< Acts 16 >

1 And he came to Derbe and Lystra; and lo! a certain disciple was there, named Timothy, the son of a believing Jewess, but whose father was a Greek;
Paulo alifika Derbe na Lustra, ambako aliishi mfuasi mmoja aitwaye Timotheo. Mama yake ambaye pia alikuwa mfuasi, alikuwa Myahudi; lakini baba yake alikuwa Mgiriki.
2 who was well a spoken of by the brethren in Lystra and Iconium.
Timotheo alikuwa na sifa kubwa kati ya wale ndugu wa Lustra na Ikonio.
3 Him Paul wished to go forth with him, and took and circumcised him on account of the Jews who were in those places; for they all knew that his father was a Greek.
Paulo alitaka Timotheo aandamane naye safarini, kwa hiyo alimtahiri. Alifanya hivyo kwa sababu Wayahudi wote walioishi sehemu hizo walijua kwamba baba yake Timotheo alikuwa Mgiriki.
4 And as they journeyed through the cities, they delivered to them for their observance the decrees which had been ordained by the apostles and elders that were at Jerusalem.
Walipokuwa wanapita katika ile miji waliwapa watu yale maagizo yaliyotolewa na mitume na wazee kule Yerusalemu, wakawaambia wayazingatie.
5 The churches therefore were established in the faith, and increased in number daily.
Hivyo, yale makanisa yalizidi kuwa imara katika imani, na idadi ya waumini ikaongezeka kila siku.
6 And having gone through Phrygia and the Galatian country, on being forbidden by the Holy Spirit to preach the word in Asia,
Walipitia sehemu za Frugia na Galatia kwani Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kuhubiri huo ujumbe mkoani Asia.
7 they came to Mysia, and were attempting to go into Bithynia; but the Spirit of Jesus did not permit them.
Walipofika kwenye mipaka ya Musia, walijaribu kuingia mkoani Bithunia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.
8 And passing by Mysia, they came to Troas.
Basi, walipitia Musia, wakaenda moja kwa moja mpaka Troa.
9 And a vision appeared to Paul in the night. There stood a man of Macedonia beseeching him and saying, Come over into Macedonia and help us.
Usiku huo, Paulo aliona ono ambalo alimwona mtu mmoja wa Makedonia amesimama pale na kumwomba: “Vuka, uje Makedonia ukatusaidie.”
10 And when he had seen the vision, we immediately endeavored to go into Macedonia, concluding that the Lord had called us to publish the glad tidings to them.
Mara baada ya Paulo kuona ono hilo, tulijitayarisha kwenda Makedonia bila kukawia, tukiwa na hakika kwamba Mungu ametuita tuwapelekee Habari Njema.
11 And setting sail from Troas, we came with a straight course to Samothrace, and on the day following to Neapolis;
Kutoka Troa, tulisafiri kwa meli moja kwa moja mpaka Samothrake, na kesho yake tukatia nanga Neapoli.
12 and thence to Philippi, which is a chief city of the province of Macedonia, a colony. And we remained in the city some days.
Kutoka huko, tulikwenda mpaka Filipi, mji wa wilaya ya kwanza ya Makedonia, na ambao pia ni koloni la Waroma. Tulikaa katika mji huo siku kadhaa.
13 And on the sabbath-day we went forth out of the gate to a river-side, where was wont to be a place of prayer, and we sat down, and spoke to the women who had assembled.
Siku ya Sabato tulitoka nje ya mji, tukaenda kando ya mto ambapo tulidhani ya kuwa ni mahali pa kusali. Tuliketi, tukaongea na wanawake waliokusanyika mahali hapo.
14 And a certain woman named Lydia, a seller of purple, of the city of Thyatira, who worshipped God, was listening; whose heart the Lord opened to attend to the things which were spoken by Paul.
Miongoni mwa wale waliotusikiliza alikuwa mwanamke mmoja mcha Mungu aitwaye Ludia mwenyeji wa Thuatira, ambaye alikuwa mfanyabiashara ya nguo za kitani za rangi ya zambarau. Bwana aliufungua moyo wake hata akayapokea yale maneno Paulo aliyokuwa anasema.
15 And when she had been baptized, and her household, she besought us, saying, If ye have judged me to be a believer in the Lord, come into my house, and abide. And she constrained us.
Baada ya huyo mama pamoja na jamaa yake kubatizwa, alitualika akisema, “Kama kweli mmeona kwamba mimi namwamini Bwana, karibuni nyumbani kwangu mkakae.” Akatuhimiza twende.
16 And it came to pass, as we were going to the place of prayer, that a certain bond-maid having a soothsaying spirit met us, who brought her masters much gain by soothsaying.
Siku moja, tulipokuwa tunakwenda mahali pa kusali, msichana mmoja aliyekuwa na pepo mwenye uwezo wa kuagua alikutana nasi. Msichana huyo alikuwa anawapatia matajiri wake fedha nyingi kwa uaguzi wake.
17 This woman followed Paul and us, and cried, saying, These men are the servants of the most high God, who announce to you the way of salvation.
Basi, huyo msichana alimfuata Paulo na sisi, akipiga kelele na kusema, “Hawa watu ni watumishi wa Mungu Mkuu. Wanawatangazieni njia ya wokovu.”
18 And this she did for many days. But Paul, being much displeased, turned and said to the spirit, I command thee in the name of Jesus Christ to come out of her. And it came out immediately.
Akawa anafanya hivyo kwa siku nyingi hata siku moja Paulo alikasirika, akamgeukia na kumwambia huyo pepo, “Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu!” Mara huyo pepo akamtoka.
