< Ecclesiastes 10 >
1 Dead flies make the oil of the perfumer loathsome and corrupt; thus doth a little folly weigh down wisdom and honor.
Kama vile nzi waliokufa huacha harufu mbaya kwenye manukato, ndivyo upumbavu kidogo huzidi nguvu hekima na heshima.
2 A wise man's mind is at his right hand; but a fool's mind is at his left.
Moyo wa mwenye hekima huelekea kuume, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
3 Yea, even when the fool walketh in the way, his understanding faileth him, and he saith to every one that he is a fool.
Hata anapotembea barabarani, mpumbavu hukosa ufahamu na kudhihirisha kwa kila mmoja jinsi alivyo mpumbavu.
4 If the anger of a ruler rise up against thee, leave not thy place! for gentleness pacifieth great offences.
Kama hasira ya mtawala ikiwaka dhidi yako, usiache mahali pako, utulivu huweza kuzuia makosa mengi.
5 There is an evil which I have seen under the sun; an error which proceedeth from a ruler.
Kuna ubaya niliouona chini ya jua, aina ya kosa litokalo kwa mtawala:
6 Folly is set in many high stations, and the noble sit in a low place.
Wapumbavu kuwekwa kwenye nafasi nyingi za juu, wakati matajiri hushika nafasi za chini.
7 I have seen servants upon horses, and princes walking as servants on foot.
Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, wakati wakuu wakitembea kwa miguu kama watumwa.
8 He that diggeth a pit shall fall into it; and whoso breaketh down a wall, a serpent shall bite him.
Yeye achimbaye shimo aweza kutumbukia ndani yake, yeyote abomoaye ukuta anaweza kuumwa na nyoka.
9 Whoso removeth stones shall be hurt therewith, and he that cleaveth wood shall be endangered thereby.
Yeyote apasuaye mawe inawezekana yakamuumiza, yeyote apasuaye magogo inawezekana yakamuumiza.
10 If the iron be blunt, and one do not whet the edge, then must he put forth more strength; but an advantage for giving success hath wisdom.
Kama shoka ni butu na halikunolewa, nguvu nyingi zinahitajika, lakini ustadi utaleta mafanikio.
11 If a serpent bite before he is charmed, then there is no advantage to the charmer.
Kama nyoka akiuma kabla ya kufanyiwa uaguzi, mwaguzi hatahitajika tena.
12 The words of a wise man's mouth are gracious; but the lips of a fool are his destruction.
Maneno yatokayo kinywani mwa mtu mwenye hekima yana neema, bali mpumbavu huangamizwa na midomo yake mwenyewe.
13 The beginning of the words of his mouth is folly, and the end of his talk is mischievous madness.
Mwanzoni maneno yake ni upumbavu, mwishoni ni wazimu mbaya,
14 A fool also multiplieth words, though no man knoweth what shall be; and who can tell him what shall be after him?
naye mpumbavu huzidisha maneno. Hakuna yeyote ajuaye linalokuja, ni nani awezaye kueleza ni jambo gani litakalotokea baada yake?
15 The labor of the foolish man wearieth him, because he knoweth not how to go to the city.
Kazi ya mpumbavu humchosha mwenyewe, hajui njia iendayo mjini.
16 Woe to thee, O land, when thy king is a child, and thy princes feast in the morning!
Ole wako, ee nchi ambayo mfalme wako alikuwa mtumwa na ambayo wakuu wako hufanya karamu asubuhi.
17 Happy thou, O land, when thy king is a noble, and thy princes eat in due season, for strength, and not for drunkenness!
Heri wewe, ee nchi ambayo mfalme wako ni wa uzao wenye kuheshimika na ambayo wakuu wako hula chakula kwa wakati unaofaa: ili kupata nguvu na si kwa ajili ya ulevi.
18 By much slothfulness the building decayeth; and by the slackness of the hands the house leaketh.
Kama mtu ni mvivu paa la nyumba huinama, kutokana na mikono milegevu, nyumba huvuja.
19 A feast is made for laughter, and wine makes merry; but money answereth all things.
Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, nao mvinyo hufurahisha maisha, lakini fedha ni jawabu la mambo yote.
20 Curse not the king; no, not in thy thought; and curse not the rich in thy bed-chamber! for a bird of the air shall carry the voice; and that which hath wings shall tell the matter.
Usimshutumu mfalme hata ikiwa ni katika mawazo yako, au kumlaani tajiri katika chumba chako cha kulala, kwa sababu ndege wa angani wanaweza kuchukua maneno yako, naye ndege anayeruka anaweza kutoa taarifa ya yale uliyosema.