< Ezekiel 11 >
1 Then the spirit lifted me up, and brought me to the east gate of the house of Jehovah, that looketh toward the east; and behold, at the entrance of the gate were five and twenty men; among whom I saw Jaazaniah, the son of Azur, and Pelatiah, the son of Benaiah, princes of the people.
Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
2 Then said He to me: These are the men that devise mischief, and form evil designs in this city;
Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
3 who say, “The time is not near that we should build houses. This city is the caldron, and we are the flesh.”
Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
4 Therefore, prophesy against them, prophesy, O son of man!
Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
5 And the spirit of Jehovah fell upon me, and he said to me, Speak: Thus saith Jehovah: Thus have ye said, O house of Israel! For I know the things that come into your mind, every one of them.
Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
6 Ye have multiplied your slain in this city, and ye have filled the streets thereof with the slain.
Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
7 Therefore thus saith the Lord Jehovah: Your slain, whom ye have laid in the midst of it, they are the flesh, and this city is the caldron; but you will I bring forth out of the midst of it.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
8 Ye have feared the sword, and the sword will I bring upon you, saith the Lord Jehovah.
Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
9 And I will bring you out of the midst thereof, and deliver you into the hands of strangers, and execute judgments upon you.
Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
10 Ye shall fall by the sword; on the borders of Israel will I judge you, that ye may know that I am Jehovah.
Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
11 This city shall not be your caldron, neither shall ye be the flesh in the midst thereof. On the borders of Israel will I judge you,
Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
12 that ye may know that I am Jehovah, in whose statutes ye have not walked, and whose ordinances ye have not observed, but have done according to the manners of the nations, that are round about you.
Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
13 And it came to pass, when I prophesied, that Pelatiah, the son of Benaiah, died. Then I fell down on my face, and cried with a loud voice, and said, Ah, Lord Jehovah, wilt thou make a full end of the remnant of Israel?
Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
14 And the word of Jehovah came to me, saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
15 Son of man, thy brethren, even thy brethren, the men of thy near kindred, and the whole house of Israel, are they to whom the inhabitants of Jerusalem say, “Remove ye far from Jehovah; to us is the land given in possession!”
“Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
16 Therefore say, Thus saith the Lord Jehovah: Though I have cast them far off among the nations, and scattered them among the countries, yet I will be to them as a sanctuary for a short time in the countries whither they are come.
“Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
17 Therefore say, Thus saith the Lord Jehovah: I will gather you from the nations, and assemble you from the countries where ye have been scattered, and I will give you the land of Israel.
“Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
18 And they shall come thither, and they shall take away from thence all the detestable things thereof, and all the abominations thereof.
“Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
19 And I will give them one heart, and I will put a new spirit within them; and I will take out of them the heart of stone, and will give them a heart of flesh,
Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
20 that they may walk in my statutes, and observe my ordinances, and keep them; and they shall be my people, and I will be their God.
Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
21 But as for them whose heart walketh according to the pleasure of their detestable things and their abominations, I will recompense their way upon their heads, saith the Lord Jehovah.
Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
22 Then did the cherubs lift up their wings, and the wheels were beside them; and the glory of the God of Israel was over them above.
Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
23 And the glory of Jehovah went up from the midst of the city, and stood upon the mountain which is on the east side of the city.
Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
24 Then the spirit took me up, and brought me to Chaldaea, to them of the captivity, in vision, by the spirit of God. And the vision which I had seen went up from me.
Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
25 Then I spake to them of the captivity all the words of Jehovah which he had showed me.
nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.