19 But her masters seeing that the hope of their gain was gone, laid hold of Paul and Silas, and dragged them into the market-place to the rulers;
Matajiri wa yule msichana walipoona kwamba tumaini lao la kupata mali limekwisha, waliwakamata Paulo na Sila, wakawaburuta mpaka hadharani, mbele ya wakuu.
20 and having brought them before the magistrates, said, These men are grievously disturbing our city, being Jews;
Wakawashtaki kwa mahakimu wakisema, “Watu hawa ni Wayahudi na wanafanya fujo katika mji wetu.
21 and they teach customs which it is not lawful for us Romans to receive or observe.
Wanafundisha desturi ambazo sisi raia wa Roma haturuhusiwi kuzikubali wala kuzifuata.”
22 And the multitude rose up together against them, and the magistrates, tearing off their clothes, commanded to beat them with rods;
Kundi la watu likajiunga nao, likawashambulia. Wale mahakimu wakawatatulia Paulo na Sila mavazi yao, wakaamuru wapigwe viboko.
23 and when they had laid on them many stripes, they cast them into prison, charging the jailer to keep them safely;
Baada ya kupigwa sana wakatiwa ndani, na askari wa gereza akaamriwa kuwaweka chini ya ulinzi mkali.
24 who having received such a charge, thrust them into the inner prison, and made their feet fast in the stocks.
Kutokana na maagizo hayo, huyo askari aliwaweka katika chumba cha ndani kabisa cha gereza na kuifunga miguu yao kwenye nguzo.
25 But at midnight Paul and Silas praying, were singing praises to God; and the prisoners were listening to them.
Karibu na usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakisali na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwa wanasikiliza.
26 And suddenly there was a great earthquake, so that the foundations of the prison were shaken; and all the doors were immediately opened, and the bands of all were loosed.
Ghafla, kulitokea mtetemeko mkuu wa ardhi ambao uliitikisa misingi ya gereza. Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.
27 And the jailer awakening out of sleep, and seeing the prison-doors open, drew his sword, and was about to kill himself, supposing that the prisoners had escaped.
Askari wa gereza alipoamka na kuiona milango ya gereza imefunguliwa, alidhani kwamba wafungwa wote walikuwa wametoroka na hivyo akauchomoa upanga wake, akataka kujiua.
28 But Paul cried with a loud voice, saying, Do thyself no harm, for we are all here.
Lakini Paulo akaita kwa sauti kubwa: “Usijidhuru mwenyewe kwa maana sisi sote tuko hapa.”
29 Then he called for a light, and sprang in, and fell down trembling before Paul and Silas;
Baada ya kumwita mtu alete taa, huyo askari wa gereza alikimbilia ndani, akajitupa mbele ya miguu ya Paulo na Sila huku akitetemeka kwa hofu.
30 and having brought them out, he said, Sirs, what must I do to be saved?
Halafu aliwaongoza nje, akawauliza, “Waheshimiwa, nifanye nini nipate kuokoka?”
31 And they said, Believe in the Lord Jesus, and thou wilt be saved, and thy household.
Wao wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa pamoja na jamaa yako yote.”
32 And they spoke to him the word of the Lord, and to all that were in his house.
Basi, wakamhubiria neno la Bwana yeye pamoja na jamaa yake.
33 And he took them with him at that hour of the night, and washed their stripes; and he was immediately baptized, himself and all that belonged to him.
Yule askari aliwachukua saa ileile ya usiku akawasafisha majeraha yao, kisha yeye na jamaa yake wakabatizwa papo hapo.
34 And when he had brought them up into his house, he set food before them, and rejoiced with all his house, having become a believer in God.
Halafu akawachukua Paulo na Sila nyumbani kwake, akawapa chakula. Yeye na jamaa yake yote wakafanya sherehe kwa vile sasa walikuwa wanamwamini Mungu.
35 And when it was day, the magistrates sent the sergeants, saying, Release those men.
Kesho yake asubuhi, mahakimu waliwatuma maofisa wao wakisema, “Wafungueni wale watu.”
36 And the jailer reported these words to Paul: The magistrates have sent to release you; now therefore come out, and go in peace.
Yule askari wa gereza alimpasha habari Paulo: “Mahakimu wametuma ujumbe ili mfunguliwe. Sasa mnaweza kutoka na kwenda zenu kwa amani.”
37 But Paul said to them, They have publicly beaten us uncondemned, although we are Romans, and have thrust us into prison; and now do they thrust us out secretly? No; but let them come themselves, and bring us out.
Lakini Paulo alimjibu, “Ati nini? Ingawa hatukuwa na kosa, walitupiga viboko hadharani hali sisi ni raia wa Roma. Tena, walitutia ndani na sasa wanataka kutufungulia kwa siri! Hata kidogo! Ni lazima wao wenyewe waje hapa watufungulie.”
38 And the sergeants reported these words to the magistrates; and they were afraid when they heard that they were Romans.
Hao maofisa waliwapasha habari mahakimu juu ya jambo hilo, nao waliposikia kwamba Paulo na Sila walikuwa raia wa Roma, waliogopa.
39 And they came and besought them; and when they had brought them out, they entreated them to leave the city.
Hivyo, walikwenda kuwataka radhi na baada ya kuwatoa ndani waliwaomba watoke katika mji ule.
40 And when they had come out of the prison, they went into the house of Lydia; and when they saw the brethren, they exhorted them, and departed.
Paulo na Sila walitoka gerezani, wakaenda nyumbani kwa Ludia. Huko walionana na ndugu waumini na baada ya kuwatia moyo wakaondoka.

< Acts 16 >