< Daniel 12 >
1 And at that time shall Michael arise, the great prince that standeth up for the sons of thy people; and there shall be a time of trouble, such as never was since there was a nation even to that time; and at that time shall thy people be delivered, every one that is found written in the book.
“Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
2 And many of them that sleep in the dust of the earth shall awake, some to everlasting life, and some to shame, to everlasting contempt.
Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
3 And they that are wise shall shine as the brightness of the firmament; and they that turn the many to righteousness, as the stars for ever and ever.
Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
4 But thou, Daniel, shut up these words, and seal this book even to the time of the end. Many shall run eagerly through it, and much knowledge shall be gained.
Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
5 And I Daniel looked, and behold, two others stood there, one on this side of the bank of the river, and the other on that side of the bank of the river.
Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
6 And one of them said to the man clothed in linen, who was upon the waters of the river, How long shall it be to the end of these wonders?
Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
7 And I heard the man clothed in linen, who was upon the waters of the river, and he lifted up his right hand and his left hand to heaven, and swore by Him that liveth forever, that in a time, times, and a half, even when the dispersion of a portion of the holy people should be at an end, all these things should be fulfilled.
Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
8 And I heard but understood not; and I said, My lord, what is the latter end of these things?
Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
9 And he said, Go thy way, Daniel, for the words are closed up and sealed till the time of the end.
Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
10 Many shall be cleansed, and made white, and purified, and the wicked will do wickedly; and none of the wicked will understand, but the wise will understand.
Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
11 And from the time when the daily sacrifice shall be taken away, and the abomination of the destroyer set up, there shall be a thousand two hundred and ninety days.
“Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
12 Happy is he that waiteth and cometh to a thousand three hundred and thirty-five days!
Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
13 But go thou thy way even to the end; for thou shalt rest, and rise up to thy lot at the end of the days.
“Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”