Jehovah: I will make this proverb to cease, and they shall no more use it as a proverb in Israel. But say to them, The days are at hand, and what is declared in every vision.
Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia wakati kila maono yatakapotimizwa.
24 For there shall be no longer any vain vision or deceptive divination within the house of Israel.
Kwa maana hapatakuwepo tena na maono ya uongo wala ubashiri wa udanganyifu miongoni mwa watu wa Israeli.
25 For I am Jehovah; I speak, and the word which I speak shall come to pass; it shall no more be delayed. In your own days, ye rebellious house, will I speak the word and perform it, saith the Lord Jehovah.
Lakini Mimi Bwana nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa maana katika siku zako, wewe nyumba ya kuasi, nitatimiza kila nisemalo, asema Bwana Mwenyezi.’”
26 And the word of Jehovah came to me, saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
27 Son of man, behold, they of the house of Israel say, “The vision which he seeth is for many days to come, and he prophesieth of times that are far off.”
“Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’
28 Therefore say to them, Thus saith the Lord Jehovah: There shall none of my words be deferred any more; what I speak shall be done, saith the Lord Jehovah.
“Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema Bwana Mwenyezi.’”